2 Wafalme 21 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 21:1-26

Manase Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 33:1-20)

121:1 2Fal 21:16Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na mitano. Mama yake aliitwa Hefsiba. 221:2 Yer 15:4; 2Fal 16:3Akafanya maovu machoni pa Bwana, akafuata desturi za machukizo za mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli. 321:3 Amu 6:28; Kum 17:3Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amepabomoa. Pia akasimamisha madhabahu za Baali na kutengeneza nguzo ya Ashera, kama Ahabu mfalme wa Israeli alivyofanya. Akalisujudia jeshi lote la angani na kuliabudu. 421:4 Isa 66:4; Kut 20:24Akajenga madhabahu katika Hekalu la Bwana, ambamo Bwana alikuwa amesema, “Katika Yerusalemu nitaliweka Jina langu.” 521:5 1Fal 17:12Katika nyua zote mbili za Hekalu la Bwana, akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la angani. 621:6 Law 18:21; Kum 18:14; 2Fal 23:26Akamtoa kafara mwanawe mwenyewe katika moto, akafanya uchawi na uaguzi, na akataka shauri kwa wapiga ramli na kwa mizimu. Akafanya maovu mengi sana machoni mwa Bwana na kumghadhibisha.

721:7 Kum 16:21; Law 15:31; Kut 20:24Akachukua nguzo ya Ashera aliyoichonga na kuiweka katika Hekalu, ambalo Bwana alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele. 821:8 2Sam 7:10Sitaifanya tena miguu ya Waisraeli itangetange kutoka nchi niliyowapa baba zao, ikiwa watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru, na kuishika Sheria yote ambayo walipewa na Mose mtumishi wangu.” 921:9 1Fal 14:9; Eze 5:7Lakini hawa watu hawakusikiliza. Manase akawapotosha, hivyo kwamba walifanya maovu mengi kuliko mataifa ambayo Bwana aliyaangamiza mbele ya Waisraeli.

10Bwana akasema kupitia watumishi wake manabii: 1121:11 1Fal 14:9; Mwa 15:6“Manase mfalme wa Yuda ametenda dhambi hizi za kuchukiza. Amefanya maovu mengi kuliko Waamori waliokuwepo kabla yake, na ameiongoza Yuda katika dhambi kwa sanamu zake. 1221:12 Yer 15:4; 1Sam 3:11Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nitaleta maafa makubwa juu ya Yerusalemu na Yuda, kiasi kwamba masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yatawasha. 1321:13 Isa 34:11; Amo 7:7-9Nitanyoosha juu ya Yerusalemu kamba ya kupimia iliyotumika dhidi ya Samaria, na timazi iliyotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu. Nitaifutilia mbali Yerusalemu kama mtu afutaye sahani, nikiifuta na kuifunikiza. 1421:14 2Fal 19:4; Za 78:60Nitawakataa mabaki wa urithi wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao. Watapokonywa mali zao na kutekwa nyara na adui zao wote, 1521:15 Yer 25:7kwa sababu wametenda uovu machoni pangu na kunighadhibisha tangu siku baba zao walipotoka Misri mpaka siku ya leo.”

1621:16 2Fal 24:4; Mao 4:13; Sef 1:12Zaidi ya hayo, Manase pia alimwaga damu nyingi isiyo na hatia, hivi kwamba aliijaza Yerusalemu kutoka mwanzo hadi mwisho, mbali na dhambi ambayo alikuwa amesababisha Yuda kufanya, na hivyo wakatenda maovu machoni pa Bwana.

17Matukio mengine ya utawala wa Manase, na yote aliyoyafanya, pamoja na dhambi alizotenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 1821:18 Es 1:5; 7:7Manase akalala pamoja na baba zake na akazikwa katika bustani ya jumba lake la kifalme, katika bustani ya Uza. Naye Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.

Amoni Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 33:21-25)

19Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili. Mamaye aliitwa Meshulemethi binti Haruzi, kutoka Yotba. 2021:20 1Fal 15:26Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya. 21Akaenenda katika njia zote za baba yake, akaabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu na kuzisujudia. 2221:22 1Fal 11:33; 1Sam 8:8Akamwacha Bwana, Mungu wa baba zake, wala hakuenenda katika njia za Bwana.

23Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani. 24Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme mahali pake.

25Matukio mengine ya utawala wa Amoni na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 26Akazikwa kwenye kaburi lake katika bustani ya Uza. Naye Yosia mwanawe akawa mfalme baada yake.

Persian Contemporary Bible

دوم پادشاهان 21:1-26

منسی، پادشاه يهودا

(دوم تواريخ 33‏:1‏-20)

1منسی دوازده ساله بود كه پادشاه يهودا شد و پنجاه و پنج سال در اورشليم سلطنت نمود. (اسم مادرش حفصيبه بود.) 2او از اعمال زشت قومهای بت‌پرستی كه خداوند آنها را از كنعان بيرون رانده بود، پيروی می‌كرد و نسبت به خداوند گناه می‌ورزيد.

