Hesabu 3 – NEN & TNCV

Kiswahili Contemporary Version

Hesabu 3:1-51

Walawi

13:1 Kut 6:27; 19:11Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.

23:2 Hes 1:20; 26:30; Kut 6:23; 1Nya 6:3Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari. 33:3 Kut 28:41; 29:30Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani. 43:4 Law 10:1-6, 12; Hes 4:28; 1Nya 24:1; Hes 26:61; Kum 4:24; Isa 66:15; 2The 1:8; Ebr 12:29Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.

5Bwana akamwambia Mose, 63:6 Kum 10:8; 31:9; 1Nya 15:2; Hes 8:6-22; 18:1-7; 2Nya 29:11“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie. 73:7 Hes 1:53; 8:19; Law 8:35Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani. 8Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani. 93:9 Hes 8:19; 18:6Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa. 103:10 Kut 30:7; 29:9; Hes 1:51; 18:7; Mdo 6:3-4; Rum 12:7; 1Sam 6:19; Hes 16:40; 18:7Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”

11Bwana akamwambia Mose, 123:12 Neh 13:12; Mal 2:4; Hes 8:14, 16-18; 16:9; Kut 13:2“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu, 133:13 Kut 13:12; Law 11:44kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”

14Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai, 153:15 Hes 1:19; 18:16; 26:62“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.” 16Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

173:17 Mwa 29:34; 46:11; Hes 1:47; 1Nya 15:4; 23:6; 2Nya 29:12; Yos 21:4-6Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi:

Gershoni, Kohathi na Merari.

183:18 Kut 6:16-17Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni:

Libni na Shimei.

193:19 Kut 6:18Koo za Wakohathi zilikuwa ni:

Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

203:20 Mwa 46:11; Kut 6:19Koo za Wamerari zilikuwa ni:

Mahli na Mushi.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.

213:21 Mwa 46:11; Kut 6:17Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni. 22Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500. 233:23 Hes 2:18Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani. 24Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli. 253:25 Kut 25:9; 26:14, 36; 40:2; Hes 7:1; 4:25; 1Nya 9:14-33; Ezr 8:28-30Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania, 263:26 Kut 27:9; 35:18; Hes 4:26mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.

273:27 Mwa 46:11; Kut 6:18; 1Nya 26:23; Hes 4:15, 37Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi. 283:28 Hes 4:4, 15; Kut 25:8; 30:13; 2Nya 30:19; Za 15:1; 20:2; Eze 44:27Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu. 293:29 Hes 1:53Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani. 303:30 Kut 6:22Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli. 313:31 Kut 25:10-22, 23, 31; 26:33; Kum 10:1-8; 2Nya 5:2; Yer 3:16; 1Nya 28:15; Yer 52:19; Hes 1:50; 4:5, 15; 18:3Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake. 323:32 Kut 6:23; Hes 4:19; 18:3; 20:25-28; 2Fal 25:18Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.

333:33 Kut 6:19; Mwa 46:11Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari. 34Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200. 353:35 Hes 1:53; 2:25Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani. 363:36 Hes 4:32; Kut 26:15-25; 35:20-29; 36:36; Hes 18:3Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake, 373:37 Kut 27:10-19na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.

383:38 Hes 2:3; 18:5; 1:51; 1Nya 9:27; 23:32Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.

393:39 Hes 26:62Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.

40Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao. 413:41 Law 11:44Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”

42Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru. 43Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.

44Bwana akamwambia Mose, 453:45 Hes 3:12; 1Sam 1:28“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana. 463:46 Kut 13:13; Hes 18:15Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi, 473:47 Law 27:6, 25; Kut 30:13; Hes 18:16; Eze 45:12kusanya shekeli tano3:47 Shekeli tano ni sawa na gramu 55. kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.3:47 Gera 20 ni sawa na gramu 11. 48Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”

493:49 1Tim 2:6; Tit 2:14; Gal 4:4-5; 1Pet 1:18; Ebr 9:12Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi. 503:50 1Sam 12:3-4; Mdo 20:33Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,3653:50 Shekeli 1,365 ni sawa na kilo 15.5. kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu. 51Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

Thai New Contemporary Version

กันดารวิถี 3:1-51

คนเลวี

1ต่อไปนี้เป็นเรื่องราวของครอบครัวอาโรนและโมเสส เมื่อครั้งองค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสกับโมเสสบนภูเขาซีนาย

