Ezekieli 10 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 10:1-22

Utukufu Unaondoka Hekaluni

110:1 Kut 23:10; Eze 1:22; Ufu 4:2-3; Mwa 3:24Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. 210:2 Eze 1:15; 9:2; Ufu 8:5; 2Sam 22:9Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.

3Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani. 410:4 Kut 24:16; Eze 44:4; 1:28Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana. 510:5 Ay 40:9; Eze 1:24; 3:15Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi10:5 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). wakati anapoongea.

610:6 Dan 7:9Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu. 710:7 Eze 5:4Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje. 810:8 Eze 1:8(Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)

910:9 Kut 28:20; Eze 1:15-21; 24:6Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi. 10Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine. 1110:11 Eze 1:17Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda. 1210:12 Ufu 4:6-8; Eze 1:15-21; 24:6Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne. 13Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.” 1410:14 1Fal 7:36; Eze 41:19; Dan 9:21; Ufu 4:7Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.

1510:15 Isa 6:2; Eze 1:3-5; Za 137:1Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari. 1610:16 Eze 1:19Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao. 1710:17 Eze 1:20-21; 3:13Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.

1810:18 Za 78:60; 18:10; Eze 7:20-22; 1Sam 4:21Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi. 1910:19 Eze 11:1-22; 43:4Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.

2010:20 Eze 1:1-8Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi. 2110:21 Eze 1:6, 8Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu. 2210:22 Eze 1:10, 12Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.

La Bible du Semeur

Ezéchiel 10:1-22

La gloire de l’Eternel quitte le Temple

1Je regardai et je vis dans l’étendue céleste qui s’étendait au-dessus de la tête des chérubins comme une pierre de saphir ; au-dessus de cette pierre, on apercevait quelque chose qui paraissait ressembler à un trône10.1 Voir 1.26.. 2Il dit à l’individu vêtu de lin : Passe entre les roues qui sont sous les chérubins et remplis tes mains des braises incandescentes qui se trouvent entre les chérubins, et répands-les sur la ville.

Il s’exécuta sous mes yeux10.2 Voir 1.13-21 ; cf. 2 R 25.8-9.. 3Or, les chérubins se tenaient à droite du Temple au moment où l’individu se rendit vers eux, et la nuée remplit le parvis intérieur. 4La gloire de l’Eternel s’était élevée de dessus le chérubin pour se diriger vers le seuil de la maison ; alors le Temple fut rempli par la nuée, et le parvis resplendit de l’éclat de la gloire de l’Eternel. 5Le bruissement des ailes des chérubins se fit entendre jusque dans le parvis extérieur. C’était comme la voix du Dieu tout-puissant quand il parle.

6Quand il avait ordonné à l’individu vêtu de lin : « Prends du feu entre les roues et entre les chérubins », l’individu y était allé et il se tenait à côté d’une roue. 7L’un des chérubins avança la main vers le feu qui était entre les chérubins. Il en retira des braises et les mit dans les mains de l’individu vêtu de lin. Celui-ci les prit et se retira. 8Alors apparut, sous les ailes des chérubins, une forme de main humaine.

9Je regardai et je vis quatre roues à côté des chérubins, une roue à côté de chacun d’eux. Elles avaient l’éclat de la chrysolithe. 10Toutes les quatre étaient pareilles et paraissaient imbriquées au milieu l’une de l’autre. 11Elles pouvaient donc se déplacer dans les quatre directions sans se tourner ; en effet, elles allaient du côté vers lequel se tournait la tête, sans pivoter dans leur mouvement. 12Tout le corps des chérubins, leurs dos et leurs mains, leurs ailes et les roues, étaient couverts d’yeux tout autour. Chacun des quatre avait sa roue. 13J’entendis qu’on donnait à ces roues le nom de tourbillon. 14Chacun des êtres vivants avait quatre faces. Les premières faces étaient des faces de chérubin, les deuxièmes des faces d’homme, les troisièmes des faces de lion et les quatrièmes des faces d’aigle.

15Les chérubins s’élevèrent : c’étaient les êtres vivants que j’avais vus sur les bords du canal du Kebar10.15 Voir 1.5 et note.. 16Quand les chérubins se déplaçaient, les roues se déplaçaient à côté d’eux, et quand ils déployaient leurs ailes pour s’élever au-dessus de la terre, les roues ne se détournaient pas d’eux, mais restaient à leurs côtés. 17Quand ils s’arrêtaient, elles s’arrêtaient, quand ils s’élevaient, elles s’élevaient avec eux, car l’Esprit qui animait les êtres vivants était aussi dans les roues.

18La gloire de l’Eternel quitta le seuil du Temple et vint se placer sur les chérubins. 19Ceux-ci déployèrent leurs ailes et s’élevèrent de terre sous mes yeux ; ils sortirent, et les roues sortirent avec eux. Ils s’arrêtèrent à l’entrée de la porte orientale du temple de l’Eternel et la gloire du Dieu d’Israël reposait sur eux tout au-dessus10.19 Voir 8.4 et note.. 20C’étaient les êtres vivants que j’avais vus au-dessous du Dieu d’Israël près du canal du Kebar, et je reconnus que c’étaient des chérubins. 21Chacun d’eux avait quatre faces et quatre ailes, sous lesquelles apparaissaient ce qui était comme des mains humaines. 22Leurs faces avaient la même apparence que celles que j’avais vues près du canal du Kebar, elles avaient le même aspect ; c’étaient bien eux. Chacun des êtres avançait droit devant lui.