Hesabu 25 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Hesabu 25:1-18

Moabu Yashawishi Israeli

125:1 Hes 21:16; Yos 2:1; Isa 66:11; Yoe 3:18; Mik 6:5; Yer 5:7; 7:9; 9:2; 1Kor 10:8; Ufu 2:14; Mwa 19:37; Hes 31:16Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu, 225:2 Kut 32:6; 20:5; Kum 32:38; 1Kor 10:20; Yos 22:17; Hos 9:10; Kut 34:15; 20:5ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii. 325:3 Kum 4:19; Amu 2:19; 1Fal 9:9; Yer 1:16; 44:3; Hes 23:26Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.

425:4 Hes 7:2; 13:3; 2Sam 21:6; Kum 4:3; Kut 32:12; Kum 13:17; Yos 7:26; 2Fal 23:26; 2Nya 28:11; 29:10; 30:8; Eze 10:14; Yer 44:3Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”

525:5 Kut 32:27; Hos 9:10Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”

625:6 Mwa 25:2; Hes 14:1; Amu 2:4; Rut 1:9; 1Sam 11:4; 2Sam 15:30; Ezr 10:1; Za 126:6; Yer 41:6Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania. 725:7 Kut 6:25; Yos 22:13; Amu 20:28; 5:8; 1Sam 13:19; 1Fal 18:28; Za 35:3; 46:9; Yoe 3:10; Mik 4:3Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake, 825:8 Za 106:30akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma. 925:9 Hes 14:37; 1Kor 10:8; Hes 31:16Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.

10Bwana akamwambia Mose, 1125:11 Za 106:30; Kut 20:5; Kum 32:16; Za 78:58; Nah 1:3; Sef 1:13“Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza. 1225:12 Isa 11:9; 54:10; Eze 34:25; 37:26; Mal 2:4Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye. 1325:13 Kut 29:9; 1Fal 19:10; 2Fal 10:16; Kut 29:36; Rum 3:26; Za 106:31; Yer 33:18Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”

1425:14 Hes 1:6; 25:6Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni. 1525:15 Hes 31:8; Yos 13:21; Hab 3:7Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.

1625:16 Hes 31:7Bwana akamwambia Mose, 1725:17 Hes 31:1-3; Kut 23:22; Amu 2:16-18; Neh 9:27; Za 8:2; 21:8; 74:23; Kum 21:1; 1Sam 17:9; 2Fal 9:27; 10:25“Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue, 1825:18 Hes 23:28kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”