Isaya 22 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 22:1-25

Unabii Kuhusu Yerusalemu

122:1 Za 125:2; Yoe 3:2-14; Yos 2:8; Isa 13:1; Yer 48:38; 21:13Neno kuhusu Bonde la Maono:

Nini kinachokutaabisha sasa,

kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?

222:2 Isa 5:14; 32:13; Eze 22:5; Isa 21:5; 10:4; 2Fal 25:3Ewe mji uliojaa ghasia,

ewe mji wa makelele na sherehe!

Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga,

wala hawakufa vitani.

322:3 Isa 13:14; 2Fal 25:6Viongozi wako wote wamekimbia pamoja,

wamekamatwa bila kutumia upinde.

Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja,

mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.

422:4 Mao 1:16; Lk 19:41; Yer 9:1; Eze 21:6; Isa 15:3; Lk 19:41Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami,

niache nilie kwa uchungu.

Usijaribu kunifariji

juu ya maangamizi ya watu wangu.”

522:5 Amo 5:18-20; Es 3:15; Sef 1:15; Isa 2:12; Ay 40:12; 2Sam 22:43; Eze 8:17-18; 13:14; Mao 1:5Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku

ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya

katika Bonde la Maono,

siku ya kuangusha kuta

na ya kupiga kelele mpaka milimani.

622:6 Isa 21:2; 2Fal 16:9; Yer 51:56; 49:35; Za 46:9Elamu analichukua podo,

pamoja na waendesha magari ya vita na farasi.

Kiri anaifungua ngao.

722:7 Yos 15:18; 2Nya 32:1-2Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita,

nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;

822:8 2Nya 32:5; 1Fal 7:2; Isa 2:12ulinzi wa Yuda umeondolewa.

Nawe ulitazama siku ile

silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,

922:9 2Fal 18:17; 2Nya 32:4-5; Wim 4:4; 2Fal 20:20mkaona kuwa Mji wa Daudi

una matundu mengi katika ulinzi wake,

mkaweka akiba ya maji

kwenye Bwawa la Chini.

1022:10 Yer 33:4; 2Nya 32:15; 32:5; Yer 33:4Mlihesabu majengo katika Yerusalemu

nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.

1122:11 Yer 39:4; Neh 3:16; 2Fal 25:4; 19:25; 1Sam 12:24Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili

kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani,

lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza,

au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.

1222:12 Yoe 2:17; Law 13:40; Mik 1:16; Isa 3:24; Yoe 1:9-13Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

aliwaita siku ile

ili kulia na kuomboleza,

kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.

1322:13 Mhu 8:15; Isa 5:12; 21:5; Lk 17:26-29; 1Kor 15:32; 1Sam 25:36; Isa 28:7-8Lakini tazama, kuna furaha na sherehe,

kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo,

kula nyama na kunywa mvinyo!

Mnasema, “Tuleni na kunywa,

kwa kuwa kesho tutakufa!”

1422:14 Eze 24:13; Isa 5:9; 1Sam 2:25; Isa 13:11; 30:13-14; 1Sam 3:14Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”

1522:15 2Fal 6:30; 18:18; Mwa 41:40; Isa 36:3; 1Fal 4:6Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo:

“Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna,

ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:

1622:16 Mt 27:60; Hes 32:42Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa

kujikatia kaburi lako mwenyewe,

ukichonga kaburi lako mahali palipo juu,

na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?

1722:17 Yer 10:18; 13:18; 22:26“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti,

na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.

1822:18 Ay 18:11; Isa 14:19; Mwa 41:43Atakuvingirisha uwe kama mpira

na kukutupa katika nchi kubwa.

Huko ndiko utakakofia,

na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia,

wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!

1922:19 Za 52:5; Lk 16:3Nitakuondoa kutoka kazi yako,

nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.

2022:20 2Fal 18:18“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia. 2122:21 Ay 29:16Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda. 2222:22 1Nya 9:27; Mt 16:19; Ay 12:14; Ufu 3:7; Isa 7:2Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua. 2322:23 Eze 15:3; Zek 10:4; Ezr 9:8; Ay 6:25; 1Sam 2:7-8; Ay 36:7Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake. 24Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”

2522:25 Isa 46:11; Mik 4:4Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 22:1-25

关于耶路撒冷的预言

1以下是关于异象谷22:1 “异象谷”指耶路撒冷。的预言:

为什么你们全都上到房顶呢?

2你们这座充满喧闹、骚动和欢乐的城啊,

你们中间被杀的人既非丧身刀下,

也非死于战场。

3你们的官长都一起逃跑,

一箭未发便束手就缚,

逃到远方的也一同被擒。

4所以,我说:“你们不要管我,

让我痛哭吧!

不要安慰我,

我的同胞都被毁灭了。”

5主——万军之耶和华已经定了日子,

要使异象谷饱受恐慌、

失败和混乱,

城墙被攻破,

哭喊声响彻山间。

6以拦人带着箭袋,

率领战车和骑兵前来,

吉珥人也亮出盾牌。

7你们佳美的山谷中布满战车,

骑兵在你们的城门前列阵。

8主除去了犹大的防卫。

那时,你们寄望于藏在林宫里的兵器。 9你们看见大卫城破口累累,你们储存下池的水, 10数点耶路撒冷城的房屋,把房屋拆掉修补城墙。 11你们又在两道城墙之间建造新的蓄水池,用来盛旧池的水。耶和华从古时已定了这一切,要使这一切发生,但你们既不仰望祂,也不理会祂。

12那日,主——万军之耶和华要你们哭泣哀号,

剃光头发,身披麻衣。

13但你们却欢喜作乐,

宰牛杀羊,喝酒吃肉,说:

“让我们吃喝吧!

因为明天我们就死了。”

14万军之耶和华启示我说:

“你们这罪到死也得不到赦免。

这是主——万军之耶和华说的。”

15主——万军之耶和华吩咐我去见宫廷总管舍伯那,对他说: 16“你在这里做什么?你凭什么在这里为自己挖坟墓,在高处为自己挖坟墓,在磐石上为自己凿安息之所? 17看啊,你这有权有势的人,耶和华必紧紧抓住你,把你猛力抛出去。 18祂必把你揉作一团,像球一样扔到宽阔之地。在那里,你必死亡,你华美的战车也必遭毁灭,你是你主人家的羞辱。” 19耶和华对舍伯那说:“我必解除你的官职,把你从高位上拉下来。

20“到那日,我必召来希勒迦的儿子——我的仆人以利亚敬21给他穿上你的朝服,系上你的腰带,把你的权柄交给他。他必像父亲一样保护耶路撒冷的居民和犹大人。 22我必把大卫家的钥匙放在他的肩头。他开启的,没有人能关;他关闭的,没有人能开。 23我要使他像深嵌在坚固之处的橛子一样稳固,他必给他的家族带来尊荣。 24他的家族及其子孙后代都靠他得荣耀,如同杯子和酒瓶等小器皿挂在一个橛子上。”

25万军之耶和华说:“到那日,牢牢钉在坚固之处的橛子必松动,被砍落在地上,挂在上面的东西必被除掉。这是耶和华说的。”