Ezekieli 28 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 28:1-26

Unabii Dhidi Ya Mfalme Wa Tiro

1Neno la Bwana likanijia kusema: 228:2 Isa 14:13; Mwa 3:4-5; 2The 2:4; Kum 8:14; Mit 16:18; Sef 2:15; Za 9:20“Mwanadamu, mwambie mfalme wa Tiro, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Kwa sababu moyo wako umejivuna

na umesema, “Mimi ni mungu;

nami ninaketi katika kiti cha enzi cha mungu

katika moyo wa bahari.”

Lakini wewe ni mwanadamu, wala si mungu,

ingawa unafikiri kuwa una hekima kama mungu.

328:3 Dan 1:20; 2:20-23, 28; Zek 9:2; Eze 14:14Je, wewe una hekima kuliko Danieli?

Je, hakuna siri iliyofichika kwako?

428:4 Zek 9:3; Isa 10:13Kwa hekima yako na ufahamu wako,

umejipatia utajiri,

nawe umejikusanyia dhahabu

na fedha katika hazina zako.

528:5 Ay 31:25; Hos 13:6; Kum 8:12-14; Isa 23:8; Yer 9:23; 9:23; Eze 27:33Kwa werevu wako mwingi katika biashara,

umeongeza utajiri wako

na kwa sababu ya utajiri wako

moyo wako umekuwa na kiburi.

6“ ‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Kwa sababu unafikiri una hekima,

mwenye hekima kama mungu,

728:7 Eze 32:12; 30:11; 31:12; Yer 9:23; Eze 7:24mimi nitawaleta wageni dhidi yako,

taifa katili kuliko yote;

watafuta panga zao dhidi ya uzuri wa hekima yako,

na kuchafua fahari yako inayongʼaa.

828:8 Za 55:23; Eze 32:30; 27:27; 26:12; Ufu 18:7Watakushusha chini shimoni,

nawe utakufa kifo cha kikatili

katika moyo wa bahari.

928:9 Isa 31:3; Eze 16:49Je, wakati huo utasema, “Mimi ni mungu,”

mbele ya wale wanaokuua?

Utakuwa mwanadamu tu, wala si mungu,

mikononi mwa hao wanaokuua.

1028:10 1Sam 14:6; Yer 9:26; Eze 32:18-19Utakufa kifo cha wasiotahiriwa

kwa mkono wa wageni.

Kwa kuwa mimi nimenena, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

11Neno la Bwana likanijia kusema: 1228:12 Eze 19:1; 27:2-4“Mwanadamu, mfanyie maombolezo mfalme wa Tiro, nawe umwambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ulikuwa kipeo cha ukamilifu,

ukiwa umejaa hekima

na mkamilifu katika uzuri.

1328:13 Mwa 2:8; Eze 31:8-9; 27:16; Ufu 17:4; Isa 14:11; Ufu 21:20Ulikuwa ndani ya Edeni,

bustani ya Mungu;

kila kito cha thamani kilikupamba:

akiki nyekundu, yakuti manjano na zumaridi,

krisolitho, shohamu na yaspi,

yakuti samawi, almasi na zabarajadi.

Kuwekwa kwa hayo mapambo na kushikizwa kwake

kulifanywa kwa dhahabu;

siku ile ulipoumbwa yaliandaliwa tayari.

1428:14 Kut 30:26; 40:9; 25:17-20Ulitiwa mafuta kuwa kerubi mlinzi,

kwa kuwa hivyo ndivyo nilivyokuweka wakfu.

Ulikuwa kwenye mlima mtakatifu wa Mungu;

ulitembea katikati ya vito vya moto.

15Ulikuwa mnyofu katika njia zako

tangu siku ile ya kuumbwa kwako,

hadi uovu ulipoonekana ndani yako.

1628:16 Mwa 6:11; Hab 2:17; Mwa 3:24Kutokana na biashara yako iliyoenea,

ulijazwa na dhuluma,

nawe ukatenda dhambi.

Hivyo nilikuondoa kwa aibu kutoka mlima wa Mungu,

nami nikakufukuza, ee kerubi mlinzi,

kutoka katikati ya vito vya moto.

1728:17 Isa 10:12; Eze 16:49; 31:10; 19:12Moyo wako ukawa na kiburi

kwa ajili ya uzuri wako,

nawe ukaiharibu hekima yako

kwa sababu ya fahari yako.

Kwa hiyo nikakutupa chini;

nimekufanya kioja mbele ya wafalme.

1828:18 Oba 1:18; Mal 4:3; Zek 9:2-4Kwa dhambi zako nyingi na biashara yako ya dhuluma,

umenajisi mahali pako patakatifu.

Kwa hiyo nilifanya moto utoke ndani yako,

nao ukakuteketeza,

nami nikakufanya majivu juu ya nchi,

machoni pa wote waliokuwa wakitazama.

