Ndoto Ya Nebukadneza
12:1 Mwa 20:3; 41:8; Ay 33:15-18; Es 6:1; Dan 6:18; 4:5Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala. 22:2 Mwa 41:8; Kut 7:11; Yer 27:9; Isa 9:13; 44:25; Dan 4:6Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme, 32:3 Dan 4:5akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”
42:4 Ezr 4:7; Neh 2:3; Dan 5:10Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu,2:4 Kutoka hapa hadi Dan 7:28, mwandishi aliandika na Kiaramu. “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”
52:5 Ezr 6:11; Dan 3:29; Mwa 41:32Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi. 62:6 Dan 5:7, 16Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”
7Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”
8Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti: 92:9 Es 4:11; Isa 41:22-24; 2:10Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”
102:10 Dan 3:8; 4:7; 5:8Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote. 112:11 Kut 8:10; Mwa 41:38; Dan 5:11Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”
122:12 Dan 3:13-19; Mit 16:14; 28:15Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli. 132:13 Dan 1:20; 5:19Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.
14Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara. 15Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo. 16Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.
17Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo. 182:18 Isa 37:4; Yer 33:3; Ufu 11:13; Ezr 1:2; Neh 1:4Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli. 192:19 Ay 33:15; Dan 1:17; Hes 12:6; Yos 22:23Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni, 202:20 Za 113:2; 145:1-2; Ay 9:4; Yer 32:19; Ay 12:13na akasema:
“Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele;
hekima na uweza ni vyake.
212:21 Dan 7:25; Ay 12:19; Rum 13:1; Yak 1:5; Yer 27:5; Za 75:6-7; 2Sam 14:17; Dan 4:17Yeye hubadili nyakati na majira;
huwaweka wafalme na kuwaondoa.
Huwapa hekima wenye hekima,
na maarifa wenye ufahamu.
222:22 Mwa 40:8; 1Kor 2:10; Ay 12:22; Ebr 4:13; Isa 45:7; Yak 1:17; Za 139:11-12; Dan 4:17Hufunua siri na mambo yaliyofichika;
anajua yale yaliyo gizani,
nayo nuru hukaa kwake.
232:23 Mwa 31:5; Kut 3:15; Dan 1:17; Eze 28:3Ninakushukuru na kukuhimidi,
Ee Mungu wa baba zangu:
Umenipa hekima na uwezo,
umenijulisha kile tulichokuomba,
umetujulisha ndoto ya mfalme.”
Danieli Aifasiri Ndoto
242:24 Eze 28:3Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”
252:25 Dan 5:13; 6:13; Kum 21:10; Dan 1:6Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”
262:26 Dan 1:7Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”
272:27 Mwa 41:8Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza, 282:28 Yer 10:7; Amo 4:13; Dan 4:5; Mwa 40:8; Dan 10:14; Mt 24:6; Eze 28:3; Dan 1:20lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:
29“Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea. 302:30 Mwa 41:16; Mdo 3:12; Isa 45:3; Amo 4:13; Dan 1:7Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.
312:31 Isa 25:3-5; Hab 1:7“Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake. 32Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba, 33miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa. 342:34 Ay 12:19; Zek 4:6; Isa 60:12; Dan 8:25; Ay 34:24; Za 2:9Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja. 352:35 Isa 41:15-16; 2:3; Ufu 11:15; Za 37:10; Isa 17:13; Zek 12:3; Za 1:4Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.
362:36 Mwa 40:12“Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme. 372:37 Ezr 7:12; Eze 26:7; Yer 27:7; Dan 4:26Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu. 382:38 Dan 4:21; Yer 27:6; Dan 5:18Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.
392:39 Dan 7:5“Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote. 402:40 Dan 7:7; Yn 11:48; Dan 7:232:40 Ufu 12:3; Eze 40:2; Dan 8:7-10Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote. 41Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi. 42Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu. 43Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.
442:44 Mwa 27:29; Mt 21:43-44; 1Sam 9:20; Isa 60:12; Ufu 11:15; 1Kor 15:24-25; Za 145:13; Isa 9:7; Dan 4:34; 6:26; 7:14, 27; Oba 1:12; Mik 4:7, 13; Lk 1:33“Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele. 452:45 Isa 28:16; Dan 8:25; Mwa 41:25; Ufu 22:6Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande.
“Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”
462:46 Mdo 10:25; Dan 8:17; Mdo 14:13; Ezr 6:10Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba. 472:47 Kum 10:17; Dan 11:36; 4:25; 1Tim 6:15; Dan 4:25; 4:9Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”
482:48 Es 8:2; Dan 8:27; Mwa 41:40; 2Fal 25:28; Dan 1:20; 4:9; 5:11Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote. 492:49 Dan 3:30; Mit 28:12; 1:7; Es 2:19; Amo 5:15; Dan 6:2; 3:30Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.
Сон Навуходоносора
1На втором году правления Навуходоносора (в 603 г. до н. э.) приснились ему сны; он встревожился духом и не мог заснуть. 2Тогда царь призвал всех чародеев, волшебников, колдунов и астрологов, чтобы они рассказали, что ему приснилось. Когда они пришли и встали перед царём, 3он сказал им:
– Мне снился сон, и я тревожусь духом, желая понять, что это был за сон.
4Тогда астрологи ответили царю по-арамейски:
– О царь, живи вечно! Расскажи нам, твоим рабам, этот сон, и мы истолкуем его.
5Царь ответил астрологам:
– Вот что я решил: если вы сами не расскажете мне содержание сна и его истолкование, то вас разрубят на куски, а ваши дома разрушат до основания. 6Но если вы расскажете мне этот сон и истолкуете его, то получите от меня подарки, награды и великие почести. Итак, расскажите мне этот сон и истолкуйте его.
7Они ответили ещё раз:
– Пусть царь расскажет своим рабам сон, а мы истолкуем его.
8Тогда царь сказал:
– Я точно знаю, что вы стараетесь выиграть время, так как знаете, что я твёрдо решил 9наказать вас, если не расскажете мне мой сон. Поэтому вы и сговорились лгать и обманывать меня в надежде, что дело изменится. Итак, расскажите мне сон, и я узнаю, что вы можете мне его и истолковать.
10Астрологи ответили царю:
– На земле нет человека, который мог бы сделать то, чего просит царь! Никакой царь, как бы он ни был велик и могуществен, никогда не просил такого ни у одного чародея, волшебника или астролога. 11То, о чём просит царь, слишком трудно. Никто не может открыть этого царю, кроме богов, а они среди людей не живут.
12Это так разгневало и разъярило царя Вавилона, что он приказал казнить всех мудрецов Вавилона. 13Был издан указ предать смерти всех мудрецов. Искали и Дониёла с его друзьями, чтобы предать их смерти.
14Когда Ариох, начальник царских стражей, вышел предать смерти вавилонских мудрецов, Дониёл заговорил с ним с мудростью и рассудительностью. 15Он спросил царского сановника:
– Почему царь издал такой суровый указ?
И Ариох рассказал обо всём Дониёлу. 16Тогда Дониёл пошёл к царю и попросил дать ему время, чтобы истолковать его сон.
17Дониёл вернулся домой и рассказал об этом своим друзьям – Ханании, Мисаилу и Азарии. 18Он велел им просить у Бога2:18 Бог – на языке оригинала: «Элах» – слово, родственное арабскому «Аллах». Это имя Всевышнего часто встречается в этой книге. См. приложение V. небесного милости, чтобы Он открыл им эту тайну, и они не были казнены вместе с остальными вавилонскими мудрецами. 19Ночью эта тайна была открыта Дониёлу в видении.
Дониёл восславил Бога небесного 20такими словами:
– Слава имени Твоему, Всевышний, вовеки;
у Тебя мудрость и сила.
21Ты сменяешь времена и эпохи;
Ты возводишь и низлагаешь царей.
Ты даёшь мудрость мудрым
и знание – разумным.
22Ты открываешь глубокое и сокровенное;
Ты знаешь, что таится во тьме,
и свет обитает с Тобой.
23Благодарю и славлю Тебя, Бог моих предков,
потому что Ты дал мне мудрость и силу;
Ты открыл мне то, о чём мы Тебя молили,
Ты открыл нам царский сон!
Дониёл толкует сон
24Дониёл пошёл к Ариоху, которому царь велел казнить вавилонских мудрецов, и сказал ему:
– Не казни вавилонских мудрецов. Отведи меня к царю, и я истолкую ему его сон.
25Ариох тотчас же отвёл Дониёла к царю и сказал:
– Я нашёл среди пленников из Иудеи человека, который может рассказать царю, что означает его сон.
