Ezekieli 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 2:1-10

Wito Wa Ezekieli

12:1 Dan 10:11; Mdo 26:16; Ay 25:6; Za 8:4; Eze 1:26; Mdo 9:6; 14:10Akaniambia, “Mwanadamu, simama kwa miguu yako nami nitasema nawe.” 22:2 Eze 3:24; Dan 8:18; Amu 13:25Alipokuwa akiongea nami, Roho akanijia na kunisimamisha wima, nikamsikia akisema nami.

32:3 Yer 3:25; Eze 24:3; 20:8-24Akaniambia: “Mwanadamu, ninakutuma kwa Waisraeli, kwa taifa asi ambalo limeniasi mimi, wao na baba zao wananikosea mimi hadi leo. 42:4 Kut 32:9; Isa 9:9; Eze 3:7; Amo 7:15Watu ambao ninakutuma kwao ni wapotovu na wakaidi. Waambie, ‘Hivi ndivyo anavyosema Bwana Mwenyezi.’ 52:5 Eze 3:11; 3:27; Yn 15:22; Eze 33:33; Yer 5:3Kama watasikiliza au hawatasikiliza, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi, watajua nabii amekuwa miongoni mwao. 62:6 1Pet 3:14; Yer 1:8, 17; Hes 33:55; Mik 7:4Nawe mwanadamu, usiwaogope wao wala maneno yao, usiogope, ingawa michongoma na miiba vinakuzunguka na unaishi katikati ya nge. Usiogope yale wasemayo wala usitishwe nao, ingawa wao ni nyumba ya uasi. 72:7 Yer 7:27; 42:21; Eze 3:10-11; Mt 28:20Wewe lazima uwaambie maneno yangu, ikiwa wanasikiliza au hawasikilizi, kwa kuwa wao ni watu waasi. 82:8 Isa 8:11; 50:5; Ufu 10:9; Za 81:10; Hes 20:10-13; Yer 15:16Lakini wewe mwanadamu, sikiliza ninalokuambia. Usiwe mwenye kuasi kama hiyo nyumba ya kuasi. Fungua kinywa chako na ule nikupacho.”

92:9 Eze 8:3; Yer 1:9; Za 40:7; Yer 36:4; Ufu 5:1-5; 10:8-10Ndipo nikatazama, nami nikaona mkono ulionyooshwa kunielekea. Nao ulikuwa na ukurasa wa kitabu, 102:10 Isa 3:11; Ufu 8:13ambao aliukunjua mbele yangu. Pande zote mbili ulikuwa umeandikwa maneno ya maombolezo, vilio na ole.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以西结书 2:1-10

以西结蒙召

1那声音对我说:“人子啊,你站起来,我要对你说话。” 2正说的时候,耶和华的灵就进入我里面,使我站起来。我听见那声音对我说: 3“人子啊,我派你去那背叛我的国民以色列人那里。他们和他们的祖先至今仍背叛我。 4我派你到那些心里刚硬的人那里,向他们宣告,‘主耶和华这样说。’ 5不管那群叛逆的人听不听,他们都会知道有一位先知在他们当中。 6人子啊,不要怕他们和他们的话,虽然你周围布满荆棘和毒蝎,也不要害怕。他们是一群叛逆的人,你不要怕他们的话,也不要因为他们的脸色而惊慌。 7他们是叛逆的,不论他们听不听,你都要把我的话告诉他们。

8“人子啊,你要听我对你说的话,不要像他们那样叛逆,要张开口吃我赐给你的。” 9这时我观看,见一只手向我伸来,手中拿着书卷。 10那只手把那书卷在我面前打开,书卷的两面都写满了哀伤、叹息和悲痛的话。