Ayubu 31 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 31:1-40

131:1 Kum 5:18; Mt 5:18“Nimefanya agano na macho yangu

yasimtazame msichana kwa kumtamani.

231:2 Ay 16:19; 20:29Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu,

urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?

331:3 Ay 21:30; 34:22; Rum 2:9Je, si uharibifu kwa watu waovu,

maangamizi kwa wale watendao mabaya?

431:4 2Nya 16:9; Mit 5:21; Yer 32:19; Dan 4:37Je, yeye hazioni njia zangu

na kuihesabu kila hatua yangu?

531:5 Ay 15:31; Mik 2:11“Kama nimeishi katika uongo

au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,

631:6 Law 19:36; Ay 6:2Mungu na anipime katika mizani za uaminifu,

naye atajua kwamba sina hatia:

731:7 Ay 9:30; Hes 15:39; Eze 6:9; Mt 5:29; Mhu 11:9kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia,

kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu,

au kama mikono yangu imetiwa unajisi,

831:8 Law 26:16; Yn 4:37; Mik 6:15basi wengine na wale nilichokipanda,

nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.

931:9 Kum 11:16; Yak 1:14“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke,

au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,

1031:10 Kum 28:30; Yer 8:16; Mit 14:31basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine,

nao wanaume wengine walale naye.

1131:11 Law 20:10; Yn 8:4-5Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu,

naam, dhambi ya kuhukumiwa.

1231:12 Ay 15:30; 26:6Ni moto uwakao kwa Uharibifu;31:12 Kwa Kiebrania ni Abadon (Ay 26:6; Mit 15:11).

ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.

1331:13 Kut 21:2-11; Law 25:39-46“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu,

walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,

1431:14 Ay 33:5; Hos 9:7; Za 10:13, 15; Isa 10:3; Yer 5:31nitafanya nini Mungu atakaponikabili?

Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?

1531:15 Ay 10:3; Efe 6:9Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu,

si ndiye aliwaumba?

Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote

ndani ya mama zetu?

1631:16 Law 25:17; Ay 20:19; Yak 1:27“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao,

au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,

1731:17 Ay 6:27; 29:12kama nimekula chakula changu mwenyewe,

bila kuwashirikisha yatima;

1831:18 Isa 51:18lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya,

nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:

1931:19 Ay 22:6; 24:4; Isa 58:7kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo,

au mtu mhitaji asiye na mavazi

2031:20 Ay 29:13; Amu 6:37ambaye wala moyo wake haukunibariki

kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,

2131:21 Ay 22:7-9; Yak 1:27na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima,

nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,

2231:22 Hes 15:30; Za 10:15basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu,

nao na uvunjike kutoka kiungio chake.

2331:23 Ay 10:3; 13:11; Mwa 20:11Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu,

nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.

2431:24 Ay 22:25; Mk 10:24; Lk 12:15“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu,

au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’

2531:25 Mwa 12:16; Isa 10:14kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu,

ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,

2631:26 Hes 11:20; Kum 4:19; Eze 8:16kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake

au mwezi ukienda kwa fahari yake,

2731:27 Ay 24:15; Yak 1:14; Yer 8:2; 16:11hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri,

au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,

2831:28 Mwa 38:24; Kum 17:2-7; Yos 24:23-27; Mit 30:9basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa,

kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.

2931:29 Za 35:15; Mt 5:44; Mit 17:5; 24:17-18“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu,

au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,

30lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi

kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;

31kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema,

‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’

3231:32 Amu 19:20; Mt 25:35; Ebr 13:2; 1Pet 4:9Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani,

kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;

3331:33 Za 32:5; Mit 28:13; Mwa 3:8kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo,

kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,

3431:34 Kut 23:2; Mit 29:25kwa sababu ya kuogopa umati wa watu,

na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa,

nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:

35(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia!

Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu:

Mwenyezi na anijibu;

mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.

36Hakika ningeyavaa begani mwangu,

ningeyavaa kama taji.

3731:37 Ay 1:3; 21:28Ningempa hesabu ya kila hatua yangu,

ningemwendea kama mwana wa mfalme.)

