2 Samweli 20 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

2 Samweli 20:1-26

Sheba Aasi Dhidi Ya Daudi

120:1 Mwa 31:14; 29:14; 1Fal 12:16; 1Sam 22:7-8; 2Nya 10:16; 2Sam 12:10; Kum 13:13; Amu 19:22; 1Sam 2:12; 10:27; 1Fal 21:10-13; 2Nya 13:7; 2Sam 19:43Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti,

“Hatuna fungu katika Daudi,

wala hatuna sehemu

katika mwana wa Yese!

Kila mtu aende hemani mwake,

enyi Israeli!”

220:2 Mit 17:14Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.

320:3 2Sam 15:16; 16:21-22Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.

420:4 2Sam 17:25; 19:13Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.” 5Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.

620:6 2Sam 21:17; 1Sam 26:6; 2Sam 18:2; 11:11; 1Fal 1:33Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.” 720:7 1Sam 30:14; 2Sam 15:18; 1Fal 1:38; 2Sam 8:18Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.

820:8 Yos 9:3; 2Sam 2:18Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.

920:9 Mt 26:49; Lk 22:47; Mwa 4:8; 2Sam 2:23; 3:27; 1Fal 2:5Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu. 1020:10 Amu 3:21; 2Sam 3:27; 1Fal 2:5Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.

11Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!” 1220:12 2Sam 2:23Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake. 13Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.

1420:14 Hes 21:16; 1Fal 15:20; 2Fal 15:29; 2Nya 16:4Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata. 1520:15 1Fal 15:20; 2Fal 15:29; Isa 37:33; Yer 6:6; 32:24; Lk 19:43Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini, 1620:16 2Sam 14:2mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.” 17Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?”

Akamjibu, “Ndiye mimi.”

Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”

18Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri. 1920:19 Kum 2:26; 1Sam 26:19; 2Sam 21:3Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”

20Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu. 2120:21 2Sam 4:8Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.”

Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”

2220:22 Mhu 9:13-14; 7:19Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.

2320:23 2Sam 2:28; 8:16-18; 24:2Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi; 2420:24 1Fal 4:6; 5:14; 12:18; 2Nya 10:18; 2Sam 8:16; 1Fal 4:3Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu; 2520:25 1Sam 2:35; 2Sam 8:17Sheva20:25 Sheva mahali pengine ameitwa Shausha (1Nya 18:16; 1Fal 4:3). alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani; 2620:26 2Sam 23:38na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

撒母耳記下 20:1-26

示巴反叛大衛

1有一個無賴名叫示巴,是便雅憫比基利的兒子,當時剛好在吉甲。他吹響號角,大喊:「我們與大衛毫無關係,耶西兒子的產業沒有我們的份。以色列人啊,各自回家去吧!」 2於是,以色列人都離開了大衛,跟隨了比基利的兒子示巴。但猶大人仍然緊緊跟隨他們的王,從約旦河一直來到耶路撒冷3大衛回到耶路撒冷的宮裡,把從前留下來看守王宮的十個妃嬪關進冷宮,供養她們,卻不再和她們同房。她們像寡婦一樣在軟禁中度過餘生。

4王對亞瑪撒說:「你要在三天內招聚猶大人,跟他們一起來見我。」 5亞瑪撒就去招聚猶大人,但他超過了王所定的期限。 6大衛亞比篩說:「現在比基利的兒子示巴給我們帶來的危害恐怕比押沙龍還要大。你帶領我的部下去捉拿他,免得他佔據了堅固的城池,得以逃脫。」

7於是,約押的部下和基利提人、比利提人,以及所有的勇士都跟隨亞比篩離開耶路撒冷,去追趕比基利的兒子示巴8他們來到基遍的巨石旁,見亞瑪撒迎面而來。約押當時身穿戰袍,腰間佩刀,他迎上去的時候,刀從鞘中滑落出來。 9約押亞瑪撒說:「兄弟,你好嗎?」他用右手抓住亞瑪撒的鬍子,親吻他。 10亞瑪撒毫無防備,被約押一刀刺入肚子,肚破腸流而死。然後,約押和他兄弟亞比篩繼續追趕比基利的兒子示巴

11約押的一個部下站在亞瑪撒的屍體旁邊說:「擁護約押大衛的人來跟隨約押吧!」 12亞瑪撒的屍體倒在路中間的血泊中。那人見眾人駐足圍觀,便把屍體從路上拖到田裡,扔了一件衣服蓋上。 13屍體搬走以後,眾人都跟隨約押去追比基利的兒子示巴

14示巴走遍以色列各支派,一直到伯·瑪迦亞比拉城。他的本族比利人都聚集起來跟隨他。 15約押率大軍來到伯·瑪迦,把示巴圍困在亞比拉城內,他們修築攻城的高臺,撞擊城牆,要摧毀它。 16有一個聰明的婦人從城上喊:「請聽我說!請聽我說!請約押到這邊來,我有話要對他說。」 17約押就走上前去,那婦人問道:「你是約押嗎?」約押答道:「我就是。」婦人說:「請聽婢女說幾句。」約押說:「你說吧!」 18婦人說:「古時候人們常說,『有事到亞比拉去請教,問題都會解決。』 19我們這座城的人在以色列素來熱愛和平、忠心耿耿,你卻要毀滅這座大城。你為什麼要吞掉耶和華的產業?」 20約押答道:「我根本不想吞掉或毀滅這城。 21事情不是這樣。以法蓮山區比基利的兒子示巴背叛大衛王,你們只要把他交出來,我就撤退。」那婦人說:「我們一定把他的首級從城上拋下來給你。」 22婦人把自己的良策告訴眾人,他們便把比基利的兒子示巴的頭割下來,拋給約押約押就吹響號角令軍隊各自回家,自己回耶路撒冷見王。

23約押負責統率以色列全軍;耶何耶大的兒子比拿雅統管基利提人和比利提人; 24亞多蘭管理服勞役的;亞希律的兒子約沙法做史官; 25示法做書記;撒督亞比亞他做祭司; 26雅珥以拉大衛的祭司。