Bildadi Anasema: Mwanadamu Awezaje Kuwa Mwadilifu Mbele Za Mungu?
125:1 Ay 8:1Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:
225:2 Zek 9:2; Ufu 1:6“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
325:3 Mt 5:45; Yak 1:17; Mwa 1:14-16Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
425:4 Ay 4:17; 14:4; Rum 3:19-20Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
525:5 Ay 31:26; 4:18Ikiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
625:6 Za 22:6; 80:17; Eze 2:1; Ay 7:5sembuse mtu ambaye ni funza:
mwanadamu ambaye ni buu tu!”