Ayubu 28 – NEN & NASV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 28:1-28

Mapumziko: Imani Inakopatikana

128:1 Za 12:6; 66:10; Yer 9:7; Mal 3:3; Dan 11:35“Kuna machimbo ya fedha,

na mahali dhahabu isafishwapo.

228:2 Kum 8:9Chuma hupatikana ardhini,

nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.

328:3 Mhu 7:25; 8:17; Mit 2:4Mwanadamu hukomesha giza;

huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali,

kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini

katika giza jeusi sana.

428:4 2Sam 5:8Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu,

mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu;

mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.

528:5 Mwa 1:29; Za 145:15Ardhi, ambako chakula hutoka,

chini hugeuzwa kwa moto;

628:6 Isa 54:11; Wim 5:14; Ay 22:24yakuti samawi hutoka katika miamba yake,

nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.

728:7 Ay 28:21Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika,

wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.

828:8 Ay 41:34; Isa 35:9Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga,

wala simba azungukaye huko.

928:9 Kum 8:15; Yn 2:6Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana,

na kuiacha wazi mizizi ya milima.

1028:10 Mit 2:4; Ay 28:4Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba;

macho yake huona hazina zake zote.

1128:11 Mwa 7:11; Isa 48:6; Yer 33:3Hutafuta vyanzo vya mito

na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.

1228:12 Mit 1:20; Mhu 7:24“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi?

Ufahamu unakaa wapi?

1328:13 Mit 3:15; Mt 13:44-46Mwanadamu hatambui thamani yake;

haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.

14Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’;

bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’

1528:15 Mit 16:16; Mdo 8:20Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote,

wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.

16Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri,

kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.

1728:17 Za 119:72; Mit 8:10; Ay 28:15Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo,

wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.

18Marijani na yaspi hazistahili kutajwa;

thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.

1928:19 Mit 3:14-15; 8:10-19Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,

wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.

20“Ni wapi basi hekima itokako?

Ufahamu hukaa wapi?

2128:21 Ay 28:7Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai,

imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.

2228:22 Ay 26:6Uharibifu na Mauti husema,

‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’

2328:23 Mdo 15:18; Ay 22:22; Mit 8:22-31Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima

na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,

2428:24 Isa 11:12; Yos 3:11; Ebr 4:13; Za 66:7kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia

na huona kila kitu chini ya mbingu.

2528:25 Ay 38:8-11; Za 135:7Alipofanyiza nguvu za upepo

na kuyapima maji,

2628:26 Ay 38:25-27; Isa 35:7; Yer 14:22alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua

na njia kwa ajili ya umeme wa radi,

27ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake,

akaithibitisha na kuihakikisha.

2828:28 Kut 20:20; Kum 4:6Naye Mungu akamwambia mwanadamu,

‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima,

nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’ ”

New Amharic Standard Version

ኢዮብ 28:1-28

1“የብር ማዕድን የሚወጣበት፣

ወርቅም የሚነጠርበት ስፍራ አለ።

2ብረት ከመሬት ውስጥ ይገኛል፤

መዳብም ከማዕድን ድንጋይ ቀልጦ ይወጣል።

3ሰው፣ እስከ ጨለማ መጨረሻ ይዘልቃል፤

ከድቅድቅ ጨለማ የማዕድን ድንጋይ ለማግኘት፣

እስከ ውስጠኛው ዋሻ ገብቶ ይፈልጋል።

4የሰው እግር ረግጦት በማያውቅበት ስፍራ፣

ከሰዎች መኖሪያ ርቆ መውረጃ ጕድጓድ ይቈፍራል፤

ሰው በሌለበት ቦታ ይንጠላጠላል፤ ይወዛወዛል።

5ከላይዋ ምግብን የምታስገኝ ምድር፣

ከታች በእሳት እንደሚሆን ትለዋወጣለች።

6ሰንፔር28፥6 በዚህና በ16 ላይ፣ ላፒስ ላዙሊ ከዐለቷ ይወጣል፤

ከዐፈሯም የወርቅ አንኳር ይገኛል።

7ያን መንገድ ጭልፊት አያውቀውም፤

የአሞራም ዐይን አላየውም፣

8ኵሩ አራዊት አልረገጡትም፤

አንበሳም በዚያ አላለፈም።

9ሰው እጁን በቡላድ ድንጋይ ላይ ያነሣል፤

ተራሮችንም ከሥር ይገለብጣል።

10በድንጋይ ውስጥ መተላለፊያ ያበጃል፤

ዐይኖቹም የከበሩ ነገሮችን ሁሉ ያያሉ።

11የወንዞችን ምንጭ ይበረብራል፤28፥11 የሰብዓ ሊቃናት ትርጕምና ቩልጌት ከዚህ ጋር ይስማማል፤ ዕብራይስጡ ግን ይገድባል ይላል።

የተሰወረውንም ነገር ወደ ብርሃን ያወጣል።

12“ነገር ግን ጥበብ ከወዴት ትገኛለች?

ማስተዋልስ መኖሪያዋ የት ነው?

13ሰው ዋጋዋን አያውቅም፤

በሕያዋንም ምድር አትገኝም።

14ውቅያኖስ፣ ‘በእኔ ውስጥ የለችም’ ይላል፤

ባሕርም፣ ‘በእኔ ዘንድ አይደለችም’ ይላል።

15ንጹሕ ወርቅ ሊገዛት አይችልም፤

ዋጋዋም በብር አይመዘንም።

16በኦፊር ወርቅ፣

በከበረም መረግድና በሰንፔር አትገመትም።

17ወርቅም ብርሌም አይወዳደሯትም፤

በወርቅ ጌጥም አትለወጥም።

18ዛጐልና አልማዝ ከቍጥር አይገቡም፤

የጥበብ ዋጋ ከቀይ ዕንቍም ይበልጣል።

19የኢትዮጵያ ቶጳዝዮን ሊስተካከላት አይችልም፤

ዋጋዋም በንጹሕ ወርቅ አይተመንም።

20“ታዲያ፣ ጥበብ ከወዴት ትመጣለች?

ማስተዋልስ የት ትገኛለች?

21ከሕያዋን ፍጥረታት ዐይን ሁሉ ተሰውራለች፤

ከሰማይ ወፎችም ተሸሽጋለች።

22ጥፋትና28፥22 ዕብራይስጡ፣ አባዶን ይላል። ሞት፣

‘ወሬዋን ብቻ ሰማን’ ይላሉ።

23ወደ እርሷ የሚወስደውን መንገድ የሚረዳ፣

መኖሪያዋንም የሚያውቅ እግዚአብሔር ብቻ ነው፤

24እርሱ የምድርን ዳርቻ ይመለከታልና፤

ከሰማይ በታች ያለውንም ሁሉ ያያል።

25ለነፋስ ኀይልን በሰጠ ጊዜ፣

የውሆችን መጠን በለካ ጊዜ፣

26ለዝናብ ሥርዐትን፣

ለነጐድጓድም መንገድን ባበጀ ጊዜ፣

27በዚያን ጊዜ ጥበብን ተመለከታት፤ ገመገማትም፤

አጸናት፤ መረመራትም።

28ከዚያም ሰውን፣

‘እግዚአብሔርን መፍራት ጥበብ ነው፤

ከክፋትም መራቅ ማስተዋል ነው’ አለው።”