Ayubu 23 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 23:1-17

Hotuba Ya Nane Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Kulalamika Kwangu Ni Uchungu

1Ndipo Ayubu akajibu:

223:2 Ay 6:3; 7:11; 1Sam 1:10“Hata leo malalamiko yangu ni chungu;

mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.

323:3 Kum 4:29Laiti ningefahamu mahali pa kumwona;

laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!

423:4 Ay 13:18; 9:15Ningeliweka shauri langu mbele zake,

na kukijaza kinywa changu na hoja.

5Ningejua kwamba angenijibu nini,

na kuelewa lile ambalo angelisema.

623:6 Ay 9:4, 19; Isa 27:4Je, angenipinga kwa nguvu nyingi?

La, asingenigandamiza.

723:7 Mwa 3:8; Ay 9:3Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake,

nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.

8“Lakini nikienda mashariki, hayupo;

nikienda magharibi, simpati.

923:9 Ay 9:11Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni;

akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.

1023:10 Za 66:10; 139:1-3; 12:6; 1Pet 1:7; Yak 1:12Lakini anaijua njia niiendeayo;

akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

1123:11 Za 17:5; Ay 31:7; Yer 11:20; Za 44:18; 125:5Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu;

nimeishika njia yake bila kukengeuka.

1223:12 Ay 6:10; 15:11; Yn 4:32, 34; Mt 4:4Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake;

nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.

1323:13 Za 115:3; Isa 55:11; Mhu 3:14; Rum 9:19“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga?

Yeye hufanya lolote atakalo.

1423:14 1The 3:3; 1Pet 4:12Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu,

na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.

1523:15 Mwa 45:3; Yos 24:14; Mhu 3:14; 12:13; 2Kor 5:11Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake;

nifikiriapo haya yote ninamwogopa.

1623:16 Za 22:14; Yer 51:46; Ay 27:223:16 Kum 20:3; Ay 27:2; Kut 3:6; Ufu 6:16Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia;

yeye Mwenyezi amenitia hofu.

1723:17 Ay 3:6; 6:9; 19:8Hata hivyo sijanyamazishwa na giza,

wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.