Habakuki 3 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Habakuki 3:1-19

Maombi Ya Habakuki

1Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.3:1 Ni kifaa cha uimbaji chenye nyuzi; pia maombi kutumia kifaa hiki.

23:2 Ay 26:14; Za 119:120; 90:16; 44:1; 85:6; Isa 54:8Bwana, nimezisikia sifa zako;

nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana.

Fufua kazi yako katikati ya miaka,

katikati ya miaka tangaza habari yako;

katika ghadhabu kumbuka rehema.

33:3 Mwa 36:11, 15; Isa 31:1; Hes 10:12; Za 48:10Mungu alitoka Temani,

yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani.

Utukufu wake ulifunika mbingu,

na sifa zake zikaifunika dunia.

43:4 Isa 18:4; Ay 9:6Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo;

mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake,

ambako nguvu zake zilifichwa.

53:5 Law 26:25Tauni ilimtangulia;

maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.

63:6 Za 46:2; 114:1-6; 18:7; Kut 19:18; 23:31; Kum 32:8; Hes 21:24, 34; Mwa 49:26; 21:33Alisimama, akaitikisa dunia;

alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke.

Milima ya zamani iligeuka mavumbi

na vilima vilivyozeeka vikaanguka.

Njia zake ni za milele.

73:7 Mwa 25:2; Hes 25:15; Amu 7:24-25; Kut 15:14Niliona watu wa Kushani katika dhiki,

na makazi ya Midiani katika maumivu makali.

83:8 Kut 7:20; 14:21, 22; 2Fal 2:11; Za 77:16; 68:17Ee Bwana, uliikasirikia mito?

Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito?

Je, ulighadhibikia bahari

ulipoendesha farasi wako

na magari yako ya ushindi?

93:9 Kum 32:23; Za 7:12-13Uliufunua upinde wako

na kuita mishale mingi.

Uliigawa dunia kwa mito;

103:10 Za 77:16; 98:7; 93:3milima ilikuona ikatetemeka.

Mafuriko ya maji yakapita huko;

vilindi vilinguruma

na kuinua mawimbi yake juu.

113:11 Yos 10:13; Za 18:14; 144:6; Zek 9:14Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni

katika mngʼao wa mishale yako inayoruka,

na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.

123:12 Za 44:2, 3; Mik 4:13; Isa 41:15Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia,

na katika hasira ulikanyaga mataifa.

133:13 Kut 13:21; Za 20:6; 28:8; 68:21; 2Sam 5:20; 23:1Ulikuja kuwaokoa watu wako,

kumwokoa uliyemtia mafuta.

Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu,

ukamvua toka kichwani hadi wayo.

143:14 Amu 7:22; Za 64:2-5Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake

wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya,

wakifurahi kama walio karibu kutafuna

wale wanyonge waliokuwa mafichoni.

153:15 Ay 9:8; Kut 15:8Ulikanyaga bahari kwa farasi wako,

ukisukasuka maji makuu.

163:16 Ay 4:14; Za 37:7Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu,

midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti;

uchakavu ukanyemelea mifupa yangu,

na miguu yangu ikatetemeka.

Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa

kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.

173:17 Yoe 1:10-18; 2Kor 4:8, 9; Yer 5:17Ingawa mtini hauchanui maua

na hakuna zabibu juu ya mizabibu,

ingawaje mzeituni hauzai,

na hata mashamba hayatoi chakula,

iwapo hakuna kondoo katika banda,

wala ngʼombe katika zizi,

183:18 Za 42:5; 97:12; Isa 61:10; Kut 15:2; Lk 1:47; Flp 4:4hata hivyo nitashangilia katika Bwana,

nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.

193:19 Kum 32:13; 33:29; Za 27:1; 46:1-5; 18:33Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu;

huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala,

huniwezesha kupita juu ya vilima.

Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.