Ezekieli 27 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 27:1-36

Maombolezo Kwa Ajili Ya Tiro

1Neno la Bwana likanijia kusema: 227:2 Eze 19:1; 26:17; 28:12; 32:2“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro. 327:3 Hos 9:13; Isa 23:9; Eze 28:2; Za 83:16Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ee Tiro, wewe umesema,

“Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”

427:4 Eze 28:12Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari,

wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.

527:5 Kum 3:9; Isa 2:13Walizifanya mbao zako zote

kwa misunobari itokayo Seniri;27:5 Yaani Hermoni.

walichukua mierezi kutoka Lebanoni

kukutengenezea mlingoti.

627:6 Za 29:9; Zek 11:2; Mwa 10:4; Isa 23:12; Yer 22:20; Hes 21:33Walichukua mialoni toka Bashani

wakakutengenezea makasia yako;

kwa miti ya msanduku

kutoka pwani ya Kitimu

wakatengeneza sitaha27:6 Yaani sakafu ya merikebu au mashua. yako

na kuipamba kwa pembe za ndovu.

727:7 Kut 25:4; Yer 10:9; Isa 19:9; Mwa 10:4; Kut 26:36Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako,

nacho kilikuwa bendera yako;

chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau

kutoka visiwa vya Elisha.

827:8 Mwa 10:18; 1Fal 9:23-27Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako;

watu wako wenye ustadi, ee Tiro,

walikuwa ndio mabaharia wako.

927:9 Yos 13:5; 1Fal 5:18; Za 104:26Wazee wa Gebali27:9 Yaani Bubilo, mji wa zamani sana wa Ufoinike (kama kilomita 80 kaskazini mwa Beiruti). pamoja na mafundi stadi

walikuwa mafundi wako melini.

Meli zote za baharini na mabaharia wao

walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.

1027:10 Dan 8:20; Mwa 10:6; Nah 3:9; Yer 46:9; Eze 38:5; 2Nya 36:20; Isa 66:19; Wim 4:4“ ‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu

walikuwa askari katika jeshi lako.

Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako,

wakileta fahari yako.

1127:11 Eze 27:27Watu wa Arvadi na wa Heleki

walikuwa juu ya kuta zako pande zote;

watu wa Gamadi

walikuwa kwenye minara yako.

Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako;

wakaukamilisha uzuri wako.

1227:12 Mwa 10:4; 2Nya 20:36“ ‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.

1327:13 Isa 66:19; Ufu 18:13; Yoe 3:6; Mwa 10:2; Eze 32:26; 38:2“ ‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.

1427:14 Mwa 10:3; Eze 38:6“ ‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.

1527:15 Mwa 10:7; Yer 25:22; 1Fal 10:22; Ufu 18:12“ ‘Watu wa Dedani27:15 Yaani Rhodes. walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.

1627:16 Amu 10:6; Isa 7:1-8; Kut 28:18; 39:11; Eze 28:13; 16:10; Ay 28:18“ ‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe27:16 Yaani marijani, jiwe laini la pwani au baharini, kama mawe ya chokaa. na akiki nyekundu.

1727:17 Amu 11:33; Mdo 12:20; Mwa 43:11“ ‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.

1827:18 Mwa 14:15; Eze 47:16-18“ ‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.

1927:19 Kut 30:24; Mwa 10:2, 27“ ‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.

2027:20 Mwa 10:7“ ‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.

2127:21 Mwa 25:13; Isa 60:7; 2Nya 9:14; Isa 21:17“ ‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.

2227:22 1Fal 10:1-2; Isa 60:8; Mwa 43:11; Za 72:10; Ufu 18:12“ ‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.

2327:23 Mwa 11:26; 2Fal 19:12; Isa 37:12; Mwa 10:22; Hes 24:24“ ‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe. 24Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.

2527:25 Mwa 10:4; Isa 2:16; Ufu 18:3“ ‘Merikebu za Tarshishi ndizo

zinazokusafirishia bidhaa zako.

Umejazwa shehena kubwa

katika moyo wa bahari.

2627:26 Mwa 41:6; Za 48:7; Yer 18:7Wapiga makasia wako wanakupeleka

mpaka kwenye maji makavu.

Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande

katika moyo wa bahari.

2727:27 Mit 11:4; Eze 28:8Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako,

mabaharia wako, manahodha wako,

mafundi wako wa meli,

wafanyabiashara wako na askari wako wote,

na kila mmoja aliyeko melini

atazama kwenye moyo wa bahari

siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.

2827:28 Yer 49:21; Eze 26:15Nchi za pwani zitatetemeka

wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.

2927:29 Ufu 18:17Wote wapigao makasia

wataacha meli zao,

mabaharia wote na wanamaji wote

watasimama pwani.

3027:30 Yos 7:6; Yer 6:26; Ufu 18:17-19; Mao 2:10Watapaza sauti zao

na kulia sana kwa ajili yako;

watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao

na kujivingirisha kwenye majivu.

