Ayubu 35 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 35:1-16

Elihu Analaumu Mtu Kujiona Kuwa Mwenye Haki

1Ndipo Elihu akasema:

235:2 Ay 33:32; 2:9; 32:2“Je, unadhani hili ni haki?

Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’

335:3 Ay 21:15; 34:9Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata,

na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’

4“Ningependa nikujibu wewe

pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe.

535:5 Kum 10:14; Mwa 15:5; Ay 22:12; Za 19:1-4Tazama juu mbinguni ukaone;

yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.

635:6 Ay 7:20; Mit 8:36Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu?

Kama dhambi zako zikiwa nyingi,

hilo linamfanyia nini Mungu?

735:7 Rum 11:35; Mit 9:12; 1Kor 4:7; Lk 17:10Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini,

au yeye anapokea nini mkononi kwako?

835:8 Eze 18:24; 18:5-9; Zek 7:9-10Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe,

nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.

935:9 Kut 2:23; Ay 5:15; 12:19; Lk 18:3-7“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso;

huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.

1035:10 Ay 4:17; Isa 51:13; Za 77:6; Mdo 16:25; 1Pet 4:19Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu,

yeye anifanyaye niimbe usiku,

1135:11 Za 94:12; Lk 12:24; Ay 32:8yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia,

na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’

1235:12 1Sam 8:18; Mit 1:1Yeye hajibu wakati watu waliapo

kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

1335:13 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Ay 15:31; Mit 15:8Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili;

Mwenyezi hayazingatii.

1435:14 Ay 9:11; Yer 11:11Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza

wewe usemapo humwoni,

tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake

na wewe lazima umngojee,

15pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu

wala haangalii uovu hata kidogo?

1635:16 Ay 34:35-37; 1Kor 4:20Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana;

anaongea maneno mengi bila maarifa.”

Het Boek

Job 35:1-16

1Elihoe vervolgde, en sprak: 2Houdt ge dit voor behoorlijk, Noemt ge dit “mijn rechtvaardiging voor God”, 3Als ge vraagt: Wat baat het mij, Wat voordeel heb ik, als ik niet zondig? 4Ik zal u antwoord geven op uw vraag, En aan uw vrienden met u. 5Blik naar de hemel op, en zie, Aanschouw de wolken, hoog boven u uit! 6Wanneer ge zondigt, wat deert het Hem; Zijn uw misdrijven talrijk, wat doet het Hem; 7Zijt ge rechtschapen, wat schenkt ge Hem, Of wat ontvangt Hij van u? 8Uw boosheid raakt enkel den mens, als gij, Uw gerechtigheid het mensenkind! 9Men klaagt wel over allerhande verdrukking En jammert onder de macht der tyrannen, 10Maar men zegt niet: Waar is God, die ons schiep, Die ons visioenen geeft in de nacht, 11Die ons onderricht door de dieren der aarde Door de vogels in de lucht ons wijsheid leert. 12Zo roept men wel, maar Hij antwoordt niet, Om de hoogmoed der bozen. 13Maar als God niet luistert naar ijdel geroep, De Almachtige er geen aandacht aan schenkt, 14Hoeveel te minder, als ge beweert, dat ge Hem niet bespeurt, Dat ge een proces met Hem aangaat, en gij op Hem wacht; 15Of zelfs, dat zijn gramschap niet straft, En dat Hij niet eens de misdaad kent! 16Job opent zijn mond tot ijdel gezwets, Spreekt grote woorden in onverstand.