2 Wathesalonike 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wathesalonike 3:1-18

Hitaji La Maombi

13:1 1The 4:1; 5:25; 1:8Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu. 23:2 Rum 15:31Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini. 33:3 1Kor 1:9; Mt 5:37Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu. 43:4 2Kor 2:3Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza. 53:5 1Nya 29:18Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.

Onyo Dhidi Ya Uvivu

63:6 1Kor 5:4; Rum 16:17; 1Kor 11:2Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa. 73:7 1Kor 4:16Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi, 83:8 Mdo 18:3; Efe 4:28wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu. 93:9 1Kor 9:4-14; 4:16Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo. 103:10 1The 3:4; 4:11Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”

113:11 1Tim 5:13Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine. 123:12 1The 4:1; 4:11; Efe 4:28Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe. 133:13 Gal 6:9Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.

143:14 Rum 16:17Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu. 153:15 Gal 6:1Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.

Salamu Za Mwisho

163:16 Rum 15:33; Rut 2:4Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.

173:17 1Kor 16:21Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.

183:18 Rum 16:20Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.

New International Version – UK

2 Thessalonians 3:1-18

Request for prayer

1As for other matters, brothers and sisters, pray for us that the message of the Lord may spread rapidly and be honoured, just as it was with you. 2And pray that we may be delivered from wicked and evil people, for not everyone has faith. 3But the Lord is faithful, and he will strengthen you and protect you from the evil one. 4We have confidence in the Lord that you are doing and will continue to do the things we command. 5May the Lord direct your hearts into God’s love and Christ’s perseverance.

Warning against idleness

6In the name of the Lord Jesus Christ, we command you, brothers and sisters, to keep away from every believer who is idle and disruptive and does not live according to the teaching3:6 Or tradition you received from us. 7For you yourselves know how you ought to follow our example. We were not idle when we were with you, 8nor did we eat anyone’s food without paying for it. On the contrary, we worked night and day, labouring and toiling so that we would not be a burden to any of you. 9We did this, not because we do not have the right to such help, but in order to offer ourselves as a model for you to imitate. 10For even when we were with you, we gave you this rule: ‘The one who is unwilling to work shall not eat.’

11We hear that some among you are idle and disruptive. They are not busy; they are busybodies. 12Such people we command and urge in the Lord Jesus Christ to settle down and earn the food they eat. 13And as for you, brothers and sisters, never tire of doing what is good.

14Take special note of anyone who does not obey our instruction in this letter. Do not associate with them, in order that they may feel ashamed. 15Yet do not regard them as an enemy, but warn them as you would a fellow believer.

Final greetings

16Now may the Lord of peace himself give you peace at all times and in every way. The Lord be with all of you.

17I, Paul, write this greeting in my own hand, which is the distinguishing mark in all my letters. This is how I write.

18The grace of our Lord Jesus Christ be with you all.