Hosea 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Hosea 2:1-23

12:1 1Pet 2:10; Hos 2:5“Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’

Israeli Aadhibiwa Na Kurudishwa

22:2 Isa 1:21; 50:1; Eze 16:25; 23:45; Hos 4:5“Mkemeeni mama yenu, mkemeeni,

kwa maana yeye si mke wangu,

nami si mume wake.

Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake

na uzinzi kati ya matiti yake.

32:3 Eze 16:4, 37; 19:13; Isa 32:13-14Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi

na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa.

Nitamfanya kama jangwa,

nitamgeuza awe nchi ya kiu,

nami nitamuua kwa kiu.

42:4 Eze 8:18; Hos 1:6; 5:7Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake,

kwa sababu ni watoto wa uzinzi.

52:5 Yer 3:6; 44:17-18; Hos 1:2Mama yao amekosa uaminifu

na amewachukua mimba katika aibu.

Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu,

ambao hunipa chakula changu

na maji yangu,

sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu

na kinywaji changu.’

62:6 Ay 3:23; 19:8; Mao 3:9Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake

kwa vichaka vya miiba,

nitamjengea ukuta ili kwamba

asiweze kutoka.

72:7 Hos 5:13; Yer 3:1; Eze 16:8; Isa 54:5Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata;

atawatafuta lakini hatawapata.

Kisha atasema,

‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza,

kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi

kuliko sasa.’

82:8 Eze 16:15-19; Hes 18:12; Kum 8:18; Hos 8:4Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye

niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta,

niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia

kwa kumtumikia Baali.

92:9 Hos 8:7; 9:2“Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa

na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari.

Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu

iliyokusudiwa kufunika uchi wake.

102:10 Eze 16:37; 23:10; Yer 13:26Basi sasa nitaufunua ufisadi wake

mbele ya wapenzi wake;

hakuna yeyote atakayemtoa

mikononi mwangu.

112:11 Isa 1:14; 24:8; Amo 5:21; 8:10; Yer 7:34; 16:9; Hos 9:5Nitakomesha furaha na macheko yake yote:

sikukuu zake za mwaka,

sikukuu za Miandamo ya Mwezi,

siku zake za Sabato,

sikukuu zake zote zilizoamriwa.

122:12 Isa 5:6; 7:23; Yer 8:13; Hos 5:7; 13:8Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake,

ambayo alisema yalikuwa malipo yake

kutoka kwa wapenzi wake;

nitaifanya kuwa kichaka,

nao wanyama pori wataila.

132:13 Yer 7:9; Hos 4:13; 8:14; 11:2; 13:6; Eze 16:17; 23:40; Isa 65:7Nitamwadhibu kwa ajili ya siku

alizowafukizia uvumba Mabaali;

alipojipamba kwa pete

na kwa vito vya thamani,

na kuwaendea wapenzi wake,

lakini mimi alinisahau,”

asema Bwana.

142:14 Eze 19:14“Kwa hiyo sasa nitamshawishi;

nitamwongoza hadi jangwani

na kuzungumza naye kwa upole.

152:15 Yos 7:24-26; Kut 15:1-18; Eze 16:22; 28:26; Hos 12:9; 1Kor 13:13Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu,

nami nitalifanya Bonde la Akori2:15 Akori maana yake ni Taabu.

mlango wa matumaini.

Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake,

kama siku zile alizotoka Misri.

162:16 Isa 54:5“Katika siku ile,” asema Bwana,

“utaniita mimi ‘Mume wangu’;

hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’

172:17 Kut 23:13; Za 16:4; Yer 23:7; Zek 13:2Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake,

wala hataomba tena kwa majina yao.

182:18 Ay 5:22-23; Za 49:6; Zek 9:10; Eze 34:25; Yer 23:6Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao

na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani,

na viumbe vile vitambaavyo ardhini.

Upinde, upanga na vita,

nitaondolea mbali katika nchi,

ili kwamba wote waweze kukaa salama.

192:19 Isa 1:27; 62:4; 54:8; 2Kor 11:2Nitakuposa uwe wangu milele;

nitakuposa kwa uadilifu na haki,

kwa upendo na huruma.

