Ezekieli 34 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 34:1-31

Wachungaji Na Kondoo

1Neno la Bwana likanijia kusema: 234:2 Mik 3:11; Yud 12; Yer 3:15; Isa 40:11; Za 78:70-72; Yn 21:15-17“Mwanadamu, tabiri juu ya wachungaji wa Israeli, tabiri na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wa wachungaji wa Israeli ambao hujitunza wenyewe tu! Je, haiwapasi wachungaji kutunza kundi la kondoo? 334:3 Amo 6:4; Zek 11:5; Eze 22:27; Isa 56:11Mnakula mafuta ya wanyama, mnavaa mavazi ya sufu na kuchinja kondoo walionona, lakini hamlitunzi kundi. 434:4 Law 25:43; Mik 3:3; 2Tim 2:24; Mdo 9:36; Isa 3:7; Zek 11:15-17Hamkuwatia nguvu walio dhaifu wala hamkuwaganga wenye maradhi wala kuwafunga waliojeruhiwa. Hamkuwarudisha waliotangatanga wala kuwatafuta wale waliopotea. Badala yake mmewatawala kwa ukali na kwa ukatili. 534:5 Hes 27:17; Isa 56:9; Mdo 20:29Hivyo walitawanyika kwa sababu hapakuwepo mchungaji, nao walipotawanyika, wakawa chakula cha wanyama wa mwitu wote. 634:6 Yer 50:6; Law 26:33; Za 95:10; Yer 10:21; 2Nya 18:16; Za 142:4; Hos 7:13; Mt 9:36; 18:12-13Kondoo wangu walitawanyika, wakatangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu. Kondoo wangu walitawanyika juu ya uso wa dunia yote bila kuwa na yeyote wa kuwaulizia wala wa kuwatafuta.

7“ ‘Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana: 834:8 2Nya 18:16; 1Pet 2:25; Yer 50:6; Za 95:10; Yer 10:21; Hos 7:13; Za 42:4; Mt 18:12-13Kwa hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa sababu kondoo zangu wamekosa mchungaji na hivyo wametekwa nyara na kuwa chakula cha wanyama wote wa mwituni na kwa sababu wachungaji wangu, hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji wamejitunza wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo zangu, 934:9 Amu 2:14; Isa 59:6; Yud 12kwa hiyo enyi wachungaji, sikieni neno la Bwana: 1034:10 Yer 21:13; Za 72:14; Yer 23:2; Zek 10:3; 1Sam 2:29-30Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na wachungaji nami nitawadai kondoo zangu mikononi mwao. Nitawafukuza kutoka kwenye kuchunga kundi langu, ili wachungaji wasiendelee kujitunza wenyewe. Nitaokoa kondoo zangu kutoka kwenye vinywa vyao, nao kondoo hawatakuwa tena chakula chao.

1134:11 Za 119:176“ ‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitawaulizia kondoo wangu na kuwatafuta. 1234:12 Zek 10:3; Lk 19:10; Eze 30:3; 32:7; Mdo 2:19-21; Isa 40:11Kama vile mchungaji atafutavyo kundi lake lililotawanyika wakati akiwa pamoja nalo, hivyo ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawaokoa kutoka mahali pote walipokuwa wametawanyikia katika siku ya mawingu na giza nene. 1334:13 Mwa 48:21; Yer 23:3, 8; 50:19; Kum 30:4; Eze 11:17Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mbalimbali, nami nitawaleta katika nchi yao wenyewe. Nitawalisha kwenye milima ya Israeli, katika mabonde na mahali pote panapokalika katika nchi. 1434:14 Eze 20:40; 37:22; Za 23:2; 37:3; Isa 65:10; Amo 9:14; Eze 36:29-30Nitawachunga kwenye malisho mazuri na miinuko ya mlima wa Israeli patakuwa mahali pao pa malisho. Huko watajipumzisha kwa amani katika nchi ya malisho mazuri, nao watajilisha huko katika malisho tele katika milima ya Israeli. 1534:15 Sef 3:13; Mik 5:4; Za 23:1-2; Yer 33:12Mimi mwenyewe nitawachunga kondoo zangu na kuwafanya wapumzike, asema Bwana Mwenyezi. 1634:16 Isa 61:1-2; Mik 4:6; Sef 3:19; Yer 31:8; Lk 5:32; Mt 2:17; 15:24Nitawaulizia kondoo waliopotea na kuwaleta waliotangatanga. Nitawafunga waliojeruhiwa na kuwatia nguvu walio dhaifu lakini wale waliojikinai na wenye nguvu nitawaangamiza. Nitalichunga kundi kwa haki.

