Isaya 12 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 12:1-6

Kushukuru Na Kusifu

112:1 Zek 14:20-21; Isa 25:1; 10:20; Ay 13:16; Za 71:21; 9:1Katika siku ile utasema:

“Nitakusifu wewe, Ee Bwana.

Ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imegeukia mbali

nawe umenifariji.

212:2 Kut 15:2; Dan 6:23; Za 26:1; 118:14; Isa 17:10; 25:9; 26:4; Ay 13:15Hakika Mungu ni wokovu wangu;

nitamtumaini wala sitaogopa.

Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu;

amekuwa wokovu wangu.”

312:3 Yer 2:13; 17:13; Za 39:6; Yn 4:10, 14; 2Fal 3:17; Kut 15:25Kwa furaha mtachota maji

kutoka visima vya wokovu.

412:4 Za 80:18; 113:2; Hos 12:5; Kut 3:15; Isa 10:20; 24:15; Yer 10:7Katika siku hiyo mtasema:

“Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake;

julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

512:5 Kut 15:1; Za 98:1Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu,

hili na lijulikane duniani kote.

612:6 Za 78:41; Eze 39:7; Sef 3:14-17; Za 46:5; 98:4; Mwa 21:6; Isa 48:20; Zek 2:10Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,

kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”

New International Version

Isaiah 12:1-6

Songs of Praise

1In that day you will say:

“I will praise you, Lord.

Although you were angry with me,

your anger has turned away

and you have comforted me.

2Surely God is my salvation;

I will trust and not be afraid.

The Lord, the Lord himself, is my strength and my defense12:2 Or song;

he has become my salvation.”

3With joy you will draw water

from the wells of salvation.

4In that day you will say:

“Give praise to the Lord, proclaim his name;

make known among the nations what he has done,

and proclaim that his name is exalted.

5Sing to the Lord, for he has done glorious things;

let this be known to all the world.

6Shout aloud and sing for joy, people of Zion,

for great is the Holy One of Israel among you.”