Ezekieli 10 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 10:1-22

Utukufu Unaondoka Hekaluni

110:1 Kut 23:10; Eze 1:22; Ufu 4:2-3; Mwa 3:24Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. 210:2 Eze 1:15; 9:2; Ufu 8:5; 2Sam 22:9Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.

3Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani. 410:4 Kut 24:16; Eze 44:4; 1:28Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana. 510:5 Ay 40:9; Eze 1:24; 3:15Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi10:5 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). wakati anapoongea.

610:6 Dan 7:9Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu. 710:7 Eze 5:4Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje. 810:8 Eze 1:8(Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)

910:9 Kut 28:20; Eze 1:15-21; 24:6Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi. 10Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine. 1110:11 Eze 1:17Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda. 1210:12 Ufu 4:6-8; Eze 1:15-21; 24:6Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne. 13Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.” 1410:14 1Fal 7:36; Eze 41:19; Dan 9:21; Ufu 4:7Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.

1510:15 Isa 6:2; Eze 1:3-5; Za 137:1Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari. 1610:16 Eze 1:19Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao. 1710:17 Eze 1:20-21; 3:13Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.

1810:18 Za 78:60; 18:10; Eze 7:20-22; 1Sam 4:21Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi. 1910:19 Eze 11:1-22; 43:4Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.

2010:20 Eze 1:1-8Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi. 2110:21 Eze 1:6, 8Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu. 2210:22 Eze 1:10, 12Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

以西結書 10:1-22

耶和華的榮耀離開聖殿

1我觀看,只見基路伯天使頭頂上的穹蒼之中好像有一個藍寶石寶座。 2耶和華對那穿細麻衣的人說:「你到基路伯天使下邊旋轉的輪子中間,雙手捧滿火炭,撒在城上。」我見他進去了。

3當他進去的時候,基路伯天使站在殿的南邊,內院充滿了雲彩。 4耶和華的榮耀從基路伯天使的上面升起,停在殿的門口,殿裡充滿了雲彩,院子也充滿了耶和華榮耀的光輝。 5基路伯天使展翅的響聲好像全能上帝說話的聲音,在外院也可以聽見。

6祂對那穿細麻衣的人說:「你要從基路伯天使下面旋轉的輪子中取火。」那人便進去,站在一個輪子旁邊。 7有一個基路伯天使伸手到他們中間的火裡,取了些火放在那穿細麻衣的人手裡,那人就拿了出去。 8基路伯天使的翅膀下彷彿有人的手。

9我又看見四個基路伯天使旁各有一個閃耀如綠寶石的輪子。 10四個輪子結構一樣,好像輪套輪。 11基路伯天使移動時,不必轉身就可以向四方移動。前輪朝哪個方向移動,其他輪子也朝哪個方向移動,不必轉向。 12這四個基路伯天使的手、背、翅膀及全身都佈滿了眼睛,包括他們的四個輪子。 13我聽見他們稱這些輪子為「旋轉輪」。 14每一個基路伯天使都有四張臉:第一張是基路伯天使的臉,第二張是人的臉,第三張是獅子的臉,第四張是鷹的臉。

15然後,這些基路伯天使都向上升去,他們就是我在迦巴魯河邊所見的活物。 16基路伯天使移動,輪子也隨之移動;基路伯天使展翅飛離地面,輪子也隨之離開地面,不離他們旁邊; 17基路伯天使停住,輪子也隨之停住;基路伯天使上升,輪子也隨之上升。因為活物的靈在輪子中。

18那時,耶和華的榮耀離開了殿的門口,停在基路伯天使上面。 19我正觀看時,基路伯天使展翅飛離地面,他們旁邊的輪子也隨之飛離。他們停在耶和華殿的東門口,以色列上帝的榮耀在他們上面。 20這些是我在迦巴魯河邊所看見的活物,他們在以色列上帝的下面。我知道他們是基路伯天使。 21他們各有四張臉,兩對翅膀,翅膀下彷彿有人的手, 22他們的面貌和我在迦巴魯河邊所見的一樣,每一個都向前直走。