Elifazi Anaongea: Ayubu Anadhoofisha Imani
115:1 Ay 4:1Kisha Elifazi Mtemani akajibu:
215:2 Mwa 41:6; Ay 6:26“Je, mtu mwenye hekima hujibu kwa mawazo matupu,
au kujaza tumbo lake kwa upepo wenye joto wa mashariki?
315:3 Neh 4:2-3; Ay 6:26Je, aweza kubishana juu ya maneno yasiyofaa,
kwa hotuba zisizo na maana?
415:4 Ay 25:6Lakini unadhoofisha hata uchaji wa Mungu
na kuzuia ibada mbele za Mungu.
515:5 Ay 11:6; 22:5; 5:13; Mt 16:23Dhambi yako inasukuma kinywa chako,
nawe umechagua ulimi wa hila.
615:6 Za 10:2; Mt 12:37; Lk 19:22; Ay 7:15; 18:7Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala si changu;
midomo yako mwenyewe inashuhudia dhidi yako.
715:7 Ay 38:21; 1Sam 2:8; Mit 8:25; Za 90:2“Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa?
Ulizaliwa kabla ya vilima?
815:8 Yer 23:18; 1Kor 2:11Je, wewe husikiliza mashauri ya siri ya Mungu?
Je, wewe unaizuia hekima iwe yako mwenyewe?
915:9 Ay 12:3Wewe unajua kitu gani tusichokijua sisi?
Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?
1015:10 Ay 12:12; 32:6-7; 8:8-10Wale wenye mvi na wazee wako upande wetu,
watu ambao ni wazee hata kuliko baba yako.
1115:11 Mwa 37:35; 2Kor 1:3-4; Kum 8:3; Yer 15:16Je, faraja za Mungu hazikutoshi,
au maneno yaliyosemwa kwako kwa upole si kitu?
1215:12 Ay 11:13; 36:13Kwa nini moyo wako unakudanganya,
na kwa nini macho yako yanangʼaa,
1315:13 Mit 29:11; Dan 11:30; Za 94:4; Ay 11:8; 22:5; 30:2ili kwamba upate kutoa hasira yako dhidi ya Mungu,
na kumwaga maneno kama hayo kutoka kinywani mwako?
1415:14 Ay 14:1; 4:17; 2Nya 6:36; Mhu 7:18, 20“Mwanadamu ni kitu gani, hata aweze kuwa safi,
au yeye aliyezaliwa na mwanamke, hata aweze kuwa mwadilifu?
1515:15 Ay 5:1; 4:18Kama Mungu hawaamini watakatifu wake,
kama hata mbingu zenyewe si safi machoni pake,
1615:16 Law 5:2; Ay 12:4; 20:12; Mit 19:28; Za 14:1sembuse mwanadamu ambaye ni mwovu na mpotovu,
ambaye hunywa uovu kama anywavyo maji!
1715:17 Ay 4:8“Nisikilize mimi nami nitakueleza,
acha nikuambie yale niliyoyaona,
1815:18 Kum 32:7; Ay 8:8; Mwa 18:19ambayo watu wenye hekima wameyanena,
bila kuficha lolote walilopokea toka kwa baba zao
1915:19 Mwa 12:1; Ay 22:8(wakati ambao wao peke yao ndio walipewa nchi,
hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao):
2015:20 Oba 1:15; Sef 1:17Mtu mwovu siku zake zote hupata mateso,
miaka yote aliwekewa mkorofi.
2115:21 1Sam 3:11; Yer 6:25; Isa 13:3; 1The 5:3Sauti za kutisha hujaa masikioni mwake;
katika kufanikiwa kwake, wanyangʼanyi humshambulia.
2215:22 Hos 9:13; Amo 5:19Hukata tamaa kuokoka gizani;
amewekwa kwa ajili ya upanga.
2315:23 Za 59:15; 109:10; Ay 18:12Hutangatanga, akitafuta chakula;
anajua kwamba siku ya giza iko karibu.
2415:24 Isa 8:22; 9:1; Ay 15:20; 18:14Taabu na maumivu makuu vinamtia hofu;
humshinda kama mfalme aliye tayari kwa vita,
2515:25 Za 2:2-3; Mit 21:30kwa sababu amemkunjia Mungu ngumi yake
na kujigamba dhidi ya Mwenyezi,
2615:26 Yer 44:16kwa kiburi akishambulia dhidi ya Mungu
akiwa na ngao nene, iliyo imara.
2715:27 Amu 3:17; Za 17:10“Ingawa uso wake umefunikwa na mafuta kwa unene
na kiuno chake kimevimba kwa kunenepa,
2815:28 Isa 5:9; Ay 3:14ataishi katika miji ya magofu,
na katika nyumba ambazo haziishi mwanadamu yeyote,
nyumba zinazokuwa vifusi.
2915:29 Ay 3:15; 7:8; Isa 5:8Hatatajirika tena, nao utajiri wake hautadumu,
wala mali zake hazitakuwa nyingi juu ya nchi.
3015:30 Ay 4:9, 15; 16:7; 20:26; Kut 15:10Hatatoka gizani;
mwali wa moto utanyausha machipukizi yake,
nayo pumzi ya kinywa cha Mungu itamwondolea mbali.
3115:31 Yer 7:4-8; Mt 6:19; Za 62:1015:31 Ay 31:5; Mit 1:16; 6:18; Isa 44:20; 59:7; Mik 2:11; Mk 13:5Asijidanganye mwenyewe kutumainia ubatili,
kwa kuwa hatapata malipo yoyote.
3215:32 Mhu 7:17; Za 109:8; Mit 10:27; Ay 18:16Atakuwa amelipwa kikamilifu kabla ya wakati wake,
nayo matawi yake hayatastawi.
3315:33 Hab 3:17Atafanana na mzabibu uliopukutishwa matunda yake kabla hayajaiva,
kama mzeituni unaodondosha maua yake.
3415:34 Kut 23:8; Ay 8:22; Isa 33:14Kwa kuwa jamii ya wasiomcha Mungu watakuwa tasa,
nao moto utateketeza hema za wale wanaopenda rushwa.
3515:35 Hos 10:13; Gal 6:7; Za 7:14Hutunga mimba ya madhara na kuzaa uovu;
matumbo yao huumba udanganyifu.”