3831:38 Mwa 4:10“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu,

na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,

3931:39 1Fal 21:19; Law 19:13; Yak 5:4kama nimekula mazao yake bila malipo,

au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,

4031:40 Mwa 3:18; Mit 13:7basi miiba na iote badala ya ngano,

na magugu badala ya shayiri.”

Mwisho wa maneno ya Ayubu.

Japanese Contemporary Bible

ヨブ 記 31:1-40

31

1情欲をもって女性を見ないようにする。

私は、そう自分の目と契約を結んだ。

2-3みだらな者に、全能の神が

災いを下すことを知っているからだ。

4神は私のなすことすべてを見ている。

5私がうそをつき、人を欺いたことがあるだろうか。

6もちろん、神は私の潔白をご存じだ。

7-8私は、神の道を踏みはずしたことも、

目に入るものへの欲望に取りつかれたこともない。

そのほかの罪についても、全く身に覚えがない。

もし少しでもやましいところがあったら、

私が種をまいて育てた作物をほかの者が刈り取り、

私の植えた木がみな根こそぎにされてもいい。

9私が人の妻を欲しがったことがあるというなら、

10殺されてもいい。

私の妻が他の人の家に労働者として入り、

あるいは他の人が彼女の夫になってもいい。

11情欲は恥ずべき罪、罰せられるべき罪過、

12何もかも焼き尽くす地獄の火だ。

それは、私の植えたものをみな根こそぎにする。

13少しでも召使たちを

不当にあしらったことがあったなら、

14神をまともに見ることなどできるわけがない。

神にそのことを問いただされたら、

何も答えようがない。

15神は私を造り、また召使たちをも造ったからだ。

16私が貧しい人を傷つけ、

未亡人を泣かせたことがあるだろうか。

17腹をすかせた孤児に、

食べ物を恵まなかったことがあるだろうか。

18いつも、孤児を引き取って親身に世話をし、

わが子同様に育てたではないか。

19-20寒さにこごえている者に着る物を与えず、

その人を暖めるために羊の毛を刈らなかったことが

あるだろうか。

21だれにも責められないからといって、

孤児の弱みにつけこんだことがあるだろうか。

22こんなことを一つでもしていたら、

腕がつけ根からもぎ取られ、

肩の骨がはずれてもかまわない。

23その程度の罰なら、

どんなものより恐ろしい神にさばかれるよりましだ。

威厳ある神を向こうに回したら、

一片の望みもなくなってしまうからだ。

24私が金銭を頼りにしたことがあるだろうか。

25財産のあるなしを

幸福の尺度にしたことがあるだろうか。

26あるいは、空に輝く太陽を見、

銀の道に沿って動く月を見て、

27心ひそかに魅せられ、

手を合わせて拝んだことがあるだろうか。

28こんな行為も、裁判にかけて罰せられるべきだ。

私がこんなことをしたのなら、

天の神を否定したことになるからだ。

29私は、敵が苦しむのを見て喜んだことがあるだろうか。

30人をのろったり、復讐したりしたことなど一度もない。

31召使を飢えさせたこともない。

32見知らぬ人でも追い返したりせず、

だれが来ても気持ちよく迎え入れた。

33私は、アダムのように罪を隠したことがあるだろうか。

34群衆におびえ、軽蔑されることを恐れて、

罪を認めようとせず、

人の力になることをためらったことがあるだろうか。

35私の言い分を聞き、

私の立場を理解してくれる者はいないのか。

だれが何と言おうと、私は正しい。

もし間違っていたら、全能者がそれを指摘すればよい。

敵の起訴状が正当であることを、全能者が認めればよい。

36私はそれを、冠のように大事にしまっておく。

37それから、自分が何をしたかを、

包み隠さず神に打ち明け、

堂々と自分の立場を弁護したい。

38-39もし私の土地が、

そこの産物を盗んだとして私を責めるなら、

あるいは、私が小作人を殺して、

彼らの収穫を奪い取ったことがあるというなら、

40小麦の代わりにいばらが生え、

大麦の代わりに雑草がはびこるように。」

ここでヨブのことばは 終わりました。