Isaya 29 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 29:1-24

Ole Wa Mji Wa Daudi

129:1 Isa 22:12-13; 1:14; 2Sam 5:7; Isa 28:1Ole wako, wewe Arieli, Arieli,

mji alimokaa Daudi!

Ongezeni mwaka kwa mwaka,

na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.

229:2 Mao 2:5; Isa 3:26; Eze 43:15Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi,

utalia na kuomboleza,

utakuwa kwangu kama mahali

pa kuwashia moto madhabahuni.

329:3 Lk 19:43-44; 2Fal 25:1Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,

nitakuzunguka kwa minara

na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.

429:4 Isa 8:19; 47:1; 52:2; 26:16; Law 19:31Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini,

utamumunya maneno yako kutoka mavumbini.

Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu,

utanongʼona maneno yako toka mavumbini.

529:5 Isa 17:13; 1The 5:3; Za 55:15; Kum 9:21; Za 78:39; Isa 51:12; Za 103:15Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini,

kundi la wakatili watakuwa

kama makapi yapeperushwayo.

Naam, ghafula, mara moja,

629:6 Mk 13:8; Ufu 6:12; Isa 26:21; Zek 14:1-5; Kut 19:16; Mt 24:7; Za 83:13-15Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja

na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu,

atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.

729:7 Mik 4:11-12; Zek 12:9; Ay 20:8Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli,

yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi,

watakuwa kama ilivyo ndoto,

kama maono wakati wa usiku:

829:8 Za 73:20; Yer 30:16; Isa 17:12-14; Zek 12:3; Isa 54:17kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula,

lakini huamka, bado njaa yake ingalipo,

kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji,

lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu.

Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa

yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.

929:9 Yer 13:13; Isa 63:9; Law 10:9; Yer 4:9; Isa 6:10; 63:6; Za 60:3; Yer 13:13; Isa 51:22Duwaeni na kushangaa,

jifanyeni vipofu wenyewe na msione,

leweni, lakini si kwa mvinyo,

pepesukeni lakini si kwa kileo.

1029:10 2The 2:9-11; Za 69:23; Mik 3:6; Amu 4:21; Isa 44:18; 6:9-10; Rum 11:8Bwana amewaleteeni usingizi mzito:

Ameziba macho yenu (ninyi manabii);

amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).

1129:11 Dan 8:26; Mt 13:11; Isa 28:7; Ufu 5:1-2; Isa 8:16; Dan 12:9Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.” 12Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”

1329:13 Yer 12:2; Kol 2:22; Eze 33:31; Mt 15:8-9; Mk 7:6-7; Isa 58:2; Za 119:70; Yer 14:11Bwana anasema:

“Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao

na kuniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

Ibada yao kwangu inatokana na maagizo

waliyofundishwa na wanadamu.

1429:14 Yer 49:7; Ay 10:16; 5:13; Isa 6:9-10; 1Kor 1:19; Yer 8:9; Isa 6:9-10Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa,

kwa ajabu juu ya ajabu.

Hekima ya wenye hekima itapotea,

nayo akili ya wenye akili itatoweka.”

1529:15 Ay 22:13-14; Eze 8:12; 2Fal 21:16; Ay 22:13; Isa 28:15; Ay 8:3; Za 10:11-13Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu

kumficha Bwana mipango yao,

wafanyao kazi zao gizani na kufikiri,

“Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”

1629:16 Yer 18:6; Rum 9:20-21; Za 94:9; Ay 10:9; Isa 10:15; 45:9; Ay 9:12; Yer 18:6; Mwa 2:7Mnapindua mambo juu chini,

kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi!

Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga,

“Wewe hukunifinyanga mimi?”

Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi,

“Wewe hujui chochote?”

1729:17 Za 84:6; Isa 32:15; 10:25; 2:13; Za 107:33Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba,

na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?

1829:18 Mk 7:37; Za 146:8; Mt 11:5; Lk 7:22; Isa 32:3; Za 107:14Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu,

na katika utusitusi na giza

macho ya kipofu yataona.

1929:19 Za 72:4; 25:9; Isa 5:19; 12:6; 3:15; Yak 2:5; Mt 5:5; 11:29; Mwa 42:26Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana,

wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

2029:20 2Nya 36:16; Isa 28:22; Eze 11:2; Isa 13:11; 59:4; Ay 15:35; Za 7:14Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea,

nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,

2129:21 Amo 5:10-15; Isa 5:23; Hab 1:4; Mit 21:28wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia,

wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama,

na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki

yeye asiye na hatia.