26Царь спросил Дониёла (называемого также Валтасисаром):
– Ты можешь рассказать мне о том, что я видел во сне, и истолковать это?
27Дониёл ответил:
– Ни один мудрец, волшебник, чародей или колдун не мог открыть царю тайны, о которой он спрашивал, 28но на небе есть Бог, открывающий тайны. Он показал царю Навуходоносору то, что должно произойти в последние дни. Вот сон и видения, которые ты видел, лёжа в постели.
29Когда ты лежал в постели, о царь, ты размышлял о будущем, и Открывающий тайны показал тебе то, что должно произойти. 30А мне эта тайна была открыта не потому, что у меня больше мудрости, чем у прочих людей, но для того, чтобы ты, царь, мог узнать истолкование и понять то, о чём размышлял.
31Ты увидел, о царь, стоявшую перед тобой большую статую – огромную, сияющую ослепительным блеском, ужасную на вид. 32Голова статуи была из чистого золота, грудь и руки из серебра, живот и бёдра из бронзы, 33ноги из железа, а ступни частью из железа, частью из обожжённой глины. 34Пока ты смотрел, от горы откололся камень без помощи человеческих рук. Он ударил статую по ступням из железа и обожжённой глины и раздробил их. 35И в тот же миг железо, обожжённая глина, бронза, серебро и золото разбились на куски и стали как мякина на току летом. Ветер унёс их, не оставив и следа. Но камень, который ударил в статую, превратился в огромную гору и заполнил всю землю.
36Таков был сон, а теперь истолкуем его царю. 37Ты, о царь, есть царь царей. Бог небесный дал тебе владычество и силу, могущество и славу; 38Он отдал в твои руки человеческий род, полевых зверей и небесных птиц. Где бы они ни жили, Он сделал тебя правителем над всеми ними. Ты и есть та золотая голова.
39После тебя поднимется другое царство, уступающее твоему. После него – третье царство, бронзовое, которое будет править всей землёй. 40Наконец, явится четвёртое царство, крепкое, как железо, – ведь железо всё разбивает и всё крушит, – и как всесокрушающее железо, оно раздробит и сокрушит все остальные. 41И как ты видел то, что ступни и пальцы ступней были частью из обожжённой глины и частью из железа, так и царство это будет разделённым; но будет в нём и от крепости железа, ведь ты видел, что железо смешано с обожжённой глиной. 42Так как пальцы ступней были частью из железа и частью из глины, то и царство это будет частью крепким, частью хрупким. 43И как ты видел железо, смешанным с обожжённой глиной, так и его народ будет смешанным2:43 Букв.: «они смешаются через человеческое семя»., но не пребудет в единстве, как невозможно смешать железо и глину2:31-43 Золотая голова статуи символизирует Навуходоносора, точнее всю вавилонскую монархию, грудь и руки – Мидо-Персидскую империю, живот и бёдра – Греческую, а ноги и ступни – Римскую империи. Согласно другой трактовке видения второе царство – это Мидия, а третье и четвёртое – это Персия и Греция..
44В дни тех царей Бог небесный установит царство, которое никогда не погибнет и не перейдёт к другому народу. Оно сокрушит все эти царства и положит им конец, но само пребудет вовеки. 45Таково значение камня, отколовшегося от горы без помощи человеческих рук – камня, что разбил железо, бронзу, обожжённую глину, серебро и золото на куски2:44-45 Пятое царство – это вечное Царство Всевышнего, которое распространяется во всём мире (см. ст. 35; Мат. 13:31-32; Лк. 16:16; Отк. 11:15)..
Великий Бог показал царю то, что произойдёт в будущем. Истинен сон и верно истолкование.
46Тогда царь Навуходоносор пал на колени перед Дониёлом и повелел почтить его приношениями и возжиганием благовоний.
47Царь сказал Дониёлу:
– Несомненно, ваш Бог есть Бог богов и Владыка царей, открывающий тайны, раз ты смог открыть эту тайну.
48Затем царь возвысил Дониёла и дал ему множество ценных подарков. Он сделал его правителем всей провинции Вавилон и главой всех её мудрецов. 49Дониёл попросил царя, и царь поставил Шадраха, Мисаха и Аведнего над делами провинции Вавилон. Сам же Дониёл остался при царском дворе.