Hesabu 10 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 10:1-36

Tarumbeta Za Fedha

1Bwana akamwambia Mose: 210:2 Hes 31:6; Neh 4:18; 12:35; Za 47:5; 98:6; 105:3; Yer 4:5; 19; 6:1; Hos 5:8; 8:1; Yoe 2:1“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka. 3Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania. 410:4 Kut 18:21; Hes 7:2Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako. 5Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka. 6Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka. 710:7 Yer 4:5; 6:1; Eze 33:3; Yoe 2:1; 1Kor 14:8Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.

810:8 Mwa 9:12; Hes 15:14; 35:29; Yos 6:4; 2Nya 13:12“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo. 910:9 Kut 3:9; Amu 2:18; 6:9; 1Sam 10:18; 2Fal 13:4; Za 106:42; Law 23:24; 2Nya 13:12; Mwa 8:1Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu. 1010:10 Hes 28:11; 1Sam 20:5, 24; 2Fal 4:23; 2Nya 8:13; Za 81:3; Isa 1:13; Eze 45:17; 46:6; Amo 8:5; Law 23:24; 1:3; 3:1; 11:44; Hes 6:14Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”

Waisraeli Waondoka Sinai

1110:11 Kut 38:21; 40:17; Hes 9:17Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda. 1210:12 Mwa 14:6; Kum 1:1; 33:2; Kut 40:36; Hes 12:16; Hab 3:3Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani. 1310:13 Kum 1:6; Hes 2:34Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.

1410:14 Hes 1:52; 2:3-9; 1:7Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao. 1510:15 Law 24:11; Hes 1:8Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari, 1610:16 Hes 2:7; 1:9naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni. 1710:17 Hes 4:21-32Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.

1810:18 Hes 2:16; 2:10-16; 1:5Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao. 19Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni, 2010:20 Hes 1:14naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi. 2110:21 Hes 2:17; 4:20Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.

2210:22 Hes 2:24; 1:10Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao. 23Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase, 2410:24 Hes 1:11naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.

2510:25 Hes 2:31; 1:12; Yos 6:9Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao. 26Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri, 27naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali. 2810:28 Za 80:1; Wim 6:10Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.

2910:29 Amu 4:11; Kut 2:18; 3:1; Mwa 12:7; 15:14Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”

3010:30 Mt 21:29; Kut 18:27Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”

3110:31 Ay 29:15Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu. 3210:32 Kut 12:48; Kum 10:18; Za 22:27-31; 67:5-7Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”

3310:33 Kum 1:33; 10:8; 31:9; Yos 3:3; Amu 20:27; 2Sam 15:24; Yer 31:2Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika. 3410:34 Hes 9:15-23; Kut 13:21; Neh 9:12, 19Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.

3510:35 2Nya 6:41; Za 17:13; 44:26; 94:2; 132:8; Amu 5:31; 2Sam 2:1; Za 68:1; 92:9; Kum 5:9; 7:10; Isa 17:12-14; 59:18Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema,

“Ee Bwana, inuka!

Watesi wako na watawanyike;

adui zako na wakimbie mbele zako.”

3610:36 Isa 52:8; 63:17; Mwa 15:5; 26:4; Kum 1:10; 10:22; Neh 9:23Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema,

“Ee Bwana, rudi,

kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

New International Version – UK

Numbers 10:1-36

The silver trumpets

1The Lord said to Moses: 2‘Make two trumpets of hammered silver, and use them for calling the community together and for the camps to set out. 3When both are sounded, the whole community is to assemble before you at the entrance to the tent of meeting. 4If only one is sounded, the leaders – the heads of the clans of Israel – are to assemble before you. 5When a trumpet blast is sounded, the tribes camping on the east are to set out. 6At the sounding of a second blast, the camps on the south are to set out. The blast will be the signal for setting out. 7To gather the assembly, blow the trumpets, but not with the signal for setting out.

8‘The sons of Aaron, the priests, are to blow the trumpets. This is to be a lasting ordinance for you and the generations to come. 9When you go into battle in your own land against an enemy who is oppressing you, sound a blast on the trumpets. Then you will be remembered by the Lord your God and rescued from your enemies. 10Also at your times of rejoicing – your appointed festivals and New Moon feasts – you are to sound the trumpets over your burnt offerings and fellowship offerings, and they will be a memorial for you before your God. I am the Lord your God.’

The Israelites leave Sinai

11On the twentieth day of the second month of the second year, the cloud lifted from above the tabernacle of the covenant law. 12Then the Israelites set out from the Desert of Sinai and travelled from place to place until the cloud came to rest in the Desert of Paran. 13They set out, this first time, at the Lord’s command through Moses.

14The divisions of the camp of Judah went first, under their standard. Nahshon son of Amminadab was in command. 15Nethanel son of Zuar was over the division of the tribe of Issachar, 16and Eliab son of Helon was over the division of the tribe of Zebulun. 17Then the tabernacle was taken down, and the Gershonites and Merarites, who carried it, set out.

18The divisions of the camp of Reuben went next, under their standard. Elizur son of Shedeur was in command. 19Shelumiel son of Zurishaddai was over the division of the tribe of Simeon, 20and Eliasaph son of Deuel was over the division of the tribe of Gad. 21Then the Kohathites set out, carrying the holy things. The tabernacle was to be set up before they arrived.

22The divisions of the camp of Ephraim went next, under their standard. Elishama son of Ammihud was in command. 23Gamaliel son of Pedahzur was over the division of the tribe of Manasseh, 24and Abidan son of Gideoni was over the division of the tribe of Benjamin.

25Finally, as the rear guard for all the units, the divisions of the camp of Dan set out under their standard. Ahiezer son of Ammishaddai was in command. 26Pagiel son of Okran was over the division of the tribe of Asher, 27and Ahira son of Enan was over the division of the tribe of Naphtali. 28This was the order of march for the Israelite divisions as they set out.

29Now Moses said to Hobab son of Reuel the Midianite, Moses’ father-in-law, ‘We are setting out for the place about which the Lord said, “I will give it to you.” Come with us and we will treat you well, for the Lord has promised good things to Israel.’

30He answered, ‘No, I will not go; I am going back to my own land and my own people.’

31But Moses said, ‘Please do not leave us. You know where we should camp in the wilderness, and you can be our eyes. 32If you come with us, we will share with you whatever good things the Lord gives us.’

33So they set out from the mountain of the Lord and travelled for three days. The ark of the covenant of the Lord went before them during those three days to find them a place to rest. 34The cloud of the Lord was over them by day when they set out from the camp.

35Whenever the ark set out, Moses said,

‘Rise up, Lord!

May your enemies be scattered;

may your foes flee before you.’

36Whenever it came to rest, he said,

‘Return, Lord,

to the countless thousands of Israel.’