Ezekieli 15 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 15:1-8

Yerusalemu Mzabibu Usiofaa

1Neno la Bwana likanijia kusema: 215:2 Za 80:8-16; Yn 15:2; Yer 2:21; Isa 27:2-6; 5:1-7; Hos 10:1“Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu? 315:3 Yer 13:10; Isa 22:23Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake? 415:4 Eze 17:3-10; Yn 15:6; Eze 19:14Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote? 5Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?

6“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu. 715:7 Yer 21:10; Law 26:17; Za 34:16; Isa 24:18; Amo 9:1-4; Eze 14:8; 5:2-4Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana. 815:8 Eze 14:13; 17:20; Amo 5:19; Eze 18:24Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

以西結書 15:1-8

葡萄樹的比喻

1耶和華對我說: 2「人子啊,葡萄木比林中其他木材更好嗎? 3葡萄木有什麼用呢?能用它製造掛鉤掛東西嗎? 4看啊,它只能用來當柴燒。如果火已經燒了它的兩頭,中間也燒黑了,它還有什麼用呢? 5看啊,它完好無損的時候,尚且毫無用處,被火燒後黑豈不更沒用了嗎? 6所以,主耶和華說:我怎樣把林中的葡萄樹扔進火中當柴燒,也必照樣丟棄耶路撒冷的居民。 7我必嚴懲他們。他們縱然火裡逃生,仍要被火燒滅。我嚴懲他們的時候,他們便知道我是耶和華。 8我必使他們的土地荒涼,因為他們對我不忠。這是主耶和華說的。」