Amosi 5 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 5:1-27

Maombolezo Na Wito Wa Toba

15:1 Yer 4:8; 7:29; Eze 9:1Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:

25:2 2Fal 19:21; Yer 14:17; 50:32; Amo 8:14“Bikira Israeli ameanguka,

kamwe hatainuka tena,

ameachwa pweke katika nchi yake,

hakuna yeyote wa kumwinua.”

35:3 Amo 6:9; Isa 6:13Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli,

mia moja tu watarudi;

wakati mji utakapopeleka mia moja,

kumi tu ndio watarudi hai.”

45:4 Kum 32:46-47; 4:29; Isa 55:3; 2Nya 15:2; Yer 29:13; Eze 18:9Hili ndilo Bwana asemalo kwa nyumba ya Israeli:

“Nitafuteni mpate kuishi;

55:5 1Sam 11:14; 7:16; 8:6; Mwa 21:31; Hos 4:15; Amu 8:14msitafute Betheli,

msiende Gilgali,

msisafiri kwenda Beer-Sheba.

Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni,

na Betheli itafanywa kuwa si kitu.”5:5 Yaani Aveni kwa Kiebrania, kumaanisha Beth-Aveni, jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

65:6 Sef 2:3; Amo 3:14; Law 18:5; Za 22:26; 105:4; Kum 4:24Mtafuteni Bwana mpate kuishi,

au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto;

utawateketeza, nayo Betheli

haitakuwa na yeyote wa kuuzima.

75:7 Isa 5:20; Amo 6:12; 3:10; Hos 10:4Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu

na kuiangusha haki chini

85:8 Ay 38:31-34; Mwa 1:16; Isa 42:16; Za 104:6-9, 20; Yer 16:21; Amo 4:13(yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni,

ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko

na mchana kuwa usiku,

ambaye huyaita maji ya bahari

na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:

Bwana ndilo jina lake;

9yeye hufanya maangamizo kwenye ngome

na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),

105:10 Isa 29:21; Mwa 4:16; 1Fal 22:8; Gal 4:16mnamchukia yule akemeaye mahakamani,

na kumdharau yule ambaye husema kweli.

115:11 Mik 6:15; Amo 8:6; 3:15; 9:14; Amu 9:27; Sef 1:13Mnamgandamiza maskini

na kumlazimisha awape nafaka.

Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari,

hamtaishi ndani yake;

ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu,

hamtakunywa divai yake.

125:12 Ay 5:4; 36:18; Isa 29:21; 5:23; 1:23; Hos 5:3; Eze 22:12; Yer 5:28; Amo 2:6-7Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu

na ukubwa wa dhambi zenu.

Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa

na kuzuia haki ya maskini mahakamani.

13Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo,

kwa kuwa nyakati ni mbaya.

145:14 Za 34:12-16; Mit 7:7; 11:27; Isa 1:16, 17; Mik 3:11; 6:8; Rum 2:7-9Tafuteni mema, wala si mabaya,

ili mpate kuishi.

Ndipo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atakuwa pamoja nanyi,

kama msemavyo yupo nanyi.

155:15 Rum 12:9; Yoe 2:14; Kut 32:30; Za 52:3; 97:10; Mik 5:7-8; 7:18; Mwa 18:25Yachukieni maovu, yapendeni mema;

dumisheni haki mahakamani.

Yamkini Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote

atawahurumia mabaki ya Yosefu.

165:16 Yer 9:17; 7:34; Sef 1:10; Yoe 1:11Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo:

“Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote

na vilio vya uchungu katika njia kuu zote.

Wakulima wataitwa kuja kulia,

na waombolezaji waje kuomboleza.

175:17 Kut 12:12; Isa 16:10; Yer 48:33Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu,

kwa kuwa nitapita katikati yenu,”

asema Bwana.

Siku Ya Bwana

185:18 Isa 2:12; 5:19, 30; Yoe 1:15; Ay 20:28; Yer 30:7; 1Sam 2:9Ole wenu ninyi mnaoitamani

siku ya Bwana!

Kwa nini mnaitamani siku ya Bwana?

Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.

195:19 Mhu 10:8; Kum 32:34; Ay 20:24; Mao 3:10; Eze 12:22; Mal 3:1; 2Pet 3:4; Isa 24:17-18; Yer 15:2-3Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba

kumbe akakutana na dubu,

kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake

na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta,

kumbe akaumwa na nyoka.

205:20 Oba 1:15; Eze 7:7; 1Sam 2:9; Isa 13:10; Sef 1:15Je, siku ya Bwana haitakuwa giza, na si nuru:

giza nene, bila mwonzi wa mwanga?

215:21 Law 26:31; Hos 2:11; Yer 44:4; Isa 1:11-16; Eze 23:18“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini;

siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.

225:22 Yer 14:12; 7:21; Mik 6:6-7; Isa 1:11-16; 66:3; Za 40:6; Amo 4:4Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka,

sitazikubali.

Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani,

sitazitambua.

23Niondoleeni kelele za nyimbo zenu!

Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.

245:24 Yer 22:3; Mik 6:8; Isa 45:8Lakini acheni haki itiririke kama mto,

na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!

255:25 Isa 43:23; Mdo 7:42; Kum 32:17; Kut 16:35“Je, mliniletea dhabihu na sadaka

kwa miaka arobaini kule jangwani,

ee nyumba ya Israeli?

265:26 Eze 18:6; 20:16Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu,

Sikuthi mungu wenu mtawala,

na Kiuni mungu wenu wa nyota,

ambao mliwatengeneza wenyewe.

275:27 Yer 38:17; Amo 6:7; Mdo 7:42-43; Mik 1:16; Kum 32:17-19Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,”

asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.

Ketab El Hayat

عاموس 5:1-27

مرثية ودعوة إلى التوبة

1اسْمَعُوا هَذِهِ الْمَرْثِيَّةَ الَّتِي أَرْثِيكُمْ بِها يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ. 2قَدْ سَقَطَتْ عَذْرَاءُ إِسْرَائِيلَ وَلَنْ تَنْهَضَ بَعْدُ. صَارَتْ طَرِيحَةً عَلَى أَرْضِهَا وَلَيْسَ مَنْ يُقِيمُهَا. 3لأَنَّهُ هَكَذَا يَقُولُ الرَّبُّ: إِنَّ الْمَدِينَةَ الَّتِي قَدَّمَتْ أَلْفاً مِنْ رِجَالِهَا لِلْحَرْبِ، لَا يَبْقَى لَهَا مِنْهُمْ سِوَى مِئَةٍ. وَالَّتِي قَدَّمَتْ مِئَةً مِنْهُمْ لِلْحَرْبِ لَا يَبْقَى لِبَيْتِ إِسْرَائِيلَ مِنْهُمْ سِوَى عَشَرَةٍ.

4لأَنَّ هَذَا مَا يَقُولُهُ الرَّبُّ لِبَيْتِ إِسْرَائِيلَ: الْتَمِسُونِي فَتَحْيَوْا. 5لَا تَسْعَوْا وَرَاءَ بَيْتِ إِيلَ، وَلا تَدْخُلُوا الْجِلْجَالَ، وَلا تَعْبُرُوا إِلَى بِئْرِ سَبْعٍ، لأَنَّ أَهْلَ الْجِلْجَالِ لابُدَّ أَنْ يَتِمَّ سَبْيُهُمْ، وَبَيْتَ إِيلَ تُصْبِحُ عَدَماً. 6الْتَمِسُوا الرَّبَّ فَتَحيَوْا لِئَلّا يَنْدَلِعَ كَنَارٍ تُحْرِقُ بَيْتَ يُوسُفَ وَتَلْتَهِمُ بَيْتَ إِيلَ، وَلَيْسَ مَنْ يُطْفِئُ. 7إِنَّكُمْ تُحَوِّلُونَ الْعَدْلَ مَرَارَةً، وَتَطْرَحُونَ الْحَقَّ إِلَى الأَرْضِ.

8إِنَّهُ هُوَ الَّذِي خَلَقَ الثُّرَيَّا وَالْجَبَّارَ، وَيُحَوِّلُ دَيَاجِيرَ الظُّلْمَةِ إِلَى نَهَارٍ، وَالنَّهَارَ إِلَى لَيْلٍ، وَيَسْتَدْعِي مِيَاهَ الْبَحْرِ وَيُفِيضُهَا عَلَى وَجْهِ الأَرْضِ، الرَّبُّ اسْمُهُ. 9الَّذِي يُنْزِلُ الْخَرَابَ بِالْقَوِيِّ، فَيَعْصِفُ الدَّمَارُ بِالْحُصُونِ. 10قَدْ أَبْغَضُوا مَنْ يُنَدِّدُ بِالْجَوْرِ فِي سَاحَةِ الْقَضَاءِ، وَيَكْرَهُونَ مَنْ يَنْطِقُ بِالْحَقِّ. 11فَلأَنَّكُمْ تَطَأُونَ الْمِسْكِينَ وَتَبْتَزُّونَ مِنْهُ رِشْوَةَ قَمْحٍ حَتَّى تُشَيِّدُوا بُيُوتاً مِنْ حِجَارَةٍ مَنْحُوتَةٍ، فَإِنَّكُمْ لَنْ تَسْكُنُوا فِيهَا، وَتَغْرِسُوا كُرُوماً شَهِيَّةً وَلَكِنَّكُمْ لَنْ تَشْرَبُوا مِنْ خَمْرِهَا. 12لأَنَّنِي عَالِمٌ بِكَثْرَةِ مَعَاصِيكُمْ وَعِظَمِ خَطَايَاكُمْ، إِذْ إِنَّكُمْ تُضَايِقُونَ الْبَارَّ أَيُّهَا الْمُرْتَشُونَ الَّذِينَ تَصُدُّونَ الْمِسْكِينَ عَنْ حَقِّهِ فِي سَاحَةِ الْقَضَاءِ. 13لِهَذَا يَصْمُتُ الْعَاقِلُ فِي مِثْلِ هَذَا الزَّمَانِ الرَّدِيءِ.

