Ayubu 21 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 21:1-34

Hotuba Ya Saba Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Waovu Mara Nyingi Huenda Bila Kuadhibiwa

1Ndipo Ayubu akajibu:

221:2 Ay 13:17; 21:34“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini;

hii na iwe faraja mnayonipa mimi.

321:3 Ay 6:14; 11:3; 16:10Nivumilieni ninapozungumza,

nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.

421:4 Za 22:1-3; Ay 6:3, 11; 1Sam 1:16“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu?

Kwa nini nisikose subira?

521:5 Amu 18:19; Ay 40:4Niangalieni mkastaajabu;

mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.

621:6 Mwa 45:3; Ay 4:14Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa,

nao mwili wangu unatetemeka.

721:7 Mhu 7:15; Mal 3:15; Yer 12:1-3Kwa nini waovu wanaendelea kuishi,

wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?

821:8 Za 17:14; Mal 3:15Huwaona watoto wao wakithibitika

wakiwa wamewazunguka,

wazao wao mbele za macho yao.

921:9 Ay 5:24; Za 73:5Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu;

fimbo ya Mungu haiko juu yao.

1021:10 Kut 23:26Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe;

ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.

1121:11 Za 78:52; 107:41Huwatoa watoto wao nje kama kundi;

wadogo wao huchezacheza.

1221:12 1Nya 15:16; Mt 15:17Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi,

nao huifurahia sauti ya filimbi.

1321:13 Ay 24:19; Za 49:14; Isa 14:15; Ay 3:13Huitumia miaka yao katika mafanikio

nao hushuka kaburini kwa amani.

1421:14 Ay 4:17; Kum 32:15; Isa 30:11; 1Sam 11:15Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’

Hatuna haja ya kufahamu njia zako.

1521:15 Yer 9:6; Mal 3:14Mwenyezi ni nani hata tumtumikie?

Tutapata faida gani kumwomba?

1621:16 Ay 22:18; Za 1:1; 26:5; 36:1Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe,

hivyo najitenga mbali na shauri la waovu.

1721:17 Ay 18:5; 18:12; 20:22, 28“Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?

Ni mara ngapi maafa huwajia,

yale yawapatayo ambayo Mungu

huwapangia katika hasira yake?

1821:18 Ay 13:15; Mwa 19:15; Ay 7:10; Mit 10:25; Mwa 7:23Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo,

kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?

1921:19 Kut 20:5; Yn 9:2Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu

kwa ajili ya wanawe.’

Mungu na amlipe mtu mwenyewe,

ili apate kulijua!

2021:20 Ay 6:4; Isa 51:17; Yer 25:15; Ufu 14:10Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake;

yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi.

2121:21 Ay 14:22; 14:5; 14:21; Mhu 9:5-6Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma,

miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho?

2221:22 Za 94:12; 86:8; Rum 11:34“Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa,

iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote?

2321:23 Mwa 15:15; Ay 13:26; 3:13Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili,

akiwa salama na mwenye raha kamili,

2421:24 Mit 3:8mwili wake ukiwa umenawiri,

nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.

2521:25 Ay 10:1Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi,

akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.

2621:26 Mhu 9:2-3; Isa 14:11Hao wote hulala mavumbini,

nao mabuu huwafunika wote.

27“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri,

mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.

2821:28 Ay 1:3; 12:21; 29:25; 31:37; 8:22Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu,

mahema ambayo watu waovu walikaa?’

29Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri?

Je, hamkutafakari taarifa zao:

3021:30 Ay 31:3; Mit 16:4; Isa 5:30; Rum 5:2kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa,

kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?

3121:31 Ay 34:11; Za 62:12; Mit 24:11-12; Isa 59:18Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake?

Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?

3221:32 Isa 14:18Hupelekwa kaburini,

nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.

3321:33 Ay 3:17-19; 17:16; 24:24Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake;

watu wote watamfuata,

nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.

34“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu?

Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”