2 Timotheo 3 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

2 Timotheo 3:1-17

Hatari Za Siku Za Mwisho

13:1 1Tim 4:1; 2Pet 3:3; 2Tim 4:3; 1Yn 2:18; Yud 18Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari. 23:2 1Tim 3:3; Rum 1:30Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu, 33:3 Rum 1:31; 2Pet 3:3wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema, 43:4 1Tim 3:6; 2Pet 2:10; Flp 3:19; 2Pet 2:13; Yud 4, 9wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu: 53:5 1Tim 5:8; Tit 1:16; 2The 3:6; 1Tim 6:5wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.

63:6 Yud 4; Mt 23:14; Tit 1:11Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya. 73:7 1Tim 2:4; 2Tim 1:11Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli. 83:8 Kut 7:11; Mdo 13:8; 1Tim 6:5Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani. 93:9 Kut 8:18; 9:11; 7:12Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.

Paulo Amwagiza Timotheo

103:10 1Tim 4:6; Flp 2:22Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu, 113:11 Mdo 13:14, 50; 2Kor 11:23-27; Za 34:19mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote. 123:12 Mdo 14:22; Za 34:19; Mdo 14:22; Mt 16:24; Yos 17:14; 1Kor 15:19Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa. 133:13 2Tim 2:16; 2The 2:11; 1Tim 4:1Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. 143:14 2Tim 1:13; 2:2Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani, 153:15 Yn 5:39; Za 119:98-99na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. 163:16 2Pet 1:20-21; Rum 4:23-24Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki, 173:17 1Tim 6:11; 2Tim 2:21ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.

New International Version

2 Timothy 3:1-17

1But mark this: There will be terrible times in the last days. 2People will be lovers of themselves, lovers of money, boastful, proud, abusive, disobedient to their parents, ungrateful, unholy, 3without love, unforgiving, slanderous, without self-control, brutal, not lovers of the good, 4treacherous, rash, conceited, lovers of pleasure rather than lovers of God— 5having a form of godliness but denying its power. Have nothing to do with such people.

6They are the kind who worm their way into homes and gain control over gullible women, who are loaded down with sins and are swayed by all kinds of evil desires, 7always learning but never able to come to a knowledge of the truth. 8Just as Jannes and Jambres opposed Moses, so also these teachers oppose the truth. They are men of depraved minds, who, as far as the faith is concerned, are rejected. 9But they will not get very far because, as in the case of those men, their folly will be clear to everyone.

A Final Charge to Timothy

10You, however, know all about my teaching, my way of life, my purpose, faith, patience, love, endurance, 11persecutions, sufferings—what kinds of things happened to me in Antioch, Iconium and Lystra, the persecutions I endured. Yet the Lord rescued me from all of them. 12In fact, everyone who wants to live a godly life in Christ Jesus will be persecuted, 13while evildoers and impostors will go from bad to worse, deceiving and being deceived. 14But as for you, continue in what you have learned and have become convinced of, because you know those from whom you learned it, 15and how from infancy you have known the Holy Scriptures, which are able to make you wise for salvation through faith in Christ Jesus. 16All Scripture is God-breathed and is useful for teaching, rebuking, correcting and training in righteousness, 17so that the servant of God3:17 Or that you, a man of God, may be thoroughly equipped for every good work.