2 Wafalme 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

2 Wafalme 2:1-25

Eliya Achukuliwa Mbinguni

12:1 Mwa 5:24; 1Fal 19:16Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali. 22:2 Rut 1:16Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.”

Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.

32:3 1Sam 10:5Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?”

Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”

42:4 Yos 3:16Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.”

Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.

52:5 2Fal 2:3Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?”

Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”

62:6 Yos 3:15Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.”

Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.

7Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani. 82:8 Kut 14:21Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.

92:9 Kum 21:17; Hes 11:17Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?”

Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”

10Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”

112:11 2Fal 6:17; Za 104:3, 4Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli. 122:12 2Fal 13:14; Mwa 37:29Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.

13Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani. 142:14 1Fal 19:19Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.

152:15 1Sam 10:5; Hes 11:17Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake. 162:16 1Fal 18:12; Mdo 8:39Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.”

Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”

172:17 Amu 3:25Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata. 18Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”

Kuponywa Kwa Maji

19Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”

20Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.

212:21 Kut 15:25; 2Fal 4:41; 6:6Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’ ” 222:22 Kut 15:22Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.

Elisha Anafanyiwa Mzaha

232:23 2Nya 30:10; Za 31:18Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!” 242:24 Mwa 4:11; Kum 18:19Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao. 25Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

列王紀下 2:1-25

以利亞被接到天上

1耶和華用旋風接以利亞升天之前,以利亞以利沙正離開吉甲2以利亞以利沙說:「你留在這裡吧,耶和華差遣我去伯特利。」以利沙說:「我憑永活的耶和華和你的性命起誓,我決不離開你。」於是二人前往伯特利3伯特利的眾先知出來見以利沙,問他:「你知道耶和華今天要接走你師傅嗎?」他說:「我知道,請不要作聲。」

4以利亞以利沙說:「你留在這裡吧,耶和華差遣我去耶利哥。」以利沙說:「我憑永活的耶和華和你的性命起誓,我決不離開你。」於是二人前往耶利哥5耶利哥的眾先知來見以利沙,問他:「你知道耶和華今天要接走你師傅嗎?」他說:「我知道,請不要作聲。」

6以利亞以利沙說:「你留在這裡吧,耶和華差遣我去約旦河。」以利沙說:「我憑永活的耶和華和你的性命起誓,我決不離開你。」於是二人繼續前行。 7先知中有五十人跟他們來到約旦河,遠遠地站著,他們二人則站在河邊。 8以利亞脫下外衣捲起來,用它擊打河水,水立即左右分開,二人腳踏乾地而過。

9到對岸後,以利亞以利沙說:「在我被接走之前,你要我為你做什麼?」以利沙說:「請將你的靈加倍給我。」 10以利亞說:「這是個很難的要求。不過,我被接走的時候,你若看得見我,就可以得到,否則就得不到。」 11他們邊走邊談,忽然有火馬拉的火車把他們二人隔開,以利亞乘著旋風升上了天。 12以利沙見此情景,便喊道:「我父啊!我父啊!以色列的戰車和騎兵啊!」以利沙以利亞消失在天空中,就悲傷地把自己的衣服撕成兩半。

13他拿起以利亞身上掉下來的外衣,回到約旦河邊, 14用它擊打河水,說:「以利亞的上帝耶和華在哪裡呢?」河水就左右分開,以利沙便過了河。

15耶利哥的先知們從遠處看見他,就說:「以利亞的靈降在以利沙身上了。」他們就上前迎接,俯伏在他面前, 16說:「僕人們這裡有五十個壯士,請讓他們去尋找你師傅吧,也許耶和華的靈把他提走,放在某座山上或某個山谷裡了。」以利沙說:「你們不要派人去找了。」 17他們再三懇求,以利沙難以推辭,就讓他們派人去了。他們派去了五十人,找了三天也沒有找到。 18他們回來的時候,以利沙仍在耶利哥。他對他們說:「我不是早就告訴你們不要去嗎?」

以利沙行神蹟

19耶利哥城的人對以利沙說:「我主,你看這城地勢很好,只是水不好,地裡長不出莊稼。」 20以利沙說:「拿一個新碗裝些鹽給我。」他們就去照辦。 21以利沙走到水源那裡,把鹽倒在水中說:「耶和華說,『我潔淨了這水,從此它不會再使人死亡,也不會再使土地貧瘠。』」 22果然如以利沙所說,那裡的水變好了,直到如今。

23以利沙從那裡去伯特利,正在趕路的時候,從城裡出來一群少年譏笑他說:「禿頭,上去吧!禿頭,上去吧!」 24以利沙轉身看著他們,奉耶和華的名咒詛他們。林中隨即走出來兩隻母熊,咬死了其中的四十二個少年。 25以利沙伯特利上了迦密山,又從迦密山回到撒瑪利亞