2บุตรชายของอาโรนได้แก่ นาดับซึ่งเป็นบุตรหัวปี อาบีฮู เอเลอาซาร์ และอิธามาร์ 3คนเหล่านี้ซึ่งเป็นบุตรของอาโรนได้รับการเจิมตั้งและสถาปนาให้ปรนนิบัติในฐานะปุโรหิต 4แต่นาดับและอาบีฮูเสียชีวิตต่อหน้าองค์พระผู้เป็นเจ้าในถิ่นกันดารซีนายเมื่อได้จุดไฟต้องห้ามขึ้น คนทั้งสองไม่มีบุตร จึงเหลือแต่เอเลอาซาร์และอิธามาร์ทำหน้าที่ปุโรหิตในช่วงชีวิตของอาโรนผู้เป็นบิดา

5องค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสกับโมเสสว่า 6“จงนำคนเผ่าเลวีมารายงานตัวต่อปุโรหิตอาโรนเพื่อช่วยงานเขา 7คนเหล่านี้จะปฏิบัติหน้าที่ในเต็นท์นัดพบแทนอาโรนและชาวอิสราเอลทั้งหมด โดยรับผิดชอบงานเกี่ยวกับพลับพลาทั้งหมด 8พวกเขาจะต้องคอยดูแลส่วนประกอบทั้งหมดของเต็นท์นัดพบ และปฏิบัติหน้าที่ที่พลับพลาเพื่อชนอิสราเอล 9จงมอบคนเลวีให้แก่อาโรนและบรรดาบุตรชายของเขา คนเลวีเป็นชาวอิสราเอลที่คอยช่วยงานเขา3:9 สำเนา MT. บางฉบับ และฉบับ SamP. และ ฉบับ LXX. ว่าช่วยงานเรา(ดูกดว.8:16) อย่างเต็มที่ 10จงแต่งตั้งอาโรนกับบุตรชายของเขาให้ปฏิบัติหน้าที่ปุโรหิต ใครอื่นล่วงล้ำเข้ามาใกล้สถานนมัสการจะมีโทษถึงตาย”

11องค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสกับโมเสสอีกว่า 12“เราได้เลือกชนเผ่าเลวีจากชนอิสราเอลให้เป็นตัวแทนบุตรชายหัวปีของหญิงชาวอิสราเอลทุกคน คนเลวีเป็นของเรา 13เพราะบุตรหัวปีเป็นของเรา ตั้งแต่วันที่เราประหารบุตรชายหัวปีทั้งปวงของชาวอียิปต์ เราได้แยกลูกหัวปีของอิสราเอลทั้งหมด ไม่ว่าคนหรือสัตว์มาเป็นของเรา เราคือพระยาห์เวห์”

14องค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสกับโมเสสในถิ่นกันดารซีนายว่า 15“จงนับจำนวนคนเลวีตามครอบครัวและตระกูลของเขา นับผู้ชายทุกคนอายุหนึ่งเดือนขึ้นไป” 16ดังนั้นโมเสสก็นับพวกเขาตามคำสั่งขององค์พระผู้เป็นเจ้า

17ต่อไปนี้เป็นรายชื่อบุตรของเลวี ได้แก่

เกอร์โชน โคฮาท และเมรารี

18คนในตระกูลเกอร์โชน ได้แก่

ลิบนีและชิเมอี

19คนในตระกูลโคฮาท ได้แก่

อัมราม อิสฮาร์ เฮโบรน และอุสซีเอล

20คนในตระกูลเมรารี ได้แก่

มาห์ลีและมูชี

ทั้งหมดนี้คือตระกูลต่างๆ ของคนเลวีตามครอบครัวของเขา

21ลูกหลานของลิบนีและชิเมอีเป็นของตระกูลเกอร์โชน 22รวมผู้ชายทั้งหมดที่อายุหนึ่งเดือนขึ้นไปมี 7,500 คน 23ตระกูลเกอร์โชนจะตั้งค่ายด้านทิศตะวันตกหลังพลับพลา 24ผู้นำครอบครัวต่างๆ ในตระกูลเกอร์โชนคือเอลียาสาฟบุตรลาเอล 25ตระกูลเกอร์โชนรับผิดชอบดูแลพลับพลาและเต็นท์ พร้อมเครื่องคลุมเต็นท์และม่านตรงทางเข้าเต็นท์นัดพบ 26ม่านกั้นรอบลานพลับพลา ม่านกั้นทางเข้าลานพลับพลาและแท่นบูชา และเชือกทั้งหมดที่ใช้โยงพลับพลาเข้าด้วยกัน และทุกอย่างที่เกี่ยวข้องเพื่อใช้ในงานนี้

