2 Wakorintho 10 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

2 Wakorintho 10:1-18

Paulo Atetea Huduma Yake

110:1 Mt 11:29; Gal 5:2; Efe 3:1Basi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi! 210:2 1Kor 4:21; Rum 12:2Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu. 310:3 2Kor 10:2Ingawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 410:4 2Kor 6:7; Yer 1:10; 2Kor 13:10Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome, 510:5 Isa 2:10-12; 1Kor 1:19; 2Kor 9:13tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo, 610:6 2Kor 6:9; 7:15tena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.

710:7 Yn 7:24; 2Kor 5:12; 1Kor 1:12; 3:23; 14:37; 2Kor 11:23Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo. 810:8 Yer 1:10; 2Kor 13:10Basi hata kama nikijisifu zaidi kidogo kuhusu mamlaka tuliyo nayo, ambayo Bwana alitupa ili kuwajenga wala si kuwabomoa, mimi sitaionea haya. 910:9 1Kor 2:3; Gal 4:13-14; 1Kor 1:17; 2Kor 11:6Sitaki nionekane kama ninayejaribu kuwatisha kwa nyaraka zangu. 1010:10 1Kor 2:3; Gal 4:13-14; 1Kor 1:17; 2Kor 11:6Kwa maana wanasema, “Nyaraka zake ni nzito na zenye nguvu, lakini ana kwa ana ni dhaifu na kuzungumza kwake ni kwa kudharauliwa.” 1110:11 2Kor 13:2, 10Watu kama hao wajue ya kuwa, yale tusemayo kwa barua tukiwa hatupo pamoja nanyi, ndivyo tulivyo na ndivyo tutakavyofanya tutakapokuwa pamoja nanyi.

1210:12 2Kor 3:1Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojitukuza wenyewe kuwa wao ni wa maana sana. Wanapojipima na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara. 1310:13 Rum 12:3Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ile Mungu aliyotuwekea, mipaka ambayo inawafikia hata ninyi. 1410:14 1Kor 3:6; 2Kor 2:12Kwa maana hatukuwa tunavuka mipaka katika kujisifu kwetu, kama vile ambavyo ingekuwa kama hatukuwa tumekuja kwenu. Kwa maana sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuja kwenu na Injili ya Kristo. 1510:15 Rum 15:20; 2The 1:3Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi, 1610:16 Rum 1:1; 2Kor 2:12; Mdo 19:21ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine. 1710:17 Yer 9:24; Za 34:2; 44:8; 1Kor 1:31Lakini, “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.” 1810:18 Rum 2:29Kwa maana si yeye ajisifuye mwenyewe akubaliwaye, bali yeye ambaye Bwana humsifu.