2 Samweli 24 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

2 Samweli 24:1-25

Daudi Ahesabu Wapiganaji

(1 Nyakati 21:1-27)

124:1 Yos 9:15; Ay 1:6; Zek 3:1; Kut 30:12; 1Nya 27:23; 2Sam 16:10; 21:11; 1Fal 22:22; 1Nya 21:1; Yak 1:13Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”

224:2 2Sam 20:23; 3:10; 2Nya 2:17; 17:14; 25:5; Amu 20:1; Mwa 26:4; Kum 8:13-14; 2Nya 32:25-26; Mit 18:12; 29:23; Yer 17:5Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”

324:3 2Sam 2:18; Kum 1:11Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”

424:4 1Nya 21:4; Mhu 8:4; Mdo 5:29Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.

524:5 Yos 13:9; Hes 21:32; Kum 2:36Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri. 624:6 Mwa 10:19; Amu 1:31; Yos 19:28; Amu 18:28-29Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni. 724:7 Yos 19:29; Kut 3:8; Kum 1:31; Yos 11:3; Mwa 21:21-33Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.

8Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.

924:9 Hes 1:44-46; 1Nya 21:5Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.

1024:10 1Sam 24:5; Hes 22:34; 12:11; 2Sam 12:13; 1Sam 13:13; Mit 18:4; 1Yn 3:20; 1Nya 21:8; Ay 33:27-28; Za 25:11Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”

1124:11 1Sam 22:5; 9:9; 1Nya 29:29Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema: 12“Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’ ”

1324:13 Kum 28:28-48; 32:24; Eze 14:21; Kut 5:3; 30:12; Law 26:25; Kum 28:21-28, 35; 1Nya 21:12Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”

1424:14 Neh 9:28; Za 4:1; 51:1; 103:8-13; Isa 54:7; 55:7; Yer 33:8; 42:12; Dan 9:9; Isa 47:6; Zek 1:15Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”

1524:15 1Nya 24:24; 21:14; 27:24Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba. 1624:16 Mwa 6:6; 16:7; 19:13; Kut 12:23; Mdo 12:23; 1Nya 21:15; Za 104:4; 1Sam 15:11; Za 78:38; Yer 18:5-10; Yoe 2:13; Yon 3:10Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna,24:16 Pia anaitwa Ornani kwa Kiebrania. Myebusi.

1724:17 Za 74:1; 100:3; Yer 49:20; Mwa 18:23; Yon 1:12; 1Nya 21:17Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”

Daudi Ajenga Madhabahu

1824:18 Mwa 22:2; 2Nya 3:1Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.” 19Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi. 20Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.

2124:21 Hes 16:44-50; Mwa 23:8Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?”

Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”

2224:22 1Sam 6:14; 1Fal 19:21Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni. 2324:23 Mwa 23:11; Eze 20:40-41; Za 20:3; 119:108; 1Pet 2:5Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”

2424:24 Mal 1:13-14; Mwa 23:16Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.”

Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.24:24 Shekeli 50 za fedha ni sawa na gramu 600. 2524:25 1Sam 7:17; 2Sam 21:14; 1Nya 21:28; 22:1; 2Sam 21:14; 2Nya 33:13Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.

New International Version

2 Samuel 24:1-25

David Enrolls the Fighting Men

1Again the anger of the Lord burned against Israel, and he incited David against them, saying, “Go and take a census of Israel and Judah.”

2So the king said to Joab and the army commanders24:2 Septuagint (see also verse 4 and 1 Chron. 21:2); Hebrew Joab the army commander with him, “Go throughout the tribes of Israel from Dan to Beersheba and enroll the fighting men, so that I may know how many there are.”

3But Joab replied to the king, “May the Lord your God multiply the troops a hundred times over, and may the eyes of my lord the king see it. But why does my lord the king want to do such a thing?”

4The king’s word, however, overruled Joab and the army commanders; so they left the presence of the king to enroll the fighting men of Israel.

5After crossing the Jordan, they camped near Aroer, south of the town in the gorge, and then went through Gad and on to Jazer. 6They went to Gilead and the region of Tahtim Hodshi, and on to Dan Jaan and around toward Sidon. 7Then they went toward the fortress of Tyre and all the towns of the Hivites and Canaanites. Finally, they went on to Beersheba in the Negev of Judah.

8After they had gone through the entire land, they came back to Jerusalem at the end of nine months and twenty days.

9Joab reported the number of the fighting men to the king: In Israel there were eight hundred thousand able-bodied men who could handle a sword, and in Judah five hundred thousand.

10David was conscience-stricken after he had counted the fighting men, and he said to the Lord, “I have sinned greatly in what I have done. Now, Lord, I beg you, take away the guilt of your servant. I have done a very foolish thing.”

11Before David got up the next morning, the word of the Lord had come to Gad the prophet, David’s seer: 12“Go and tell David, ‘This is what the Lord says: I am giving you three options. Choose one of them for me to carry out against you.’ ”

13So Gad went to David and said to him, “Shall there come on you three24:13 Septuagint (see also 1 Chron. 21:12); Hebrew seven years of famine in your land? Or three months of fleeing from your enemies while they pursue you? Or three days of plague in your land? Now then, think it over and decide how I should answer the one who sent me.”

14David said to Gad, “I am in deep distress. Let us fall into the hands of the Lord, for his mercy is great; but do not let me fall into human hands.”

15So the Lord sent a plague on Israel from that morning until the end of the time designated, and seventy thousand of the people from Dan to Beersheba died. 16When the angel stretched out his hand to destroy Jerusalem, the Lord relented concerning the disaster and said to the angel who was afflicting the people, “Enough! Withdraw your hand.” The angel of the Lord was then at the threshing floor of Araunah the Jebusite.

17When David saw the angel who was striking down the people, he said to the Lord, “I have sinned; I, the shepherd,24:17 Dead Sea Scrolls and Septuagint; Masoretic Text does not have the shepherd. have done wrong. These are but sheep. What have they done? Let your hand fall on me and my family.”

David Builds an Altar

18On that day Gad went to David and said to him, “Go up and build an altar to the Lord on the threshing floor of Araunah the Jebusite.” 19So David went up, as the Lord had commanded through Gad. 20When Araunah looked and saw the king and his officials coming toward him, he went out and bowed down before the king with his face to the ground.

21Araunah said, “Why has my lord the king come to his servant?”

“To buy your threshing floor,” David answered, “so I can build an altar to the Lord, that the plague on the people may be stopped.”

22Araunah said to David, “Let my lord the king take whatever he wishes and offer it up. Here are oxen for the burnt offering, and here are threshing sledges and ox yokes for the wood. 23Your Majesty, Araunah24:23 Some Hebrew manuscripts and Septuagint; most Hebrew manuscripts King Araunah gives all this to the king.” Araunah also said to him, “May the Lord your God accept you.”

24But the king replied to Araunah, “No, I insist on paying you for it. I will not sacrifice to the Lord my God burnt offerings that cost me nothing.”

So David bought the threshing floor and the oxen and paid fifty shekels24:24 That is, about 1 1/4 pounds or about 575 grams of silver for them. 25David built an altar to the Lord there and sacrificed burnt offerings and fellowship offerings. Then the Lord answered his prayer in behalf of the land, and the plague on Israel was stopped.