Hosea 12 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Hosea 12:1-14

112:1 Mwa 41:6; Eze 17:10; 2Fal 17:4; Za 78:67; Hos 4:19; 5:13Efraimu anajilisha upepo;

hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima

na kuzidisha uongo na jeuri.

Anafanya mkataba na Ashuru

na kutuma mafuta ya zeituni Misri.

212:2 Ay 10:212:2 Mik 6:2; Hos 4:9; 9:15; Kut 32:34; Amo 2:4Bwana analo shtaka dhidi ya Yuda,

atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake

na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.

312:3 Mwa 25:26; 32:24-29Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake;

kama mwanadamu, alishindana na Mungu.

412:4 Mwa 12:8; 28:12-15; 35:15Alishindana na malaika na kumshinda;

alilia na kuomba upendeleo wake.

Alimkuta huko Betheli

na kuzungumza naye huko:

512:5 Kut 3:15Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote,

Bwana ndilo jina lake!

612:6 Mik 6:8; 7:7; Za 106:13; Eze 18:30; Isa 19:22; Yoe 2:12; Yer 22:3Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako;

dumisha upendo na haki,

nawe umngojee Mungu wako siku zote.

712:7 Law 19:26; Amo 8:5Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu;

hupenda kupunja.

812:8 Za 62:10; Ufu 3:17; Eze 28:5Efraimu hujisifu akisema,

“Mimi ni tajiri sana; nimetajirika.

Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu

uovu wowote au dhambi.”

912:9 Law 23:43; Hos 2:15; Neh 8:17“Mimi ndimi Bwana Mungu wenu

niliyewaleta kutoka Misri;

nitawafanya mkae tena kwenye mahema,

kama vile katika siku

za sikukuu zenu zilizoamriwa.

1012:10 Amu 14:12; Eze 20:49; 2Fal 17:13; Yer 7:25Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi

na kusema mifano kupitia wao.”

1112:11 Amo 4:4; Hos 4:15; 6:8; 8:11Je, Gileadi si mwovu?

Watu wake hawafai kitu!

Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali?

Madhabahu zao zitakuwa

kama malundo ya mawe

katika shamba lililolimwa.

1212:12 Mwa 28:5; 29:18Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu;

Israeli alitumika ili apate mke,

ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo.

1312:13 Kut 14:19-22; Isa 63:11-14; Kut 13:3; Hos 11:1Bwana alimtumia nabii

kumpandisha Israeli kutoka Misri,

kwa njia ya nabii alimtunza.

1412:14 Eze 18:13; Dan 11:18Lakini Efraimu amemchochea sana hasira;

Bwana wake ataleta juu yake

hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza

kwa ajili ya dharau yake.