2229:22 Mwa 11:16; Yoe 2:26; Yos 24:3; Sef 3:11; Kut 6:6; Mwa 17:16; Isa 41:8; 51:2Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo:

“Yakobo hataaibishwa tena,

wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.

2329:23 Isa 53:10; 54:1-4; 19:25; 49:20-26; 5:19; Mt 6:9Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao,

kazi ya mikono yangu,

watalitakasa Jina langu takatifu;

wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo,

nao watamcha Mungu wa Israeli.

2429:24 Mit 12:8; Ebr 5:2; Isa 60:16; 42:16; Za 95:10; Isa 28:7; 32:4Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu,

nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”

New International Reader’s Version

Isaiah 29:1-24

The Lord Will Judge Jerusalem

1Jerusalem, how terrible it will be for you!

Ariel, you are the city where David made his home.

The years will come and go.

Keep on celebrating your regular feasts.

2The Lord says, “Ariel, I will surround you.

Jerusalem, I will get ready to attack you.

Your people will mourn.

They will sing songs of sadness.

I will make you like the front of an altar

covered with blood.

3I will be like an army camped against you on all sides.

I will surround you with towers in order to attack you.

I will build my ramps all around you and set up my ladders.

4You will be brought down to the grave.

You will speak from deep down inside the ground.

Your words will be barely heard out of the dust.

Your voice will sound like the voice of a ghost

coming from under the ground.

Your words will sound like a whisper out of the dust.”

5Jerusalem, all your enemies will become like fine dust.

Their terrifying armies will become like straw

that the wind blows away.

All of a sudden, in an instant,

6the Lord who rules over all will come.

He will come with thunder, earthquakes and a lot of noise.

He’ll bring windstorms and rainstorms with him.

He’ll send a blazing fire that will burn up everything.

7Armies from all the nations will fight against Ariel.

They will attack it and its fort.

They’ll surround it completely.

But suddenly those armies will disappear like a dream.

They will vanish like a vision in the night.

8It will be as when a hungry person dreams of eating,

but wakes up still hungry.

It will be as when a thirsty person dreams of drinking,

but wakes up weak and still thirsty.

In the same way, the armies from all the nations

that fight against Mount Zion will disappear.

9People of Jerusalem, be shocked and amazed.

Make yourselves blind so you can’t see anything.

Get drunk, but not from wine.

Be unsteady on your feet, but not because of beer.

10The Lord has made you fall into a deep sleep.

He has closed the eyes of your prophets.

He has covered the heads of your seers so they can’t see.

11For you, this whole vision is like words that are sealed up in a scroll. Suppose you give it to someone who can read. And suppose you say, “Please read this for us.” Then they’ll answer, “I can’t. It’s sealed up.” 12Or suppose you give the scroll to someone who can’t read. And suppose you say, “Please read this for us.” Then they’ll answer, “I don’t know how to read.”

13The Lord says,

“These people worship me only with their words.

They honor me by what they say.

But their hearts are far away from me.

Their worship doesn’t mean anything to me.

They teach nothing but human rules that they have been taught.

14So once more I will shock these people

with many wonderful acts.

I will destroy the wisdom of those who think they are so wise.

I will do away with the cleverness of those who think they are so smart.”

15How terrible it will be for people who try hard

to hide their plans from the Lord!

They do their work in darkness.

They think, “Who sees us? Who will know?”

16They turn everything upside down.

How silly they are to think that potters are like the clay they work with!

Can what is made say to the one who made it,

“You didn’t make me”?

Can the pot say to the potter,

“You don’t know anything”?

17In a very short time, Lebanon will be turned into rich farm lands.

The rich farm lands will seem like a forest.

18At that time those who can’t hear will hear what is read from the scroll.

Those who are blind will come out of gloom and darkness.

They will be able to see.

19Those who aren’t proud will once again find their joy in the Lord.

And those who are in need will find their joy in the Holy One of Israel.

20Those who don’t show any pity will vanish.

Those who make fun of others will disappear.

All those who look for ways to do what is evil will be cut off.

21Without any proof, they claim that a person is guilty.

In court they try to trap

the one who speaks up for others.

By using dishonest witnesses they keep people who aren’t guilty

from being treated fairly.

22Long ago the Lord saved Abraham from trouble. Now he says to Jacob’s people,

“You will not be ashamed anymore.

Your faces will no longer grow pale with fear.

23You will see your children living among you.

I myself will give you those children.

Then you will honor my name.

You will recognize how holy I am.

I am the Holy One of Jacob.

You will have great respect for me.

I am the God of Israel.

24I will give understanding to you

who find yourselves going astray.

You who are always speaking against others

will accept what I teach you.”