1734:17 Mt 25:32-33; Eze 20:37“ ‘Kwa habari yenu, enyi kundi langu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo dume na mbuzi. 1834:18 Mwa 30:15; Eze 32:2Je, haiwatoshi ninyi kujilisha kwenye malisho mazuri? Je, ni lazima ninyi kuyakanyaga pia malisho yenu yaliyobaki kwa miguu yenu? Je, haiwatoshi ninyi kunywa maji safi? Je, ni lazima kuyachafua maji mengine kwa miguu yenu? 19Je, ni lazima kundi langu wajilishe kwa yale mliyoyakanyaga na kunywa maji mliyoyachafua kwa miguu yenu?

2034:20 Eze 34:17“ ‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi awaambialo: Tazama, mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo wanono na waliokonda. 2134:21 Kum 33:17Kwa sababu mmewapiga kikumbo na kuwapiga kwa pembe zenu kondoo wote walio dhaifu mpaka wakawafukuza, 2234:22 Za 72:12-14; Yer 23:2-3; Eze 20:37-38nitaliokoa kundi langu na hawatatekwa nyara tena. Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo. 2334:23 Ebr 13:20; Isa 40:11; Eze 37:24; Isa 31:4; Mik 5:4Nitaweka juu yao mchungaji mmoja, mtumishi wangu Daudi, naye atawachunga, atawachunga na kuwa mchungaji wao. 2434:24 Eze 36:28; Yer 33:14; 30:4; Yn 10:16; Kut 29:45; Za 89:49; Isa 53:4; Ufu 7:17Mimi Bwana nitakuwa Mungu wao, naye mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu miongoni mwao. Mimi Bwana nimenena.

2534:25 Law 26:6; 25:18; Hos 2:18; Yer 23:6; Isa 11:6-9; Hes 25:12; Eze 16:62“ ‘Nitafanya nao Agano la amani na kuwaondoa wanyama wa mwitu kutoka nchi yao ili kondoo wangu waweze kupumzika nyikani na msituni kwa salama. 2634:26 Mwa 12:2; Za 68:9; Yoe 2:23; Kum 28:12; 11:13-15Nitawabariki wao pamoja na maeneo yanayozunguka kilima changu. Nitawanyeshea mvua kwa majira yake, kutakuwepo mvua za baraka. 2734:27 Yer 2:20; Law 26:13; Yer 30:8; Eze 20:42; Yer 25:14; Za 72:16; Ay 14:9Miti ya shambani itatoa matunda yake na ardhi itatoa mazao yake, watu watakaa salama katika nchi yao. Watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya nira zao na kuwaokoa kutoka mikono ya wale waliowafanya watumwa. 2834:28 Hos 11:11; Zek 14:11; Amo 9:15; Yer 30:10; 32:37; Eze 28:26; 39:26Hawatatekwa tena nyara na mataifa, wala wanyama pori hawatawala tena. Wataishi kwa salama, wala hakuna yeyote atakayewatia hofu. 2934:29 Isa 4:2; Yoe 2:19; Eze 36:15, 29; Za 137:3Nitawapa nchi yenye sifa kutokana na mazao yake, hawatapatwa na njaa katika nchi tena wala hawatadharauliwa na mataifa. 3034:30 Eze 14:11; 37:27; 2Tim 1:12Ndipo watakapojua kuwa Mimi, Bwana, Mungu wao, niko pamoja nao, na kwamba wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana Mwenyezi. 3134:31 Za 100:3; Yer 23:1; Za 28:9Ninyi ni kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

Swedish Contemporary Bible

Hesekiel 34:1-31

Profetia mot Israels herdar

1Herrens ord kom till mig: 2”Du människa, profetera mot Israels herdar, profetera och säg till dem: ’Så säger Herren, Herren till dessa herdar: Ve er, Israels herdar som bara vallar er själva! Ska inte herdarna valla fåren? 3Ni äter upp grädden, gör kläder av ullen och slaktar de bästa djuren, men ni vallar inte fåren. 4Ni har inte stärkt de svaga, inte helat de sjuka eller förbundit de sårade. Ni har inte heller fört tillbaka de försvunna eller sökt efter de vilsegångna. I stället har ni härskat över dem med hårdhet och grymhet. 5De skingrades eftersom de inte hade någon herde, och blev alla vilddjurens rov. Så skingrades de, 6och så har mina får irrat omkring på alla berg och höjder. Över hela jorden har min fårahjord skingrats, men ingen letar efter dem eller frågar efter dem.

