Ezekieli 10 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 10:1-22

Utukufu Unaondoka Hekaluni

110:1 Kut 23:10; Eze 1:22; Ufu 4:2-3; Mwa 3:24Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. 210:2 Eze 1:15; 9:2; Ufu 8:5; 2Sam 22:9Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.

3Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani. 410:4 Kut 24:16; Eze 44:4; 1:28Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana. 510:5 Ay 40:9; Eze 1:24; 3:15Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi10:5 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). wakati anapoongea.

610:6 Dan 7:9Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu. 710:7 Eze 5:4Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje. 810:8 Eze 1:8(Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)

910:9 Kut 28:20; Eze 1:15-21; 24:6Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi. 10Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine. 1110:11 Eze 1:17Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda. 1210:12 Ufu 4:6-8; Eze 1:15-21; 24:6Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne. 13Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.” 1410:14 1Fal 7:36; Eze 41:19; Dan 9:21; Ufu 4:7Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.

1510:15 Isa 6:2; Eze 1:3-5; Za 137:1Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari. 1610:16 Eze 1:19Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao. 1710:17 Eze 1:20-21; 3:13Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.

1810:18 Za 78:60; 18:10; Eze 7:20-22; 1Sam 4:21Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi. 1910:19 Eze 11:1-22; 43:4Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.

2010:20 Eze 1:1-8Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi. 2110:21 Eze 1:6, 8Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu. 2210:22 Eze 1:10, 12Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Езекиил 10:1-22

Слава Вечного покидает храм

1Я посмотрел и увидел подобие престола из сапфира над сводом, что над головами херувимов. 2Вечный сказал человеку, одетому в льняную одежду:

– Войди между колёсами под херувимами. Возьми полные пригоршни горящих углей, которые между херувимами, и брось на город.

Он вошёл, а я смотрел.

3А херувимы стояли в южной части храма, когда тот человек вошёл, и облако наполняло внутренний двор. 4Слава Вечного поднялась с херувима и перенеслась к порогу храма. Облако наполнило храм, а двор оказался залит сиянием славы Вечного. 5Шум от крыльев херувимов был слышен даже на внешнем дворе, словно голос Всемогущего Бога, когда Он говорит.

6И когда Вечный повелел человеку, одетому в льняную одежду: «Возьми огонь между колёсами, между херувимами», тот человек вошёл и встал у колеса. 7Тогда один из херувимов протянул руку к огню, который был между херувимами, взял огонь и положил в руки человека, одетого в льняную одежду, который взял его и вышел. 8(Под крыльями херувима видны были подобия человеческих рук.)

9Я посмотрел и увидел рядом с херувимами четыре колеса, по одному рядом с каждым из херувимов; колёса искрились, как хризолит. 10Что до их вида, то все четыре выглядели одинаково, словно колесо в колесе. 11Двигаясь, они могли направляться в любую из четырёх сторон, куда были обращены херувимы; когда херувимы передвигались, колёса не поворачивались. Херувимы шли в ту сторону, куда была обращена голова, не оборачиваясь на ходу. 12Все их тела, спины, руки и крылья были повсюду полны глаз, точно так же, как и их четыре колеса. 13Я слышал, как колёса называли «смерчами». 14У каждого из херувимов было четыре лица: одно – лицо херувима, другое – лицо человека, третье – лицо льва, а четвёртое – лицо орла.

15Херувимы поднялись. Это были те самые живые существа, которых я видел у реки Кевар. 16Когда херувимы двигались, двигались и колёса рядом с ними, а когда херувимы расправляли крылья, чтобы подняться с земли, то и колёса оставались рядом с ними. 17Когда херувимы останавливались, останавливались и колёса, а когда херувимы поднимались, и они поднимались с ними, потому что дух живых существ был в них.

18Слава Вечного покинула место над порогом храма и остановилась над херувимами. 19На моих глазах херувимы расправили крылья и поднялись с земли; когда они двигались, колёса двигались вместе с ними. Они остановились у входа в восточные ворота дома Вечного, и слава Бога Исроила была над ними.

20Это были живые существа, которых я видел в подножии Бога Исроила у реки Кевар, и я понял, что это были херувимы. 21У каждого из них было по четыре лица и крыла, а под крыльями у них были подобия человеческих рук. 22Их лица выглядели так же, как и те, что я видел у реки Кевар. Каждый двигался лицом вперёд.