27ลูกหลานของอัมราม อิสฮาร์ เฮโบรน และอุสซีเอลเป็นของตระกูลโคฮาท 28รวมผู้ชายทั้งหมดที่อายุหนึ่งเดือนขึ้นไปมี 8,600 คน3:28 สำเนา LXX. บางฉบับว่า8,300 คนตระกูลโคฮาทรับผิดชอบดูแลสถานนมัสการ 29ตระกูลโคฮาทจะตั้งค่ายด้านทิศใต้ของพลับพลา 30ผู้นำครอบครัวต่างๆ ในตระกูลโคฮาทคือ เอลีซาฟานบุตรอุสซีเอล 31พวกเขารับผิดชอบดูแลหีบพันธสัญญา โต๊ะ คันประทีป แท่นทั้งสองและเครื่องใช้ต่างๆ ของสถานนมัสการ ม่าน และทุกอย่างที่เกี่ยวข้องเพื่อใช้ในงานนี้ 32หัวหน้าใหญ่ของคนเลวีคือ ปุโรหิตเอเลอาซาร์บุตรของอาโรน เขาได้รับแต่งตั้งให้กำกับดูแลสถานนมัสการ

33ลูกหลานของมาห์ลีและมูชีเป็นของตระกูลเมรารี 34รวมชายทั้งหมดที่อายุหนึ่งเดือนขึ้นไปมี 6,200 คน 35ผู้นำครอบครัวต่างๆ ในตระกูลเมรารีคือศุรีเอลบุตรอาบีฮายิล พวกเขาจะตั้งค่ายด้านทิศเหนือของพลับพลา 36ตระกูลเมรารีได้รับมอบหมายให้ดูแลไม้ฝาของพลับพลา คานขวาง เสา ฐานรองรับ อุปกรณ์ต่างๆ และทุกส่วนที่เกี่ยวข้องเพื่อใช้ในงานนี้ 37ตลอดจนเสารอบลานพลับพลา ฐานรองรับ หลักหมุด และเชือก

38โมเสสและอาโรนกับบรรดาบุตรชายของเขาจะตั้งเต็นท์ที่ด้านทิศตะวันออกของพลับพลา ด้านหน้าเต็นท์นัดพบ พวกเขารับผิดชอบดูแลสถานนมัสการแทนชนอิสราเอล ใครอื่นล่วงล้ำเข้าใกล้สถานนมัสการจะมีโทษถึงตาย

39รวมชายเลวีอายุหนึ่งเดือนขึ้นไปทั้งหมด ซึ่งโมเสสและอาโรนได้นับไว้ตามตระกูลของพวกเขา ตามพระบัญชาขององค์พระผู้เป็นเจ้ามี 22,000 คน

40องค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสกับโมเสสว่า “จงทำทะเบียนรายชื่อบุตรชายหัวปีทุกคนของอิสราเอลที่มีอายุหนึ่งเดือนขึ้นไป 41คนเลวีจะเป็นของเรา เป็นตัวแทนบุตรชายหัวปีของอิสราเอล และฝูงสัตว์ของคนเลวีจะเป็นตัวแทนลูกหัวปีทั้งหมดของฝูงสัตว์ของคนอิสราเอล เราคือพระยาห์เวห์”

42ดังนั้นโมเสสจึงนับจำนวนบุตรหัวปีทั้งหมดของชนอิสราเอลตามที่องค์พระผู้เป็นเจ้าทรงบัญชา 43บุตรชายหัวปีอายุหนึ่งเดือนขึ้นไปตามรายชื่อมีทั้งสิ้น 22,273 คน

44องค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสกับโมเสสว่า 45“จงมอบคนเลวีให้เราแทนบุตรชายหัวปีทั้งหมดของอิสราเอล และมอบฝูงสัตว์ของคนเลวีให้เราแทนฝูงสัตว์ของพวกเขา คนเลวีจะเป็นของเรา เราคือพระยาห์เวห์ 46สำหรับบุตรชายหัวปีของอิสราเอล 273 คนซึ่งเกินจำนวนคนเลวีนั้น 47จงเก็บเงินหนักคนละห้าเชเขล3:47 1 เชเขล คือเงินหนักประมาณ 11.5 กรัม มีค่าเท่ากับค่าแรงสองเดือน เช่นเดียวกับข้อ 50ตามเชเขลของสถานนมัสการ ซึ่งเท่ากับยี่สิบเกราห์ 48จงมอบเงินค่าไถ่ตัวของชนอิสราเอลที่เกินมานี้ให้แก่อาโรนและบุตรชายของเขา”

49โมเสสจึงเก็บเงินค่าไถ่จากบุตรหัวปีชาวอิสราเอล ซึ่งเกินจำนวนคนที่ไถ่แล้วโดยทางคนเลวี 50รวมจำนวนเงินที่เก็บได้หนัก 1,365 เชเขล ตามเชเขลของสถานนมัสการ 51โมเสสมอบเงินค่าไถ่นี้ให้แก่อาโรนและบรรดาบุตรชายตามพระบัญชาขององค์พระผู้เป็นเจ้า