Isaya 21 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 21:1-17

Unabii Dhidi Ya Babeli

1Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari:

Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini,

mshambuliaji anakuja kutoka jangwani,

kutoka nchi inayotisha.

221:2 1Sam 24:13-16; Mwa 10:22; Za 60:3; Yer 49:34; Isa 22:6; 13:3; Yer 25:25Nimeonyeshwa maono ya kutisha:

Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara.

Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi!

Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.

321:3 Mwa 3:16; Yn 16:2; Ay 14:22; Za 48:6; Isa 26:17; Yer 30:6; Dan 7:28Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu,

maumivu makali ya ghafula yamenishika,

kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.

Nimeduwazwa na lile ninalolisikia,

nimeshangazwa na lile ninaloliona.

421:4 Isa 7:4; 35:4; 13:8; Dan 5:9; Za 55:5Moyo wangu unababaika,

woga unanifanya nitetemeke,

gizagiza la jioni nililolitamani sana,

limekuwa hofu kuu kwangu.

521:5 Yer 25:16, 27; Dan 5:2-5; Isa 5:12; 23:7; Yer 46:3; 1Sam 1:21Wanaandaa meza,

wanatandaza mazulia,

wanakula, wanakunywa!

Amkeni, enyi maafisa,

zitieni ngao mafuta!

621:6 2Fal 9:17Hili ndilo Bwana analoniambia:

“Nenda, weka mlinzi,

na atoe taarifa ya kile anachokiona.

721:7 Amu 6:5; Isa 21:9Anapoona magari ya vita

pamoja na kundi la farasi,

wapanda punda au wapanda ngamia,

na awe macho, awe macho kikamilifu.”

821:8 Mik 7:7; Hab 2:1Naye mlinzi alipaza sauti,

“Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi,

kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.

921:9 Isa 13:19; Ufu 14:8; Dan 5:30; Ufu 18:2; Yer 50:2; Isa 47:11; Yer 51:8Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita

pamoja na kundi la farasi.

Naye anajibu:

‘Babeli umeanguka, umeanguka!

Vinyago vyote vya miungu yake

vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’ ”

1021:10 Yer 51:33; Mt 3:12; Mik 4:13; Isa 27:12; Hab 3:12Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria,

ninawaambia kile nilichokisikia

kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote,

kutoka kwa Mungu wa Israeli.

Unabii Dhidi Ya Edomu

1121:11 Mwa 32:3; 1Nya 1:30; Eze 35:2; Oba 1:1Neno kuhusu Duma:

Mtu fulani ananiita kutoka Seiri,

“Mlinzi, usiku utaisha lini?

Mlinzi, usiku utaisha lini?”

12Mlinzi anajibu,

“Asubuhi inakuja, lakini pia usiku.

Kama ungeliuliza, basi uliza;

bado na urudi tena.”

Unabii Dhidi Ya Arabia

1321:13 Isa 13:1; 2Nya 9:14; Mwa 10:7; 25:3; 1Nya 1:9Neno kuhusu Arabia:

Enyi misafara ya Wadedani,

mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,

1421:14 Mwa 25:15; Ay 6:19leteni maji kwa wenye kiu,

ninyi mnaoishi Tema,

leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.

1521:15 Isa 13:14; 31:8Wanaukimbia upanga,

kutoka upanga uliochomolewa alani,

kutoka upinde uliopindwa,

na kutoka kwenye joto la vita.

1621:16 Law 25:50; Mwa 25:13; 25:13; Isa 17:3; 16:14; Za 120:5; Law 25:50; Wim 1:5; Mwa 25:13Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho. 1721:17 Hes 23:19; Kum 4:27; Isa 10; 19; 1:20; 16:14; Lk 21:33; 1Sam 15:29; Mt 24:35; Mk 13:31; 1Pet 1:25Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.