Ezekieli 19 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 19:1-14

Maombolezo Kwa Ajili Ya Wakuu Wa Israeli

119:1 Yer 7:29; 2Nya 24:6; Eze 26:17; Yer 9:10, 20; Eze 27:32; 28:12“Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli 219:2 Hes 23:24; Mwa 49:9na useme:

“ ‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike

miongoni mwa simba!

Alilala katikati ya wana simba

na kulisha watoto wake.

319:3 Eze 19:6; 2Fal 23:31, 32Alimlea mmoja wa watoto wake,

naye akawa simba mwenye nguvu.

Akajifunza kurarua mawindo

naye akala watu.

419:4 2Nya 36:4; Mao 4:20; Ay 41:2; 2Fal 23:33-34Mataifa wakasikia habari zake,

naye akanaswa katika shimo lao.

Wakamwongoza kwa ndoana

mpaka nchi ya Misri.

519:5 2Fal 23:34; Mwa 49:9“ ‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki,

nayo matarajio yake yametoweka,

akamchukua mwanawe mwingine

na kumfanya simba mwenye nguvu.

619:6 Yer 22:13; 2Nya 36:9; 2Fal 24:9Alizungukazunguka miongoni mwa simba,

kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu.

Akajifunza kurarua mawindo

naye akala watu.

719:7 Eze 29:10; 30:12Akabomoa ngome zao

na kuiharibu miji yao.

Nchi na wote waliokuwa ndani yake

wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.

819:8 2Fal 24:2, 11; Mao 4:20; Eze 12:13; 2Fal 24:11Kisha mataifa wakaja dhidi yake

kutoka sehemu zilizomzunguka.

Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake,

naye akanaswa katika shimo lao.

919:9 2Fal 25:7; 24:15; 2Nya 36:6; 2Fal 19:28; Zek 11:3Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu

na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli.

Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake

hakukusikika tena

katika milima ya Israeli.

1019:10 Za 80:8-11; Eze 15:2; Yer 17:8; Mwa 49:22“ ‘Mama yako alikuwa kama mzabibu

katika shamba lako la mizabibu

uliopandwa kando ya maji,

ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi

kwa sababu ya wingi wa maji.

1119:11 Eze 31:3; Dan 4:11Matawi yake yalikuwa na nguvu,

yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.

Ulikuwa mrefu kupita miti mingine

katikati ya matawi manene;

ulionekana kwa urahisi

kwa ajili ya urefu wake

na wingi wa matawi yake.

1219:12 Kum 29:28; Eze 17:10; Hos 13:15; Isa 27:11; Eze 28:17; Mwa 41:6Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali

na kutupwa chini.

Upepo wa mashariki uliufanya usinyae,

matunda yake yakapukutika,

matawi yake yenye nguvu yakanyauka

na moto ukayateketeza.

1319:13 Eze 20:35; Hos 2:14; 2:3Sasa umepandwa jangwani

katika nchi kame na ya kiu.

1419:14 Amu 9:15; Eze 20:47; 15:4Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa

na kuteketeza matunda yake.

Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake

lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’

Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”

Nueva Versión Internacional

Ezequiel 19:1-14

Lamento por los príncipes de Israel

1»Dedícale este lamento a los príncipes de Israel:

2»“En medio de los leones,

tu madre era toda una leona.

Recostada entre leoncillos,

amamantaba a sus cachorros.

3A uno de ellos lo crio

y este llegó a ser un león fuerte

que aprendió a desgarrar su presa

y a devorar a la gente.

4Las naciones oyeron de él,

lo atraparon en una fosa

y lo llevaron con garfios a la tierra de Egipto.

5»”Cuando la leona madre perdió toda esperanza,

con sus expectativas perdidas,

tomó a otra de sus crías

y la hizo un león fuerte.

6Cuando este león se hizo fuerte,

merodeaba entre los leones.

Aprendió a desgarrar su presa

y a devorar a la gente.

7Demolía palacios19:7 Demolía palacios (lectura probable; véanse LXX y Targum); Conocía viudas (TM).

y asolaba ciudades.

La tierra y sus habitantes

estaban aterrorizados con sus rugidos.

8Las naciones y provincias vecinas

se dispusieron a atacarlo.

Extendieron su red sobre él

y quedó atrapado en la fosa.

9Enjaulado y con garfios

lo llevaron ante el rey de Babilonia.

Lo pusieron en prisión

para que no se oyeran sus rugidos

en los montes de Israel.

10»”Tu madre era como una vid en medio del viñedo,19:10 del viñedo (dos mss. hebreos); de tu sangre (TM).

plantada junto al agua.

Era fructífera y frondosa,

gracias al agua abundante.

11Sus ramas crecieron vigorosas,

¡aptas para ser cetros de reyes!

Tanto creció que se destacaba

por encima del follaje.

Se le reconocía por su altura

y por sus ramas frondosas.

12Pero fue desarraigada con furia

y arrojada por el suelo.

El viento del este la dejó marchita

y fueron arrancados sus frutos.

Secas quedaron sus vigorosas ramas,

y fueron consumidas por el fuego.

13Ahora está plantada en el desierto,

en tierra árida y reseca.

14De una de sus ramas brotó un fuego

y consumió sus frutos.

¡No queda en ella una rama vigorosa,

apta para ser cetro de gobernante!”.

Este es un lamento y debe entonarse como tal».