1928:19 Yer 51:64; Eze 26:21; Law 26:21Mataifa yote yaliyokujua

yanakustajabia;

umefikia mwisho wa kutisha

na hutakuwepo tena milele.’ ”

Unabii Dhidi Ya Sidoni

20Neno la Bwana likanijia kusema: 2128:21 Eze 6:2; 13:17; Yer 25:2; Mwa 10:15“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Sidoni, ukatabiri dhidi yake, 2228:22 Kut 14:4; Za 9:16; Eze 30:19; 39:13; Law 10:3nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Mimi ni kinyume chako, ee Sidoni,

nami nitapata utukufu ndani yako.

Nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana,

nitakapotekeleza hukumu zangu

na kuonyesha utakatifu wangu ndani yake.

2328:23 Eze 5:17; 38:22Nitapeleka tauni ndani yake

na kufanya damu itiririke katika barabara zake.

Waliochinjwa wataanguka ndani yake,

kwa upanga dhidi yake kila upande.

Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.

2428:24 Hes 33:55; Yos 23:13; Isa 5:6; Eze 2:6“ ‘Nyumba ya Israeli hawatakuwa tena na majirani wenye nia ya kuwadhuru wanaoumiza kama michongoma na miiba mikali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.

2528:25 Za 106:47; Yer 32:37; Isa 11:12; Eze 20:41; Yer 12:15; 12:15; 23:8; Eze 11:17“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapoikusanya nyumba ya Israeli kutoka mataifa ambako wametawanyika, nitajionyesha kuwa mtakatifu miongoni mwao machoni pa mataifa. Ndipo watakapoishi katika nchi yao wenyewe, niliyompa mtumishi wangu Yakobo. 2628:26 Law 25:18; Yer 23:6; Hos 2:15; Amo 9:14-15; 1Fal 4:25; Yer 17:25; Kum 20:6; Eze 38:8; 39:26-27; Isa 65:21Wataishi humo kwa salama na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu, wataishi kwa salama nitakapowaadhibu majirani zao wote ambao waliwafanyia uovu. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.’ ”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以西结书 28:1-26

预言审判泰尔王

1耶和华对我说: 2“人子啊,你去告诉泰尔王,主耶和华这样说,

“‘你心里高傲,说,我是神明,

我坐在海中神明的宝座上。

你虽然自以为像神明,

但你不过是人,并非神明。

3看啊,你比但以理更有智慧,

什么秘密都瞒不过你。

4你凭智慧和头脑发了财,

金银装满了你的库房。

5你靠高超的经商本领使财富大增,

因而变得心高气傲。

6因此,主耶和华说,

因为你自以为像神明,

7我要使列国中最残暴的外族人来攻打你,

他们必拔刀毁坏你凭智慧得来的美物,

玷污你的荣美,

8使你坠入坟墓,

你必惨死在大海中。

9在杀戮你的人面前,

你还能自称为神明吗?

在杀你的人手中,

你不过是人,并非神明。

10你要像未受割礼的人那样死在外族人手中。’

因为我已经宣告,这是主耶和华说的。”

泰尔王的终局

11耶和华对我说: 12“人子啊,你要为泰尔王唱哀歌,告诉他,主耶和华这样说,

“‘你曾经是完美的典范,

充满智慧,美丽无瑕。

13你曾在上帝的伊甸园中,

你曾佩戴各种宝石,

有红宝石、黄玉、钻石、

绿宝石、红玛瑙、碧玉、

蓝宝石、绿松石、翡翠,

底座镶嵌着精美的黄金,

这些在你受造的那天都已经预备妥当。

14我膏立你为看守约柜的基路伯天使。

我把你安置在上帝的圣山上,

在闪闪发光的宝石中行走。

15你从受造那天开始所行的纯全无过,

但后来在你那里查出不义。

16因为贸易发达,

你便充满暴力,犯罪作恶。

因此,看守约柜的基路伯天使啊,

我把你当作污秽之物逐出上帝的山,

从闪闪发光的宝石中除掉你。

17你因俊美而心高气傲,

因辉煌而心智败坏,

所以我把你扔到地上,

让你在列国的君王面前出丑。

18你多行不义,

交易不公,

亵渎了你的圣所,

因此我使火在你那里燃起,吞噬你,

在众目睽睽之下把你烧成地上的灰烬。

19所有认识你的民族都因你而惊骇,

你落得可怕的下场,

你将永远不复存在。’”

预言审判西顿

20耶和华对我说: 21“人子啊,你要面对西顿,说预言斥责她, 22告诉她,主耶和华这样说,

“‘西顿啊,我要与你为敌,

我要在你那里彰显我的荣耀。

我要审判你,在你中间彰显我的圣洁,

那时,人们就知道我是耶和华。

23我要使瘟疫进入你境内,

刀剑从四面八方临到你,

被杀的人横尸城中,血流街头,

这样人们就知道我是耶和华。

24“‘藐视以色列人的邻邦必不再作刺他们的荆棘,伤他们的蒺藜,这样人们就知道我是主耶和华。’

25“主耶和华说,‘我要把分散到列国的以色列人招聚起来,当着列国的面在他们身上彰显我的圣洁,那时他们要住在自己的土地上,就是我赐给我仆人雅各的地方。 26他们将在那里安然居住,兴建房屋,栽种葡萄园。我审判鄙视他们的四邻后,他们必安然居住。这样,他们便知道我是他们的上帝耶和华。’”