Isaya 21 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 21:1-17

Unabii Dhidi Ya Babeli

1Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari:

Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini,

mshambuliaji anakuja kutoka jangwani,

kutoka nchi inayotisha.

221:2 1Sam 24:13-16; Mwa 10:22; Za 60:3; Yer 49:34; Isa 22:6; 13:3; Yer 25:25Nimeonyeshwa maono ya kutisha:

Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara.

Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi!

Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.

321:3 Mwa 3:16; Yn 16:2; Ay 14:22; Za 48:6; Isa 26:17; Yer 30:6; Dan 7:28Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu,

maumivu makali ya ghafula yamenishika,

kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.

Nimeduwazwa na lile ninalolisikia,

nimeshangazwa na lile ninaloliona.

421:4 Isa 7:4; 35:4; 13:8; Dan 5:9; Za 55:5Moyo wangu unababaika,

woga unanifanya nitetemeke,

gizagiza la jioni nililolitamani sana,

limekuwa hofu kuu kwangu.

521:5 Yer 25:16, 27; Dan 5:2-5; Isa 5:12; 23:7; Yer 46:3; 1Sam 1:21Wanaandaa meza,

wanatandaza mazulia,

wanakula, wanakunywa!

Amkeni, enyi maafisa,

zitieni ngao mafuta!

621:6 2Fal 9:17Hili ndilo Bwana analoniambia:

“Nenda, weka mlinzi,

na atoe taarifa ya kile anachokiona.

721:7 Amu 6:5; Isa 21:9Anapoona magari ya vita

pamoja na kundi la farasi,

wapanda punda au wapanda ngamia,

na awe macho, awe macho kikamilifu.”

821:8 Mik 7:7; Hab 2:1Naye mlinzi alipaza sauti,

“Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi,

kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.

921:9 Isa 13:19; Ufu 14:8; Dan 5:30; Ufu 18:2; Yer 50:2; Isa 47:11; Yer 51:8Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita

pamoja na kundi la farasi.

Naye anajibu:

‘Babeli umeanguka, umeanguka!

Vinyago vyote vya miungu yake

vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’ ”

1021:10 Yer 51:33; Mt 3:12; Mik 4:13; Isa 27:12; Hab 3:12Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria,

ninawaambia kile nilichokisikia

kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote,

kutoka kwa Mungu wa Israeli.

Unabii Dhidi Ya Edomu

1121:11 Mwa 32:3; 1Nya 1:30; Eze 35:2; Oba 1:1Neno kuhusu Duma:

Mtu fulani ananiita kutoka Seiri,

“Mlinzi, usiku utaisha lini?

Mlinzi, usiku utaisha lini?”

12Mlinzi anajibu,

“Asubuhi inakuja, lakini pia usiku.

Kama ungeliuliza, basi uliza;

bado na urudi tena.”

Unabii Dhidi Ya Arabia

1321:13 Isa 13:1; 2Nya 9:14; Mwa 10:7; 25:3; 1Nya 1:9Neno kuhusu Arabia:

Enyi misafara ya Wadedani,

mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,

1421:14 Mwa 25:15; Ay 6:19leteni maji kwa wenye kiu,

ninyi mnaoishi Tema,

leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.

1521:15 Isa 13:14; 31:8Wanaukimbia upanga,

kutoka upanga uliochomolewa alani,

kutoka upinde uliopindwa,

na kutoka kwenye joto la vita.

1621:16 Law 25:50; Mwa 25:13; 25:13; Isa 17:3; 16:14; Za 120:5; Law 25:50; Wim 1:5; Mwa 25:13Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho. 1721:17 Hes 23:19; Kum 4:27; Isa 10; 19; 1:20; 16:14; Lk 21:33; 1Sam 15:29; Mt 24:35; Mk 13:31; 1Pet 1:25Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 21:1-17

关于巴比伦的预言

1以下是关于海边沙漠21:1 “海边沙漠”指巴比伦。的预言:

敌人从可怕的沙漠之地上来,

好像狂风扫过南部的旷野。

2我看见一个可怖的异象:

“诡诈的在行诡诈,

毁灭的在行毁灭。

以拦人啊,攻打吧!

玛代人啊,围城吧!

耶和华必终止巴比伦带来的痛苦。”

3这使我充满痛苦,

我陷入剧痛中,

如同分娩的妇人,

我因听见的话而惊慌,

因看见的景象而害怕。

4我心慌意乱,惊惧不堪,

我期盼的黄昏却令我恐惧。

5他们摆设宴席,

铺开地毯又吃又喝。

首领啊,起来擦亮盾牌备战吧!

6主对我说:

“你去派人守望,

让他报告所看见的情况。

7他看到战车、一对对的骑兵、

驴队和骆驼队的时候,

要提高警惕,密切察看。”

8守望的人大喊:

“主啊,我终日站在瞭望塔上,

整夜守在自己的岗位上。

9看啊,战车和一对对的骑兵来了。”

他又接着说:“巴比伦倾倒了!

倾倒了!

它所有的神像都被打碎在地上。”

10于是,我说:“我的百姓啊!

你们像场上被碾、被筛的谷物,

现在我把从以色列的上帝——万军之耶和华那里听见的都告诉你们了。”

关于以东的预言

11以下是关于度玛的预言。

有人从西珥大声问道:

“守望者啊,黑夜还有多长?

守望者啊,黑夜还有多长?”

12守望者回答:

“黎明将到,但黑夜会再来。

你们想问就问吧,可以再回来。”

关于阿拉伯的预言

13以下是关于阿拉伯的预言:

底但的商队必宿在阿拉伯的树林中。

14提玛的居民啊,要送水给这些口渴的人,

拿食物给这些逃难的人。

15他们逃离了刀光箭影和激烈的战争。

16主对我说:“按雇工规定的做工年限,一年之内,基达所有的荣耀必消失, 17勇敢的弓箭手必所剩无几。这是以色列的上帝耶和华说的。”