Esta 1 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Esta 1:1-22

Malkia Vashti Aondolewa

11:1 Ezr 4:16; Es 9:30Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.1:1 Kushi hapa ina maana ya Ethiopia. 2Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani. 31:3 1Fal 3:15Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.

4Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake. 51:5 Amu 14:17; 2Fal 21:18Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani. 61:6 Eze 23:41; Amo 3:12; 6:4Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani. 7Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake. 8Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.

9Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.

101:10 Rut 3:7; Dan 5:1-4Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi, 11kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza. 121:12 Mwa 39:19; Mit 19:12Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.

131:13 1Nya 12:32Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati, 14nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.

15Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”

16Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero. 17Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’ 18Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.

191:19 Es 8:6; Dan 6:8, 12“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye. 20Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”

21Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza. 221:22 Neh 13:24Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

New Russian Translation

Есфирь 1:1-22

Наказание царицы Астинь за непослушание

1Это произошло во времена Ксеркса1:1 Ксеркс I, сын Дария I Великого (Гистаспа), правил Персидской империей в 486–465 гг. до н. э. Ахашверо́ш — еврейский вариант персидского имени Ксеркс. — того самого Ксеркса, который правил ста двадцатью семью провинциями, простирающимися от Индии до самого Куша1:1 Территория южнее Египта.. 2В те времена престол царя Ксеркса находился в крепости города Сузы. 3На третий год царствования он устроил пир для всех своих сановников и знати. Там были военачальники1:3 Букв.: военная сила. Персии и Мидии, знатные люди и наместники провинций.

4Целых сто восемьдесят дней показывал он великое богатство своего царства, блеск и славу своего величия. 5Когда эти дни минули, царь устроил для всех, от малого до великого, кто только был в крепости Сузы, семидневный пир в закрытом саду царского дворца. 6Сад был украшен завесами из белого и голубого льна, прикрепленными белыми льняными и пурпурными шнурами к серебряным кольцам на мраморных столбах. Золотые и серебряные ложа стояли на помосте, выстланном порфиром, мрамором, перламутром и другими дорогими камнями. 7Вино подавалось в золотых кубках, среди которых не было двух одинаковых, и царского вина было по щедрости царя в изобилии. 8По царскому повелению каждый гость мог пить столько, сколько хотел, потому что царь приказал виночерпиям служить всем, кто пожелает.

9Царица Астинь1:9 Евр. Вашти́. тоже устроила пир для женщин во дворце царя Ксеркса.

10На седьмой день, когда царь Ксеркс был весел от вина, он приказал семи евнухам, которые служили ему, — Мехуману, Бизте, Харбоне, Бигте, Авагте, Зетару и Каркасу — 11привести к нему царицу Астинь в ее царском венце, чтобы показать ее красоту народу и сановникам, ведь облик ее был прекрасен. 12Но царица Астинь отказалась прийти по приказу царя, переданному через евнухов. Тогда царь пришел в ярость и воспылал гневом.

13Он стал советоваться с мудрецами, знающими времена (потому что в обычае у царя было советоваться со всеми, кто был сведущ в законах и обычаях, 14а ближайшими к нему были Каршена, Шетар, Адмата, Таршиш, Мерес, Марсена и Мемухан — семеро сановников Персии и Мидии, у которых был особый доступ к царю и которые стояли выше всех в царстве):

15— Как по закону следует поступить с царицей Астинь, раз она не исполнила повеление царя Ксеркса, переданное ей через евнухов?

16Мемухан сказал царю и сановникам:

— Царица Астинь виновна не только перед царем, но и перед всеми его сановниками и народами всех провинций царя Ксеркса. 17Теперь о поступке царицы узнают все женщины и начнут презирать своих мужей, говоря: «Царь Ксеркс повелел привести к нему царицу Астинь, а она не пришла». 18Сегодня же знатные женщины Персии и Мидии, услышав о поступке царицы, взбунтуются против своих мужей, и тогда презрению жен и гневу мужей не будет конца! 19Поэтому, если угодно царю, пусть он издаст указ, что Астинь никогда больше не войдет к царю Ксерксу. Пусть это будет занесено в законы Персии и Мидии, которые не отменяются. И пусть царь отдаст ее царский сан другой, которая будет лучше нее. 20И когда царский указ будет провозглашен по всему огромному царству, все женщины будут чтить своих мужей, от малого до великого.

21Этот совет понравился царю и его сановникам, и царь сделал так, как предлагал Мемухан. 22Он отправил послания во все части царства, в каждую провинцию ее письменами и каждому народу на его языке, что каждый мужчина должен быть господином в своем доме. Об этом объявили на всех языках.