Ayubu 29 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 29:1-25

Ayubu Anamaliza Utetezi Wake

129:1 Za 18:28; Ay 13:12Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:

229:2 Yer 1:12; 44:27“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita,

zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,

329:3 Ay 11:17; 12:25wakati taa yake iliniangazia kichwani changu,

na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!

429:4 Za 25:14; Mit 3:32Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu,

wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,

529:5 Za 127:3-5; 128:3; Rum 4:1wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami,

nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,

629:6 Ay 20:17; Za 81:16; Mwa 49:20; Kum 32:13wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi,

nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.

729:7 Ay 5:4; 31:21; Yer 20:2; 38:7“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji

na kuketi katika kiwanja,

829:8 1Tim 5:1; Law 19:32vijana waliniona wakakaa kando,

nao wazee walioketi wakasimama;

929:9 Amu 16:19; Mit 30:32wakuu wakaacha kuzungumza

na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;

1029:10 Za 137:6wenye vyeo wakanyamazishwa,

nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.

1129:11 Ay 4:4; Ebr 11:4Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu,

nao walioniona walinisifu,

1229:12 Kum 24:17; Ay 31:17-21; Za 72:12; Mit 21:13kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada,

naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.

1329:13 Ay 31:20; 22:9; Kum 10:18Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki,

nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.

1429:14 2Sam 8:15; Rum 13:14; Efe 6:14Niliivaa haki kama vazi langu;

uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.

1529:15 Hes 10:31Nilikuwa macho ya kipofu

na miguu kwa kiwete.

1629:16 Ay 24:4; Mit 29:7Nilikuwa baba kwa mhitaji;

nilimtetea mgeni.

1729:17 Ay 24:9; 4:10, 11; Za 3:7Niliyavunja meno makali ya waovu,

na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.

1829:18 Za 62:2; Mit 3:1-2“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe,

nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.

1929:19 Hes 24:6; Yer 17:8Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji,

nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.

2029:20 Za 18:34; Isa 38:12; Mwa 49:24Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu,

upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’

2129:21 Ay 29:21“Watu walinisikiliza kwa tumaini,

wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.

2229:22 Kum 32:2Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi;

maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.

23Waliningojea kama manyunyu ya mvua

na kuyapokea maneno yangu

kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.

24Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha;

nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.

2529:25 Ay 31:31; 4:4Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao;

niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake;

nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.