7Hör därför Herrens ord, ni herdar: 8Så sant jag lever, säger Herren, Herren, eftersom mina får blev utan herde blev de ett byte och rov för alla vilddjur. Mina herdar letade inte efter dem utan vallade bara sig själva, inte mina får. 9Hör därför Herrens ord, ni herdar: 10Så säger Herren, Herren: Jag är emot herdarna och ska kräva tillbaka mina får av dem. Jag ska avsätta dem från deras herdeuppgift, så att de inte längre får valla sig själva. Jag ska rycka mina får ur deras gap; de får inte bli deras föda.

11Så säger Herren, Herren: Jag ska söka efter mina får och ta hand om dem. 12Som en herde tar hand om sin hjord när han är bland sina får, de skingrade, så ska jag ta hand om mina får. Jag ska rädda dem från alla de platser dit de blivit utspridda en mörk och dyster dag. 13Jag ska leda dem tillbaka från alla folken och samla dem från olika länder och leda dem tillbaka till deras eget land. Jag ska valla dem på Israels berg och vid floderna och där landet är bebott. 14Jag ska föra dem i bet på goda betesmarker. Israels höjder ska bli deras betesmarker. Där ska de få ligga i lugn och ro på goda betesmarker och äta av frodig grönska på Israels berg. 15Jag ska själv valla mina får och låta dem vila i lugn och ro, säger Herren, Herren. 16Jag ska söka upp de försvunna och föra tillbaka de vilsegångna. Jag ska förbinda de sårade och hela de sjuka. Men de feta och starka ska jag utplåna.34:16 Enligt bl.a. Septuaginta: Jag ska se till de feta och starka. Jag ska valla dem med rättvisa.

Herren som herde

17Och ni, mina får: Så säger Herren, Herren: Jag ska döma mellan får och får, mellan baggar och bockar. 18Är det inte nog för er att få beta på de bästa betesmarkerna? Måste ni också trampa ner de övriga av era betesmarker? Är det inte nog att ni får dricka klart vatten? Måste ni med era fötter grumla det som finns kvar? 19Måste mina får beta av det som ni har trampat ner och dricka av det som ni med era fötter har grumlat?

20Därför säger Herren, Herren till dem: Jag ska själv döma mellan de feta och de magra fåren. 21Ni knuffar med sida och bog alla de svaga och tränger undan dem med era horn tills ni drivit bort och skingrat dem. 22Därför ska jag själv rädda mina får så att de aldrig mer blir till ett byte. Jag ska själv döma mellan fåren.

23Jag ska sätta en herde över dem, min tjänare David, som ska valla dem. Han ska valla dem och vara en herde för dem. 24Jag, Herren, ska vara deras Gud, och min tjänare David ska vara en furste bland dem. Jag, Herren, har talat.

25Jag ska ingå ett fredsförbund med dem. Jag ska utrota vilddjuren i landet, så att man tryggt kan bo i öknen och sova i skogarna. 26Jag ska välsigna dem, mitt berg och dess omgivningar. Jag ska sända regn i rätt tid, skurar av välsignelse ska komma. 27Markens träd ska bära sin frukt och jorden ge sin gröda, och de ska leva i trygghet i sitt land. De ska inse att jag är Herren, när jag bryter sönder deras ok och befriar dem från dem som hållit dem i slaveri. 28De ska inte mer bli ett byte för andra folk, och vilddjuren i landet ska inte äta dem mer. De ska bo i trygghet, och ingen ska skrämma dem.

29Landet där de ska få bo ska vara känt för sina goda skördar, och mitt folk ska aldrig mer behöva svälta eller bli föraktade av andra folk. 30Då ska de inse att jag, Herren, deras Gud, är med dem och att de, israeliterna, är mitt folk, säger Herren, Herren. 31Ni är min hjord, fåren på mina betesmarker. Ni är människor, och jag är er Gud, säger Herren, Herren.’ ”