2 Samweli 19 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

2 Samweli 19:1-43

Yoabu Amkemea Mfalme

1Yoabu akaambiwa, “Mfalme analia na kumwombolezea Absalomu.” 2Kwa jeshi lote, ushindi wa siku ile ukageuka kuwa maombolezo, kwa sababu siku ile vikosi vilisikia ikisemwa, “Mfalme anahuzunika kwa ajili ya mwanawe.” 3Siku ile watu wakaingia mjini kimya kama vile waingiavyo kwa aibu watu waliokimbia kutoka vitani. 419:4 2Sam 15:30; 18:33; 1Sam 4:12Mfalme akafunika uso wake akalia kwa sauti, akisema, “Ee mwanangu Absalomu! Ee Absalomu, mwanangu, mwanangu!”

5Kisha Yoabu akaingia ndani ya nyumba ya mfalme na kusema, “Leo umewaaibisha watu wako wote, waliookoa maisha yako, maisha ya wanao na binti zako, maisha ya wake zako na masuria wako. 6Unawapenda wale wanaokuchukia, na unawachukia wale wanaokupenda. Leo umeonyesha wazi kwamba majemadari wako na watu wao hawana maana kwako. Naona kwamba ungefurahi kama Absalomu angekuwa hai leo na sisi sote tuwe tumekufa. 719:7 Mit 14:28Sasa utoke nje ukawatie moyo watu wako. Naapa kwa Bwana kwamba ikiwa hutatoka nje, hakuna mtu atakayesalia pamoja nawe ifikapo leo jioni. Hii itakuwa mbaya zaidi kwako kuliko maafa yote yaliyokupata tangu ujana wako hadi sasa.”

819:8 2Sam 15:2; Rut 4:1; 2Sam 18:4, 24; 2Fal 14:12; 1Fal 12:16Kwa hiyo mfalme akaondoka akaketi kitini pake penye lango. Watu walipoambiwa, “Mfalme ameketi langoni,” watu wote wakamjia.

Daudi Arudi Yerusalemu

Wakati huo, Waisraeli walikuwa wamekimbilia nyumbani kwao. 919:9 2Sam 8:1-14; 15:14; 5:18; 1Sam 17:1; 18:1Katika makabila yote ya Israeli, watu walikuwa wanabishana wao kwa wao, wakisema, “Mfalme alituokoa kutoka mikononi mwa adui zetu; ndiye alituokoa kutoka mikononi mwa Wafilisti. Lakini sasa mfalme ameikimbia nchi kwa sababu ya Absalomu, 10naye Absalomu, tuliyemtia mafuta atutawale, amekufa vitani. Basi mbona hamsemi lolote kuhusu kumrudisha mfalme?”

1119:11 2Sam 15:24Mfalme Daudi akapeleka ujumbe huu kwa makuhani Sadoki na Abiathari, kusema: “Waulizeni wazee wa Yuda, ‘Kwa nini mwe wa mwisho kumrudisha mfalme katika jumba lake la kifalme, maadamu kile kinachosemwa katika Israeli yote kimemfikia mfalme katika makao yake? 1219:12 Mwa 2:23; Amu 9:2; 2Sam 5:1Ninyi ni ndugu zangu, nyama yangu na damu yangu mwenyewe. Kwa hiyo kwa nini mwe wa mwisho kumrudisha mfalme?’ 1319:13 2Sam 17:25; Mwa 29:14; Rut 1:17; 2Sam 2:13; 1Fal 8:16; 1Nya 2:16; 17:12, 18; 1Fal 19:2Nanyi mwambieni Amasa, ‘Je, wewe si nyama yangu mwenyewe na damu yangu? Mungu na anishughulikie, tena kwa ukali, kama kuanzia sasa na kuendelea wewe si jemadari wa jeshi langu mahali pa Yoabu.’ ”

1419:14 Amu 20:1; Za 110:2-3; Mdo 4:32Aliipata mioyo ya watu wote wa Yuda kama vile walikuwa mtu mmoja. Wakapeleka ujumbe kwa mfalme, kusema, “Rudi, wewe na watu wako wote.” 1519:15 1Sam 11:15; Yos 5:9Ndipo mfalme akarudi, akaenda hadi kufikia Mto Yordani.

Basi watu wa Yuda walikuwa wamekuja mpaka Gilgali ili kutoka kwenda kumlaki mfalme na kumvusha Mto Yordani. 1619:16 2Sam 16:5-13; 1Fal 2:8Shimei mwana wa Gera, wa kabila la Benyamini kutoka Bahurimu, akaharakisha kuteremka pamoja na watu wa Yuda ili kumlaki Mfalme Daudi. 1719:17 2Sam 9:2; Mwa 43:16; 2Sam 16:1-2Pamoja naye walikuwepo Wabenyamini elfu moja wakiwa wamefuatana na Siba, msimamizi wa nyumba ya Sauli, pia wanawe kumi na watano, na watumishi ishirini. Wakaharakisha kwenda Yordani, mahali mfalme alipokuwa. 18Wakavuka kivuko ili kuwachukua watu wa nyumbani mwa mfalme ili kuwavusha na kufanya kila kitu alichotaka.

Shimei mwana wa Gera alipovuka Yordani, akaanguka kifudifudi mbele ya mfalme, 1919:19 2Sam 16:6-8; 1Sam 22:13; Za 32:2; Rum 4:6-8; 2Kor 5:19; Mit 28:13; Mt 5:25; 2Sam 16:5-6; 13:33na kumwambia, “Bwana wangu na asinihesabie hatia. Usikumbuke jinsi mtumishi wako alivyofanya kosa siku ile bwana wangu mfalme alipoondoka Yerusalemu. Mfalme aliondoe moyoni mwake. 2019:20 2Sam 16:5Kwa maana mimi mtumishi wako najua nimefanya dhambi, lakini leo nimekuja hapa kama wa kwanza wa nyumba yote ya Yosefu kushuka na kumlaki bwana wangu mfalme.”