3‏-5منسی معبدهای بالای تپه‌ها را كه پدرش حزقيا خراب كرده بود، دوباره بنا نمود، قربانگاه‌هايی برای بعل درست كرد و بت شرم‌آور اشيره را همانطور كه اخاب، پادشاه اسرائيل درست كرده بود، دوباره ساخت. منسی آفتاب و ماه و ستارگان را پرستش می‌كرد و برای آنها قربانگاه‌هايی ساخت و آنها را در حياط خانهٔ خداوند قرار داد، يعنی در همان خانه و شهری كه خداوند برای نام خود برگزيده بود. 6منسی پسر خود را به عنوان قربانی سوزانيد. او جادوگری و فالگيری می‌كرد و با احضاركنندگان ارواح و جادوگران مشورت می‌نمود. او با اين كارهای شرارت‌آميز، خداوند را به خشم آورد. 7او حتی بت شرم‌آور اشيره را در خانهٔ خداوند بر پا نمود، يعنی در همان مكانی كه خداوند راجع به آن به داوود و سليمان گفته بود: «نام خود را تا به ابد بر اين خانه و بر اورشليم، شهری كه از ميان شهرهای قبايل اسرائيل برای خود انتخاب كرده‌ام، خواهم نهاد. 8اگر قوم اسرائيل از دستوراتی كه من بوسيلهٔ موسی به آنها داده‌ام پيروی نمايند، بار ديگر هرگز ايشان را از اين سرزمين كه به اجداد ايشان دادم، بيرون نخواهم راند.» 9اما ايشان نه فقط از خداوند اطاعت نكردند، بلكه بدتر از قومهايی كه خداوند آنها را از كنعان بيرون رانده بود، رفتار نمودند زيرا منسی ايشان را گمراه نموده بود.

10پس خداوند بوسيلهٔ خدمتگزاران خود، انبيا چنين فرمود: 11«چون منسی، پادشاه يهودا اين اعمال قبيح را انجام داده و حتی بدتر از اموری‌هايی كه در گذشته در اين سرزمين ساكن بودند، رفتار نموده و مردم يهودا را به بت‌پرستی كشانيده است؛ 12من نيز بر اورشليم و يهودا چنان بلايی نازل خواهم كرد كه هر كه آن را بشنود وحشت كند. 13همان بلايی را سر اورشليم می‌آورم كه بر سر سامره و خاندان اخاب آوردم. اورشليم را از لوث وجود ساكنانش پاک می‌كنم، درست همانطور كه ظرف را پاک كرده، می‌شويند و آن را وارونه می‌گذارند تا خشک شود. 14بازماندگان قوم را نيز ترک خواهم گفت و ايشان را به دست دشمن خواهم سپرد تا آنها را غارت كنند، 15زيرا ايشان نسبت به من گناه ورزيده‌اند و از روزی كه اجدادشان را از مصر بيرون آوردم تا به امروز مرا خشمگين نموده‌اند.»

16منسی علاوه بر اين كه اهالی يهودا را به بت‌پرستی كشانده، باعث شد آنها نسبت به خداوند گناه ورزند، افراد بی‌گناه بی‌شماری را نيز كشت و اورشليم را با خون آنها رنگين ساخت.

17شرح بقيهٔ رويدادهای دوران سلطنت منسی و اعمال گناه‌آلود او در كتاب «تاريخ پادشاهان يهودا» نوشته شده است. 18وقتی منسی مرد او را در باغ كاخ خودش كه عوزا نام داشت دفن كردند و پسرش آمون به جای وی پادشاه شد.

آمون، پادشاه يهودا

(دوم تواريخ 33‏:21‏-25)

19آمون بيست و دو ساله بود كه پادشاه يهودا شد و دو سال در اورشليم سلطنت كرد. (مادرش مشلمت، دختر حاروص از اهالی يطبه بود.) 20او نيز مانند پدرش منسی نسبت به خداوند گناه ورزيد.

21آمون از تمام راههای بد پدرش پيروی می‌نمود و بتهای پدرش را می‌پرستيد. 22او از خداوند، خدای اجدادش برگشت و به دستورات خداوند عمل نكرد. 23سرانجام افرادش بر ضد او توطئه چيدند و او را در كاخ سلطنتی‌اش به قتل رساندند. 24مردم قاتلان آمون را كشتند و پسرش يوشيا را به جای او بر تخت سلطنت نشاندند. 25شرح بقيه رويدادهای دوران سلطنت آمون در كتاب «تاريخ پادشاهان يهودا» ثبت گرديده است. 26او را در آرامگاه باغ عوزا دفن كردند و پسرش يوشيا به جای او پادشاه شد.