Elihu Anatangaza Haki Ya Mungu
1Kisha Elihu akasema:
234:2 Ay 32:10“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima;
nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
334:3 Ay 12:11Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno
kama vile ulimi uonjavyo chakula.
434:4 1The 5:21Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa,
nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
534:5 Ay 33:9; 6:29; 27:2; 9; 17“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia,
lakini Mungu ameninyima haki yangu.
634:6 Yer 10:19; Ay 10:3Ingawa niko sawa,
ninaonekana mwongo;
nami ingawa sina kosa,
kidonda changu hakiponi.’
734:7 Ay 9:21; 15:16Ni mtu gani aliye kama Ayubu,
anywaye dharau kama maji?
834:8 Ay 22:15; Za 50:18Ashirikianaye na watenda mabaya
na kuchangamana na watu waovu.
934:9 Ay 9:29-31Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote
anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
1034:10 Mwa 18:25; Za 92:15; Rum 3:5“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu.
Kamwe Mungu hatendi uovu,
Mwenyezi hafanyi kosa.
1134:11 Ay 21:31; 2Kor 5:10; Yer 17:10; Eze 33; 20; Mit 24:12Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda;
huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
1234:12 Za 9:16; Kol 3:25Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa,
kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
1334:13 Ay 36:23; Isa 40:14Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia?
Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
1434:14 Hes 16:22; Za 104:29; Mhu 12:7Kama lilikuwa kusudi la Mungu,
naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
1534:15 Za 90:10; Mwa 2:7wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja,
na mtu angerudi mavumbini.
1634:16 Ay 32:10; 34:30“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili;
sikilizeni hili nisemalo.
1734:17 Mwa 18:23; 2Sam 23:3-4; Mit 20:8; Rum 3:5-7; Ay 10:7Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala?
Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
1834:18 Kut 22:28; Isa 40:24Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’
nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
1934:19 Kum 10:17; Mdo 10:34; Law 19:15; Yak 2:5yeye asiyependelea wakuu,
wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini,
kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
2034:20 Kut 11:4; 12:29; Ay 12:19Wanakufa ghafula, usiku wa manane;
watu wanatikiswa nao hupita;
wenye nguvu huondolewa
bila mkono wa mwanadamu.
2134:21 Mit 15:3; Ebr 4:13“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu;
anaona kila hatua yao.
2234:22 Za 74:20; Ay 3:5; Amo 9:2-3Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa,
ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
2334:23 Ay 11:11; Ezr 9:13Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana,
ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
2434:24 Ay 12:19; Dan 2:21Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi
na kuwaweka wengine mahali pao.
2534:25 Ay 11:11; Mit 5:21-23Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote,
huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
2634:26 Mwa 6:5; Ay 8:22; 28:24; Za 9:5; Yer 44:5Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao
mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
2734:27 Za 14:3; Isa 5:12; 1Sam 15:11kwa sababu wameacha kumfuata Mungu,
nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
2834:28 Kut 22:23; Yak 5:4; Mhu 5:8Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake,
hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
2934:29 Za 28:1; 83:1; 109:1; Rum 8:34; Za 13:1; 97:9; 83:18Lakini kama akinyamaza kimya,
ni nani awezaye kumhukumu?
Kama akiuficha uso wake,
ni nani awezaye kumwona?
Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
3034:30 Za 25:15; Mit 29:2-12; 1Fal 12:28-30ili kumzuia mtu mwovu kutawala,
au wale ambao huwategea watu mitego.
31“Kama mwanadamu akimwambia Mungu,
‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
3234:32 Kut 33:13; Za 27:11; Lk 19:8; Ay 33:27Nifundishe nisichoweza kuona;
kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
3334:33 Mit 17:23; Yn 3:8Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako,
wakati wewe umekataa kutubu?
Yakupasa wewe uamue, wala si mimi;
sasa niambie lile ulijualo.
34“Wanadamu wenye ufahamu husema,
wenye hekima wanaonisikia huniambia,
3534:35 Ay 35:16; 38:2; 42:3; 26:3‘Ayubu huongea bila maarifa;
maneno yake hayana busara.’
3634:36 Ay 6:29; 22:15Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho,
kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37Kwenye dhambi yake huongeza uasi;
kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu,
na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”