Ezekieli 35 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 35:1-15

Unabii Dhidi Ya Edomu

1Neno la Bwana likanijia kusema: 235:2 Mwa 14:6; Kum 2:5; Yer 49:7-8; Amo 1:11“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake 335:3 Yer 6:12; Eze 34:10; 25:12-14; Oba 1:10na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika. 435:4 Yer 49:10; 44:2Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

535:5 Za 137:7; Eze 21:29; Za 63:10; Oba 1:13“ ‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake, 635:6 Isa 63:2-6; 34:3kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia. 735:7 Yer 46:19; 49:17Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda. 835:8 Eze 31:12Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote. 935:9 Isa 34:5-6; Yer 49:13-17; Oba 1:10Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

1035:10 Za 83:12; Eze 36:2-5“ ‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko, 1135:11 Eze 25:14; Oba 1:15; Mt 7:2; Isa 26:9; Za 9:16kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu. 1235:12 Yer 50:7; Za 9:16Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.” 1335:13 Dan 11:36; Yer 49:16Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia. 1435:14 Yer 51:48Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa. 1535:15 Mit 17:5; Eze 36:5; Oba 1:12; Mao 4:4-21; Yer 50:11-13; Isa 34:5-6; Eze 32:29Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

New International Reader’s Version

Ezekiel 35:1-15

A Prophecy Against Edom

1A message from the Lord came to me. The Lord said, 2“Son of man, turn your attention to Mount Seir. Prophesy against it. 3Tell it, ‘The Lord and King says, “Mount Seir, I am against you. I will reach out my powerful hand against you. I will turn you into a dry and empty desert. 4I will destroy your towns. Your land will become empty. Then you will know that I am the Lord.

5“ ‘ “People of Edom, you have been Israel’s enemies for a long time. You let many Israelites be killed by swords when they were in great trouble. At that time I used Nebuchadnezzar to punish them and destroy them completely. 6Now I will hand you over to murderers. They will hunt you down. You murdered others. So murderers will chase you. And that is just as sure as I am alive,” announces the Lord and King. 7“I will turn Mount Seir into a dry and empty desert. No one will be able to go anywhere or do anything there. 8I will fill your mountains with dead bodies. Some of those who are killed by swords will fall down dead on your hills. Others will die in your valleys and in all your canyons. 9I will make your land empty forever. No one will live in your towns. Then you will know that I am the Lord.

10“ ‘ “You said, ‘The nations of Israel and Judah will belong to us. We will take them over.’ You said that, even though I was there. I am the Lord. 11You were full of anger, jealousy and hatred toward my people. So I will punish you. When I judge you, they will know that I am the Lord. And that is just as sure as I am alive,” announces the Lord and King. 12“You will know that I have heard all the terrible things you said. You said them about those who live in the mountains of Israel. You made fun of them. You said, ‘They have been destroyed. They’ve been handed over to us. Let’s wipe them out.’ 13You bragged that you were better than I am. You spoke against me. You did not hold anything back. But I heard it.” ’ ” 14The Lord and King says, “The whole earth will be glad. But I will make your land empty. 15You were happy when the land of Israel became empty. So I will treat you in the same way. Mount Seir, you will be empty. So will the whole land of Edom. Then you will know that I am the Lord.”