Habakuki 1 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Habakuki 1:1-17

11:1 Nah 1:1Neno alilopokea nabii Habakuki.

Lalamiko La Habakuki

21:2 Za 13:1-2; 22:1-2; 6:3; 27:7; Yer 14:9Ee Bwana, hata lini nitakuomba msaada,

lakini wewe husikilizi?

Au kukulilia, “Udhalimu!”

Lakini hutaki kuokoa?

31:3 Ay 9:23; Yer 20:8; Za 55:9Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma?

Kwa nini unavumilia makosa?

Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu;

kuna mabishano na mapambano kwa wingi.

41:4 Ay 12:6; Za 12:8; 58:2Kwa hiyo sheria imepotoshwa,

nayo haki haipo kabisa.

Waovu wanawazunguka wenye haki,

kwa hiyo haki imepotoshwa.

Jibu La Bwana

5“Yatazame mataifa,

uangalie na ushangae kabisa.

Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu

ambacho hungeamini,

hata kama ungeambiwa.

6Nitawainua Wakaldayo,

watu hao wakatili na wenye haraka,

ambao hupita dunia yote

kuteka mahali pa kuishi pasipo pao wenyewe.

7Ni watu wanoogopwa na wanaotisha;

wenyewe ndio sheria yao,

na huinua heshima yao wenyewe.

8Farasi wao ni wepesi kuliko chui,

na wakali kuliko mbwa mwitu wakati wa machweo.

Askari wapanda farasi wao huenda mbio;

waendesha farasi wao wanatoka mbali.

Wanaruka kasi kama tai ili kurarua;

91:9 Hab 2:5wote wanakuja tayari kwa fujo.

Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele

kama upepo wa jangwani,

na kukusanya wafungwa

kama mchanga.

101:10 2Nya 36:6; Yer 33:4Wanawabeza wafalme,

na kuwadhihaki watawala.

Wanaicheka miji yote iliyozungushiwa maboma;

wanafanya malundo ya udongo na kuiteka hiyo miji.

111:11 Yer 4:11-12; Dan 4:30Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele:

watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”

Lalamiko La Pili La Habakuki

121:12 Mwa 21:33; Isa 31:1; 37:23; Kut 33:22; Isa 10:6; Mwa 49:24; Za 118:17Ee Bwana, je, wewe sio wa tangu milele?

Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa.

Ee Bwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu;

Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.

131:13 Za 18:26; Mao 3:34-36; Za 25:3; Ay 21:7Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu,

wala huwezi kuvumilia makosa.

Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu?

Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu

wanawameza wale wenye haki

kuliko wao wenyewe?

14Umewafanya watu kama samaki baharini,

kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.

151:15 Yer 5:26; Isa 19:8; Ay 18:8; Yer 16:16Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana,

anawakamata katika wavu wake,

anawakusanya katika juya lake;

kwa hiyo anashangilia na anafurahi.

161:16 Yer 44:8Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake,

na kuchoma uvumba kwa juya lake,

kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe,

na anafurahia chakula kizuri.

171:17 Isa 14:6; 19:8Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake,

akiangamiza mataifa bila huruma?

New International Version

Habakkuk 1:1-17

1The prophecy that Habakkuk the prophet received.

Habakkuk’s Complaint

2How long, Lord, must I call for help,

but you do not listen?

Or cry out to you, “Violence!”

but you do not save?

3Why do you make me look at injustice?

Why do you tolerate wrongdoing?

Destruction and violence are before me;

there is strife, and conflict abounds.

4Therefore the law is paralyzed,

and justice never prevails.

The wicked hem in the righteous,

so that justice is perverted.

The Lord’s Answer

5“Look at the nations and watch—

and be utterly amazed.

For I am going to do something in your days

that you would not believe,

even if you were told.

6I am raising up the Babylonians,1:6 Or Chaldeans

that ruthless and impetuous people,

who sweep across the whole earth

to seize dwellings not their own.

7They are a feared and dreaded people;

they are a law to themselves

and promote their own honor.

8Their horses are swifter than leopards,

fiercer than wolves at dusk.

Their cavalry gallops headlong;

their horsemen come from afar.

They fly like an eagle swooping to devour;

9they all come intent on violence.

Their hordes1:9 The meaning of the Hebrew for this word is uncertain. advance like a desert wind

and gather prisoners like sand.

10They mock kings

and scoff at rulers.

They laugh at all fortified cities;

by building earthen ramps they capture them.

11Then they sweep past like the wind and go on—

guilty people, whose own strength is their god.”

Habakkuk’s Second Complaint

12Lord, are you not from everlasting?

My God, my Holy One, you1:12 An ancient Hebrew scribal tradition; Masoretic Text we will never die.

You, Lord, have appointed them to execute judgment;

you, my Rock, have ordained them to punish.

13Your eyes are too pure to look on evil;

you cannot tolerate wrongdoing.

Why then do you tolerate the treacherous?

Why are you silent while the wicked

swallow up those more righteous than themselves?

14You have made people like the fish in the sea,

like the sea creatures that have no ruler.

15The wicked foe pulls all of them up with hooks,

he catches them in his net,

he gathers them up in his dragnet;

and so he rejoices and is glad.

16Therefore he sacrifices to his net

and burns incense to his dragnet,

for by his net he lives in luxury

and enjoys the choicest food.

17Is he to keep on emptying his net,

destroying nations without mercy?