Ayubu 17 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 17:1-16

117:1 Za 88:3-4; Mhu 12:1-7Moyo wangu umevunjika,

siku zangu zimefupishwa,

kaburi linaningojea.

217:2 1Sam 1:6-7; Ay 11:3Hakika wenye mizaha wamenizunguka;

macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.

Ayubu Anaomba Msaada

317:3 Za 35:27; 40:17; Mit 6:1; Isa 38:14“Ee Mungu, nipe dhamana unayodai.

Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?

417:4 Ay 12:12Umezifunga akili zao zisipate ufahamu,

kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.

517:5 Kut 22:15; Ay 11:20Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira,

macho ya watoto wake yatashindwa kuona.

617:6 1Fal 9:7; Yer 15:4“Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu,

mtu ambaye watu humtemea mate usoni.

717:7 Ay 16:8; 2:12; 16:16Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi;

umbile langu lote ni kama kivuli.

817:8 Kut 4:14; Ay 22:19Watu wanyofu wanatishwa na hili;

watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu.

917:9 Mit 4:18; 2Sam 22:21; Ay 22:30Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao,

nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu.

1017:10 Ay 12:3“Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena!

Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu.

1117:11 Ay 17:15; Isa 38:10; Ay 7:6Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika,

vivyo hivyo shauku za moyo wangu.

1217:12 Isa 50:11; Ay 5:17-26; 11:17Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana,

kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’

1317:13 2Sam 14:14; Ay 3:13; Za 139:8; 88:18Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi,17:13 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

kama nikikitandika kitanda changu gizani,

1417:14 Ay 13:28; 30:28, 30; 4:19; 7:5; Za 16:10; 49:9; 17:15; Ay 7:6; Za 31:23; Mao 3:18; Eze 37:11kama nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’

na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’

15liko wapi basi tarajio langu?

Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu?

1617:16 Mwa 2:7; Yon 2:6; Ay 3:17Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti?17:16 Malango ya mauti hapa ina maana ya Kuzimu.

Je, tutashuka pamoja mavumbini?”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

约伯记 17:1-16

1“我的心灵破碎,我的年日将尽,

坟墓等候着我。

2无疑,嘲笑的人围着我,

我眼睁睁地看着他们挑衅。

3上帝啊,求你为我作保。

除你以外,谁肯做我的保人?

4你蒙蔽了他们的心智,

因此你必不让他们得胜。

5人为了分产业而控告朋友,

其子孙的眼睛要失明。

6上帝使我成了人们的笑柄,

他们在我脸上吐唾沫。

7哀伤使我眼目昏花,

我整个人骨瘦如柴。

8这使正直的人震惊,

使无辜的人起来讨伐不敬虔的人。

9义人坚守自己的道,

手洁的人更有力量。

10来吧,你们众人再来,

我在你们中间不会找到一个智者。

11我的年日已尽,

我的计划破灭,

我的心愿落空。

12他们以黑夜为白昼,

说光明与黑暗相似。

13我若期望阴间作我的家园,

在黑暗之地铺设我的床榻,

14称坟墓为父亲,

称蛆虫为母亲、姊妹,

15那么,我的希望在哪里?

谁能看到我的希望?

16我的希望会跟我下到阴间,

与我同归尘土吗?”