202:20 Yer 31:34; Hos 4:1; 6:6; 13:4; Eze 16:8Nitakuposa kwa uaminifu,

nawe utamkubali Bwana.

212:21 Zek 8:12; Mal 3:10-11; Isa 55:10“Katika siku ile nitajibu,”

asema Bwana,

“nitajibu kwa anga,

nazo anga zitajibu kwa nchi;

222:22 Yer 31:12; Yoe 2:19; Hos 14:7; Eze 36:29-30nayo nchi itajibu kwa nafaka,

divai mpya na mafuta,

navyo vitajibu kwa Yezreeli.

232:23 Yer 29:12; 31:27; Isa 19:25; Hos 1:10; Rum 9:25; Zek 13:9; 1Pet 2:10Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe;

nami nitaonyesha pendo langu kwake

yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.2:23 Kiebrania ni Lo-Ruhama.

Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’2:23 Kiebrania ni Lo-Ami.

‘Ninyi ni watu wangu’;

nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’ ”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

何西阿书 2:1-23

1“你们要称你们的弟兄为阿米2:1 “阿米”意思是“我的子民”。,要称你们的姊妹为路哈玛2:1 “路哈玛”意思是“得蒙怜悯”。

对不贞之妇的控诉

2“你们去跟你们的母亲理论吧!

因为她不再是我的妻子,

我也不再是她的丈夫。

叫她别再出卖色相,

别再露出乳间的淫态。

3不然,我要剥光她的衣服,

使她像初生之时一样赤身露体;

我要使她像沙漠,如旱地,

干渴而死。

4我也不怜悯她的儿女,

因为他们都是娼妓所生的儿女。

5他们的母亲淫乱放荡,

怀他们的人行为可耻,

她竟说,‘我要跟随我的情人,

他们给我食物和水、羊毛和麻布、油和酒。’

6因此,我要用荆棘围堵她的道,

筑墙阻断她的去路。

7她要追随情人,却追不上;

寻找情人,却找不到。

于是,她说,‘我倒不如回到丈夫身边,

我从前的光景比现在还好。’

8她不知道是我给她五谷、新酒和油,

又赐给她大量金银,

她却用这些供奉巴力

9因此,到了收割和酿酒的季节,

我要收走我的五谷和新酒,

夺回我给她遮体的羊毛和麻布。

10我要当着她情人的面揭露她的淫荡,

无人能从我手中把她救出去。

11我要终止她一切的欢庆,

终止她的节日、朔日2:11 “朔日”即每月初一。、安息日及其他节期。

12她说她的葡萄树和无花果树是情人给她的嫖资,

我要摧毁它们,

使它们变为荒林,

被野兽吞吃。

13我要惩罚她,

因为她在节日向巴力烧香。

那时她戴耳环佩首饰,

追逐她的情人,把我忘记。

这是耶和华说的。

对不贞之妇的爱

14“然而,我要引导她,

领她到旷野,

柔声安慰她。

15我要把葡萄园再赐给她,

使灾祸之谷2:15 “灾祸之谷”希伯来文是“亚割谷”,“亚割”意思是“灾祸”。参见约书亚记第七章。成为希望之门。

她要在那里欢唱,如在妙龄之时,

如从埃及出来之日。”

16耶和华说:

“那时,你要称我为丈夫,

不再称我为主人2:16 此处的“主人”希伯来文是“巴力”。“巴力”意思是“主人或丈夫”,也是迦南人神明的名字。

17我要从你口中除掉巴力的名字,

再也不让你提起它们。

18那时,我要跟田间的走兽、空中的飞鸟及地上的爬虫立约。

我要从地上折弓断剑,废止战事,

使你安居乐业。

19我要聘你永远做我的妻,

以仁义、正直、慈爱、怜悯聘你为妻。

20我要以信实聘你为妻,

这样你必认识耶和华。”

21耶和华说:

“那时,我要应允,

我要应允天的祈求,

天要应允地的祈求,

22地要应允五谷、新酒和油的祈求,

五谷、新酒和油要应允耶斯列的祈求。

23我要把你栽种在这片土地上,归我所有。

我要怜悯那不蒙怜悯的人,

对那不是我子民的人说,‘你是我的子民。’

他们也要对我说,‘你是我的上帝。’”