14اطْلُبُوا الْخَيْرَ لَا الشَّرَّ لِتَحْيَوْا، فَيَكُونَ الرَّبُّ الإِلَهُ الْقَدِيرُ مَعَكُمْ كَمَا تَقُولُونَ. 15امْقُتُوا الشَّرَّ وَأَحِبُّوا الْخَيْرَ وَأَقِيمُوا الْعَدْلَ فِي سَاحَةِ الْقَضَاءِ، لَعَلَّ الرَّبَّ الإِلَهَ الْقَدِيرَ يَتَرَفَّقُ عَلَى بَقِيَّةِ بَيْتِ يُوسُفَ.

16لِذَلِكَ، هَذَا مَا يَقُولُهُ الرَّبُّ الإِلَهُ الْقَدِيرُ، سَيَمْلأُ النَّحِيبُ أَرْجَاءَ السَّاحَاتِ، وَيَرْتَفِعُ عَوِيلُهُمْ فِي الشَّوَارِعِ قَائِلِينَ: آهِ! آهِ! وَيَدْعُونَ الْفَلاحِينَ إِلَى الْبُكَاءِ، وَالنَّادِبَاتِ إِلَى الرِّثَاءِ، 17وَتَعْلُو الْوَلْوَلَةُ فِي جَوَانِبِ الْكُرُومِ، لأَنِّي سَأَجْتَازُ مُنْتَقِماً فِي وَسَطِكُمْ يَقُولُ الرَّبُّ.

يوم الرب

18وَيْلٌ للَّذِينَ يَتَشَوَّقُونَ لِيَوْمِ الرَّبِّ. لِمَاذَا تَطْلُبُونَ مَجِيءَ يَوْمِ الرَّبِّ؟ فَيَوْمُ الرَّبِّ هُوَ ظُلْمَةٌ لَا نُورٌ. 19فَتَكُونُونَ كَرَجُلٍ هَرَبَ مِنْ وَجْهِ أَسَدٍ فَلَقِيَهُ دُبٌّ، أَوْ كَمَنْ دَخَلَ إِلَى بَيْتٍ وَاتَّكَأَ بِيَدِهِ عَلَى حَائِطٍ فَلَدَغَتْهُ أَفْعَى. 20أَوَ لَيْسَ يَوْمُ الرَّبِّ ظُلْمَةً لَا نُوراً، وَقَتَاماً خَالِياً مِنَ الضِّيَاءِ؟

21إِنِّي أَمْقُتُ أَعْيَادَكُمْ وَأَحْتَقِرُهَا، وَلا أُسَرُّ بِاحْتِفَالاتِكُمْ. 22وَمَعَ أَنَّكُمْ تُقَرِّبُونَ لِي ذَبَائِحَ مُحْرَقَاتِكُمْ وَتَقْدِمَاتِكُمْ مِنَ الدَّقِيقِ، فَإِنِّي لَا أَقْبَلُهَا وَلا أَلْتَفِتُ إِلَى ذَبَائِحِ السَّلامِ مِنْ مُسَمَّنَاتِ مَوَاشِيكُمْ. 23أَبْعِدُوا عَنِّي جَلَبَةَ أَغَانِيكُمْ لأَنِّي لَنْ أَصْغِيَ إِلَى نَغَمَاتِ رَبَابَاتِكُمْ. 24إِنَّمَا لِيَجْرِ الْحَقُّ مُتَدَفِّقاً كَالْمِيَاهِ وَالْعَدْلُ كَنَهْرٍ سَيَّالٍ.

25هَلْ قَرَّبْتُمْ لِي ذَبَائِحَ وَتَقْدِمَاتٍ طَوَالَ أَرْبَعِينَ سَنَةً فِي الْبَرِّيَّةِ، يَا بَيْتَ إِسْرَائِيلَ؟ 26بَلْ إِنَّ الْمَلِكَ الَّذِي حَمَلْتُمْ خَيْمَتَهُ وَنَصْبَ تَمَاثِيلِهِ لَمْ يَكُنْ سِوَى نَجْمٍ صَنَعْتُمُوهُ لأَنْفُسِكُمْ وَعَبَدْتُمُوهُ كَإِلَهٍ. 27لِذَلِكَ أَسْبِيكُمْ إِلَى مَا وَرَاءَ دِمَشْقَ، يَقُولُ الرَّبُّ الَّذِي اسْمُهُ الإِلَهُ الْقَدِيرُ.