Ayubu 18 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 18:1-21

Bildadi Anasema: Mungu Huwaadhibu Waovu

118:1 Ay 8:1Bildadi Mshuhi akajibu:

218:2 Ay 8:2; 16:3“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya?

Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.

318:3 Za 73:22; Ay 12:7Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama,

na kuonekana wajinga machoni pako?

418:4 Ay 13:14; 16:9; 14:18Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande

katika hasira yako,

je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe?

Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?

518:5 Yer 25:10; Yn 8:12; Mit 13:9“Taa ya mwovu imezimwa,

nao mwali wa moto wake umezimika.

618:6 Ay 8:22; 5:14; 11:17; 12:25Mwanga hemani mwake umekuwa giza;

taa iliyo karibu naye imezimika.

718:7 Za 18:36; Mit 4:12; Ay 5:13; 15:6Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa;

shauri lake baya litamwangusha.

818:8 Mik 7:2; Hab 1:15Miguu yake imemsukumia kwenye wavu,

naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.

918:9 Ay 22:10; 30:12; Isa 24:18; Yer 48:44; Amo 5:14; Mit 7:22Tanzi litamkamata kwenye kisigino;

mtego utamshikilia kwa nguvu.

1018:10 Mit 7:22; Isa 51:20; 1Sam 28:9; Za 140:5Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;

mtego uko kwenye njia yake.

1118:11 Ay 15:21; 20:8; Za 31:13; Isa 22:18; Yer 6:25Vitisho vimemtia hofu kila upande,

na adui zake humwandama kila hatua.

1218:12 Isa 9:20; 65:13; 8:21; Ay 21:17; 31:3; 15:25Janga linamwonea shauku;

maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.

1318:13 Zek 14:12; Hes 12:12Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake;

mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.

1418:14 Ay 8:22; 15:24; 18:11Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake,

na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.

1518:15 Mwa 19:24; Za 11:6; Ay 18:18; 20:26Moto utakaa katika hema lake;

moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.

1618:16 Hos 5:12; Amo 2:9; Mwa 27:28Mizizi yake chini itakauka

na matawi yake juu yatanyauka.

1718:17 Mit 2:22; 10:7; Isa 49:15; Kum 32:26; 9:14; Za 9:5; 69:28Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia,

wala hatakuwa na jina katika nchi.

1818:18 Ay 5:14; 18:11; 11:20; 30:8Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani,

naye amefukuzwa mbali atoke duniani.

1918:19 Za 37:28; 21:10; Isa 14:22; Ay 27:14-15Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake,

wala aliyenusurika mahali alipoishi.

2018:20 Yer 46:21; Eze 7:7Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata;

watu wa mashariki watapatwa na hofu.

2118:21 Ay 21:28; Yer 9:3; 1The 4:5Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu;

ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

New Arabic Version

أيوب 18:1-21

بلدد

1فَقَالَ بِلْدَدُ الشُّوحِيُّ: 2«مَتَى تَكُفُّ عَنْ تَرْدِيدِ هَذِهِ الْكَلِمَاتِ؟ تَعَقَّلْ ثُمَّ نَتَكَلَّمُ. 3لِمَاذَا تَعْتَبِرُنَا كَالْبَهِيمَةِ وَحَمْقَى فِي عَيْنَيْكَ؟ 4يَا مَنْ تُمَزِّقُ نَفْسَكَ إِرْباً غَيْظاً، هَلْ تُهْجَرُ الأَرْضُ مِنْ أَجْلِكَ أَمْ تَتَزَحْزَحُ الصَّخْرَةُ مِنْ مَوْضِعِهَا؟

5أَجَلْ! إِنَّ نُورَ الأَشْرَارِ يَنْطَفِئُ وَلَهِيبَ نَارِهِمْ لَا يُضِيءُ. 6يَتَحَوَّلُ النُّورُ إِلَى ظُلْمَةٍ فِي خَيْمَتِهِ، وَيَنْطَفِئُ سِرَاجُهُ عَلَيْهِ. 7تَقْصُرُ خَطْوَاتُهُ الْقَوِيَّةُ وَتَصْرَعُهُ تَدْبِيرَاتُهُ، 8لأَنَّ قَدَمَيْهِ تُوْقِعَانِهِ فِي الشَّرَكِ وَتَطْرَحَانِهِ فِي حُفْرَةٍ، 9يَقْبِضُ الْفَخُّ عَلَى عَقِبَيْهِ وَالشَّرَكُ يَشُدُّ عَلَيْهِ، 10حِبَالَتُهُ مَطْمُورَةٌ فِي الطَّرِيقِ، وَالْمِصْيَدَةُ كَامِنَةٌ فِي سَبِيلِهِ، 11تُرْعِبُهُ أَهْوَالٌ مِنْ حَوْلِهِ وَتُزَاحِمُهُ عِنْدَ رِجْلَيْهِ، 12قُوَّتُهُ يَلْتَهِمُهَا الْجُوعُ النَّهِمُ، وَالْكَوَارِثُ مُتَأَهِّبَةٌ تَتَرَصَّدُ كَبْوَتَهُ. 13يَفْتَرِسُ الدَّاءُ جِلْدَهُ وَيَلْتَهِمُ الْمَرَضُ الأَكَّالُ أَعْضَاءَهُ. 14يُؤْخَذُ مِنْ خَيْمَتِهِ رُكْنِ اعْتِمَادِهِ، وَيُسَاقُ أَمَامَ مَلِكِ الأَهْوَالِ. 15يُقِيمُ فِي خَيْمَتِهِ غَرِيبٌ وَيُذَرُّ كِبْرِيتٌ عَلَى مَرْبِضِهِ. 16تَجِفُّ أُصُولُهُ تَحْتَهُ، وَتَتَبَعْثَرُ فُرُوعُهُ مِنْ فَوْقِهِ. 17يَبِيدُ ذِكْرُهُ مِنَ الأَرْضِ، وَلا يَبْقَى لَهُ اسْمٌ فِيهَا. 18يُطْرَدُ مِنَ النُّورِ إِلَى الظُّلْمَةِ، وَيُنْفَى مِنَ الْمَسْكُونَةِ. 19لَا يَكُونُ لَهُ نَسْلٌ، وَلا عَقِبٌ بَيْنَ شَعْبِهِ، وَلا حَيٌّ فِي أَمَاكِنِ سُكْنَاهُ. 20يَرْتَعِبُ مِنْ مَصِيرِهِ أَهْلُ الْغَرْبِ، وَيَسْتَوْلِي الْفَزَعُ عَلَى أَبْنَاءِ الشَّرْقِ. 21حَقّاً تِلْكَ هِيَ مَسَاكِنُ الأَشْرَارِ، وَهَذَا هُوَ مَقَامُ مَنْ لَا يَعْرِفُ اللهَ!»