Hotuba Ya Mwisho Ya Ayubu
Ayubu Anadumisha Uadilifu Wake
127:1 Ay 29:1Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
227:2 Ay 9:18; 34:5; Isa 45:9; 1Sam 1:10“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu,
Mwenyezi ambaye amenifanya
nionje uchungu wa nafsi,
327:3 Mwa 2:7; Za 144:4kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu,
nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
427:4 Ay 6:28; 12:16; 16:17midomo yangu haitanena uovu,
wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
527:5 Ay 2:9; 10:7; 32:2Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi;
hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
627:6 Ay 29:14; Za 119:121; Isa 59:17; 61:10; Rum 2:15Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha;
dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
7“Watesi wangu wawe kama waovu,
nao adui zangu wawe kama wasio haki!
827:8 Ay 8:13; Hes 16:22; Lk 12:20; Mt 16:26Kwa maana mtu asiyemcha Mungu
analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali,
Mungu anapouondoa uhai wake?
927:9 Zek 7:13; Mik 3:4; 1Sam 8:18Je, Mungu husikiliza kilio chake,
shida zimjiapo?
1027:10 Ay 22:26Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi?
Je, atamwita Mungu nyakati zote?
1127:11 Ay 36:23; 27:13“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu;
njia za Mwenyezi sitazificha.
12Ninyi nyote mmeona hili wenyewe.
Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
1327:13 Ay 15:20; 16:19“Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu,
urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi:
1427:14 Mao 2:22; Es 9:10; Hos 9:13; Ay 20:10; 2Fal 10:6-10Hata kama watoto wake watakuwa wengi kiasi gani,
fungu lao ni kuuawa kwa upanga;
wazao wake hawatakuwa kamwe
na chakula cha kuwatosha.
1527:15 Za 78:64Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao,
nao wajane wao hawatawaombolezea.
1627:16 Zek 9:3Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi,
na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi,
1727:17 Mit 13:22; Mhu 2:26yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa,
naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake.
1827:18 Ay 8:14; Isa 1:8; 24:20; Mao 2:6Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui,
kama kibanda alichotengeneza mlinzi.
1927:19 Ay 3:13; Hes 20:26Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho;
afunguapo macho yake, yote yametoweka.
2027:20 Ay 15:21; 20:8Vitisho humjia kama mafuriko;
dhoruba humkumba ghafula usiku.
2127:21 Ay 38:24; Yer 13:24; Ay 30:22; 7:10; Yer 22:22Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka;
humzoa kutoka mahali pake.
2227:22 Yer 13:14; Eze 5:11; Ay 11:20Humvurumisha bila huruma,
huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.
2327:23 Ay 7:10; 18:18Upepo humpigia makofi kwa dharau,
na kumfukuza atoke mahali pake.