2 Wafalme 7 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 7:1-20

17:1 2Fal 7:16Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja7:1 Kipimo kimoja cha unga ni sawa na kilo 3. cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha,7:1 Shekeli moja ya fedha ni sawa na gramu 11. na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”

27:2 Mwa 7:11; Mal 3:10Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?”

Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”

Mwisho Wa Kuzingirwa

37:3 Law 13:45-46; Hes 5:1-4Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe? 4Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”

5Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu, 67:6 Kut 14:24; Yer 46:21kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!” 77:7 Za 48:4-6; Mit 28:1Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.

87:8 Isa 33:23Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.

9Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”

10Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.” 11Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.

127:12 Yos 8:4Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’ ”

13Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”

14Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.” 15Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme. 167:16 Isa 33:4Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.

177:17 2Fal 7:2Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake. 18Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”

197:19 2Fal 7:2Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!” 20Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

4 Царств 7:1-20

1Но Елисей сказал:

– Слушай слово Вечного. Так говорит Вечный: «Завтра к этому времени у ворот Сомарии пять килограммов лучшей муки и десять килограммов ячменя будут продаваться всего лишь за двенадцать граммов серебра»7:1 Букв.: «одна сата… две саты… за один шекель». Также в ст. 16 и 18..

2Ближайший к царю сановник сказал пророку:

– Послушай, этого не может быть, даже если Вечный откроет небесные окна!

– Ты увидишь это своими глазами, – ответил Елисей, – но есть не будешь!

Конец осады

3У входа в городские ворота сидели четверо прокажённых7:3 См. сноску на 5:1.. Они сказали друг другу:

– Чего нам сидеть тут и ждать смерти? 4Если мы решим пойти в город, то там голод, и мы умрём. И если мы останемся здесь, то всё равно умрём. Давайте же пойдём в лагерь к сирийцам и сдадимся. Если они пощадят нас, останемся в живых, а если нет, то умрём.

5В вечерних сумерках они встали и пошли в лагерь сирийцев. Когда они добрались до края лагеря, там никого не было, 6потому что Владыка сделал так, что сирийцы услышали шум колесниц, коней и огромного войска, и они сказали друг другу:

– Это царь Исроила нанял хеттейских и египетских царей, чтобы напасть на нас!

7Они встали и в сумерках бежали, бросив шатры, лошадей и ослов. Они бросили лагерь, как он был, и спасались бегством. 8Прокажённые добрались до края лагеря и вошли в один из шатров. Они наелись, напились и унесли оттуда серебро, золото и одежды, ушли и спрятали их. Потом они вернулись и вошли в другой шатёр и, взяв кое-что и из него, ушли и спрятали это тоже. 9Затем они сказали друг другу:

– Мы поступаем неправильно. Это день хороших вестей, а мы держим их при себе. Если мы будем ждать рассвета, нас постигнет кара. Пойдём сейчас же и доложим об этом в царском дворце.

10Они пошли, позвали городских привратников и сказали им:

– Мы ходили в лагерь сирийцев, но там никого не видно и не слышно. Только привязанные кони, ослы и шатры, как они были.

11Привратники разгласили весть, и об этом было доложено во дворце. 12Царь встал ночью и сказал своим приближённым:

– Я скажу вам, что сделали сирийцы. Они знают, что мы голодаем, и покинули лагерь, чтобы спрятаться в поле, думая: «Они непременно выйдут, мы возьмём их живыми и войдём в город».

13Один из его приближённых сказал:

– Пусть возьмут пять из оставшихся лошадей и узнают, что произошло. Ведь те, кто уцелел, здесь всё равно разделят судьбу всего множества исроильтян, которое уже погибло.

14Они взяли две колесницы с конями, и царь послал их за сирийским войском. Он приказал колесничим:

– Пойдите и узнайте, что произошло.

15Они ехали по следам сирийского войска до самого Иордана и видели, что вся дорога усеяна одеждами и снаряжением сирийцев, которые те бросали во время стремительного бегства. Посланцы вернулись и доложили об увиденном царю. 16Народ вышел и разграбил лагерь сирийцев. Пять килограммов лучшей муки и десять килограммов ячменя стали продавать всего лишь за двенадцать граммов серебра, как и сказал Вечный. 17А царь поставил своего ближайшего сановника следить за порядком в городских воротах, и там его растоптала толпа. Он умер, как и предсказывал пророк, когда царь приходил к нему домой. 18(Когда пророк говорил царю: «Завтра к этому времени у ворот Сомарии пять килограммов лучшей муки и десять килограммов ячменя будут продавать всего лишь за двенадцать граммов серебра», 19тот сановник сказал пророку: «Послушай, этого не может быть, даже если Вечный откроет небесные окна!» Тогда пророк ответил: «Ты увидишь это своими глазами, но есть не будешь!») 20Так с ним и произошло: толпа растоптала его в воротах, и он умер.