3127:31 Isa 16:9; Ay 3:20; Es 4:1; Law 13:40; Ay 1:20; Isa 3:17; Yer 48:37; Isa 22:12; Mao 2:10; Eze 7:16Watanyoa nywele zao kwa ajili yako,

nao watavaa nguo za magunia.

Watakulilia kwa uchungu wa moyo

na kwa maombolezo makuu.

3227:32 Eze 19:1; 26:17; Isa 23:1-6Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako,

watafanya maombolezo kukuhusu wakisema:

“Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro,

katika moyo wa bahari?”

3327:33 Eze 28:4-5Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini,

ulitosheleza mataifa mengi;

kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako

ulitajirisha wafalme wa dunia.

3427:34 Za 9:4Sasa umevunjavunjwa na bahari,

katika vilindi vya maji,

bidhaa zako na kundi lako lote

vimezama pamoja nawe.

3527:35 Eze 26:15; Law 26:32; Ay 18:20; Eze 32:10Wote waishio katika nchi za pwani

wanakustaajabia;

wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu,

nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.

3627:36 Yer 18:16; Sef 2:15; Eze 26:21; Za 37:10; Yer 19:8; 49:17; 50:13Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka;

umefikia mwisho wa kutisha

nawe hutakuwepo tena.’ ”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以西结书 27:1-36

为泰尔唱哀歌

1耶和华对我说: 2“人子啊,你要为泰尔唱哀歌, 3告诉位于海口、跟沿海各民族通商的泰尔,主耶和华这样说,

“‘泰尔啊,

你曾夸耀自己完美无瑕。

4你的疆域在大海上,

你的建造者把你造得完美无瑕。

5他们用示尼珥的松木做你的船板,

黎巴嫩的香柏木做桅杆,

6巴珊的橡木做你的桨,

把象牙镶嵌在基提沿岸的黄杨木上做甲板,

7埃及来的绣花细麻布做你的帆,

作为你的旗号,

以利沙岛来的蓝布和紫布做船篷。

8西顿亚发的居民是你的船夫,

你的智者在船上为你掌舵。

9迦巴勒的老手和巧匠在船上为你修补船篷,

所有海船和水手都来与你做生意。

10“‘你军队中的战士有波斯人、路德人、人,他们在你的墙上挂起盾牌和头盔,展示你的光彩。 11亚发人和你的军队都守卫在你的城墙上,歌玛底人把守你的城楼,他们在你四围的墙上挂满盾牌,使你完美无瑕。

12“‘他施人因你有丰富的货物,就拿银、铁、锡、铅来跟你交易。 13雅完人、土巴人、米设人也跟你通商,用奴隶和铜器来换取你的货物。 14陀迦玛人用马匹、战马和骡子来跟你交易。 15底但人也是你的客商,你的市场远及沿海一带,他们拿象牙、乌木来跟你交易。 16因为你的货物丰富,亚兰人也成了你的客户,他们用绿宝石、紫布、刺绣、细麻布、珊瑚和红宝石与你交换货物。 17犹大以色列也是你的客商,他们用米匿的麦、饼、蜜、油和香料与你交换货物。 18大马士革见你的货物丰富,就用黑本的酒和沙哈的羊毛来跟你交易。 19乌萨来的威但人和雅完人用熟铁、肉桂、菖蒲与你交换货物。 20底但人用马鞍垫来跟你交易。 21阿拉伯人和基达的所有首领都来做你的客商,他们用羊羔、绵羊和山羊来跟你交易。 22示巴拉玛的商人用各类上等香料、宝石和黄金交换你的货物。 23哈兰干尼伊甸示巴亚述基抹的商人都来跟你交易, 24他们把华丽衣服、蓝布、刺绣和彩色地毯捆扎结实,拿来跟你交易。

25“‘他施的船只替你运货,

你在海上载满沉甸甸的货物。

26船夫把你摇到汪洋之中,

但东风要把你击碎在海中。

27你的财富、货物、商品、

水手、舵手、修补匠、客商、

战士和人民在你倾覆的日子都要沉到深海里。

28你舵手的哀号声必震动海岸,

29所有的船夫、水手、舵手都必弃船登岸,

30为你放声痛哭,

把尘埃撒在头上,

在灰中打滚,

31又为你剃光头发,腰束麻布,

并为你伤心哭泣,痛苦哀号。

32他们在痛哭中为你唱起哀歌,

哀悼你说,

有哪一座城像泰尔一样在深海中销声匿迹呢?

33你的货物由海上运出,

满足了许多国家;

你的资财和货物使地上的君王富裕。

34如今你在汪洋中被海浪击碎,

你的货物和人民都一同沉没了。

35沿海的居民因你而惊骇,

君王都吓得面容失色。

36各国商人都嗤笑你,

你那可怕的末日来临了,

你将永远不复存在。’”