Ayubu 4 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 4:1-21

Elifazi Anazungumza: Ayubu Ametenda Dhambi

14:1 Mwa 36:11; Ay 15:1; 22:1Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:

24:2 Yer 4:19; 20:9; Ay 32:20“Kama mtu akithubutu kuzungumza nawe,

kutakukasirisha?

Lakini ni nani awezaye

kujizuia asiseme?

34:3 Sef 3:16; Hos 6:3; Ebr 12:12; Kum 32:2; Ay 29:23; 26:2; Za 71:9; Isa 13:7; 35:3Fikiri jinsi ambavyo umewafundisha watu wengi,

jinsi ambavyo umeitia nguvu

mikono iliyokuwa dhaifu.

44:4 Yer 31:8; Ay 16:5; 29:16, 25; Isa 1:17; 35:3; Ebr 12:12Maneno yako yamewategemeza wale waliojikwaa;

umeyatia nguvu magoti yaliyokuwa dhaifu.

54:5 Rut 1:13; Za 38:2; Ay 6:14; Mit 24:10; Lk 4:23Lakini sasa hii taabu imekujia wewe,

nawe unashuka moyo;

imekupiga wewe,

nawe unafadhaika.

64:6 Mwa 6:9; Za 71:5; Mit 3:26; Ay 1:1; 1Fal 18:19Je, kumcha Mungu kwako hakupaswi kuwa

ndiyo matumaini yako

na njia zako kutokuwa na lawama

ndilo taraja lako?

74:7 Za 41:12; 91:9-10; 37:25; 2Pet 2:9; Mit 12:21; Ay 5:11; 36:7; Mt 19:23“Fikiri sasa: Ni mtu yupi asiye na hatia ambaye aliwahi kuangamia?

Ni wapi wanyofu waliwahi kuangamizwa?

84:8 Amu 14:18; Gal 6:7-8; Hos 8:7; Za 7:14; Yos 1:9; Ay 5:3; 15:17; 5:6; 15:35; Mt 11:18Kwa jinsi ambavyo mimi nimechunguza,

wale walimao ubaya

na wale hupanda uovu,

huvuna hayo hayo hayo.

94:9 Kut 15:10; 2The 2:8; Law 26:38; Isa 25:7; Ay 41:21; 40:13Kwa pumzi ya Mungu huangamizwa;

kwa mshindo wa hasira zake huangamia.

104:10 Ay 38:15; 29:17; Za 22:13; 17:12; 22:21; Mt 28:15Simba anaweza kunguruma na kukoroma,

lakini bado meno ya simba mkubwa huvunjika.

114:11 Kum 28:41; Mit 30:14; Ay 5:4; Za 34:10; 58:6; Ay 27:14; 29:17Simba anaweza kuangamia kwa kukosa mawindo,

nao wana wa simba jike hutawanyika.

124:12 Ay 26:14; 33:14; 32:13; 12:23; Yer 9:23; Za 78:59“Neno lililetwa kwangu kwa siri,

masikio yangu yakasikia mnongʼono wake.

134:13 Ay 33:15Katikati ya ndoto za kutia wasiwasi wakati wa usiku,

hapo usingizi mzito uwapatapo wanadamu,

144:14 Dan 10:8; Hab 3:16; Ay 21:6; Za 48:6; 55:5; 119:120, 161; Yer 5:22; 2Kor 7:15hofu na kutetemeka kulinishika

na kufanya mifupa yangu yote itetemeke.

154:15 Za 104:4; Mt 14:26; Ebr 1:14; Dan 5:6; 7:15, 28; 10:8Kuna roho aliyepita mbele ya uso wangu,

nazo nywele za mwili wangu zikasimama.

164:16 1Fal 19:12Yule roho akasimama,

lakini sikuweza kutambua kilikuwa kitu gani.

Umbo fulani lilisimama mbele ya macho yangu,

kukawa na ukimya kisha nikasikia sauti:

174:17 Za 143:2; Mdo 17:24; Mal 2:10; Mit 20:9; Ay 9:2; 8:3; 10:3; 14:4; 15:14; 13:18; Mhu 7:20; Isa 51:13‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu?

Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake?

184:18 Ay 25:5; 21:22; 5:4; 1Pet 2:4; Ebr 1:14Kama Mungu hawaamini watumishi wake,

kama yeye huwalaumu malaika zake kwa kukosea,

194:19 Isa 64:8; 2Kor 4:7; 2Pet 2:4; Mwa 2:7ni mara ngapi zaidi wale waishio katika nyumba

za udongo wa mfinyanzi,

ambazo misingi yake ipo mavumbini,

ambao wamepondwa kama nondo!

204:20 Za 89:47; 90:5-6; Yak 4:14; Ay 14:2, 20; 15:33; 20:7Kati ya mawio na machweo

huvunjwa vipande vipande;

bila yeyote kutambua,

huangamia milele.

214:21 Ay 8:22; Isa 38:12; Mit 5:23; Yn 8:24; Yer 9:3Je, kamba za hema yao hazikungʼolewa,

hivyo hufa bila hekima?’