2119:21 1Sam 26:6; Kut 22:28; 1Sam 12:3; 26:9; 2Sam 16:7-8; Mhu 10:20; Mdo 23:5; 2Pet 2:10-11; Yud 8Ndipo Abishai mwana wa Seruya akasema, “Je, Shimei hapaswi kuuawa kwa ajili ya hili? Alimlaani mpakwa mafuta wa Bwana.”

2219:22 2Sam 2:18; 16:10; 1Sam 11:13; 16:8; Mt 8:29Daudi akajibu, “Mimi nina nini nanyi, enyi wana wa Seruya? Leo hii mmekuwa adui zangu! Je, leo kuna yeyote atakayeuawa katika Israeli? Je, mimi sijui kuwa leo ndimi mfalme katika Israeli yote?” 2319:23 1Fal 2:8, 42Basi mfalme akamwambia Shimei, “Hutakufa.” Naye mfalme akamwahidi kwa kiapo.

2419:24 2Sam 4:4; 9:6-10Pia Mefiboshethi mwana wa Sauli akashuka kwenda kumlaki mfalme. Hakuwa amenawa miguu wala kunyoa ndevu zake wala kufua nguo zake tangu siku mfalme alipoondoka Yerusalemu mpaka siku aliporudi ile salama. 2519:25 2Sam 16:17Wakati alipotoka Yerusalemu kuja kumlaki mfalme, mfalme akamuuliza, “Mefiboshethi, kwa nini hukufuatana nami?”

2619:26 Law 21:18; 2Sam 9:2Akasema, “Bwana wangu mfalme, maadamu mimi mtumishi wako ni kiwete, nilisema, ‘Nitandikiwe punda wangu, nimpande, ili niweze kwenda pamoja na mfalme.’ Lakini Siba mtumishi wangu akanisaliti. 2719:27 1Sam 29:9; 2Sam 14:17-20; 16:3; Za 15:3; 63:11; Mit 21:6; 26:28; Yer 9:4-5Naye amemchongea mtumishi wako kwa bwana wangu mfalme. Bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu, kwa hiyo fanya lolote linalokupendeza. 2819:28 1Sam 25:2; 2Sam 17:27; 9:7-13Wazao wote wa baba yangu hawastahili kitu kingine isipokuwa kifo kutoka kwa bwana wangu mfalme, lakini ulimpa mtumishi wako nafasi miongoni mwa wale waliokula mezani pako. Je, ninayo haki gani kumwomba mfalme zaidi ya hayo?”

2919:29 Kum 19:16-21; Za 82:2; 101:1-8; Mit 29:4Mfalme akamwambia, “Kwa nini useme zaidi? Naamuru wewe na Siba mgawanye mashamba.”

30Mefiboshethi akamwambia mfalme, “Mruhusu achukue kila kitu, kwa kuwa sasa bwana wangu mfalme amerudi nyumbani salama.”

3119:31 Za 90:10; 2Nya 35:25; Ezr 2:65; Mhu 2:8; 12:1; 2Sam 15:33; 1Fal 2:7; Neh 7:63Barzilai, Mgileadi, pia akashuka kutoka Rogelimu ili kuvuka Yordani pamoja na mfalme na kumsindikiza kutoka huko. 3219:32 2Sam 17:27Basi Barzilai alikuwa mzee sana mwenye umri wa miaka themanini. Alikuwa amempatia mfalme mahitaji wakati alipokuwa anaishi huko Mahanaimu, kwa kuwa alikuwa mtu tajiri sana. 33Mfalme akamwambia Barzilai, “Vuka pamoja nami na ukae nami huko Yerusalemu, nami nitakupatia mahitaji yako.”

3419:34 Mwa 47:9; Za 39:4-5; Yak 4:14Lakini Barzilai akamjibu mfalme, “Je, nitaishi miaka mingine mingapi, hata nipande kwenda Yerusalemu pamoja na mfalme? 3519:35 Mwa 49:29; Yer 41:17; 1Fal 2:7; Za 90:10; Mhu 12:3-6Sasa nina miaka themanini. Je, naweza kutofautisha kati ya lililo jema na lililo baya? Je, mtumishi wako anaweza kujua ladha ya kile anachokula au anachokunywa? Je, bado naweza kusikiliza sauti za waimbaji wa kiume na za wanawake? Kwa nini mtumishi wako aongeze mzigo kwa bwana wangu mfalme? 36Mtumishi wako atavuka Yordani pamoja na mfalme kwa umbali mfupi tu, lakini kwa nini mfalme anizawadie kwa namna hii? 3719:37 Mwa 49:29; Yer 41:17; 1Fal 2:7Mruhusu mtumishi wako arudi, ili mimi nikafie katika mji wangu mwenyewe karibu na kaburi la baba yangu na mama yangu. Lakini yupo hapa mtumishi wako Kimhamu. Mruhusu avuke pamoja na bwana wangu mfalme. Mtendee lolote linalokupendeza.”

38Mfalme akamwambia Barzilai, “Kimhamu atavuka Yordani pamoja nami, nami nitamtendea lolote litakalokupendeza. Nawe kitu chochote unachotaka kutoka kwangu nitakutendea.”

3919:39 Mwa 47:7; 31:55; 14:19; Kut 39:43; Yos 22:6; 1Sam 2:20Kwa hiyo watu wote wakavuka Yordani, kisha mfalme akavuka. Mfalme akambusu Barzilai na kumbariki; Barzilai akarudi nyumbani kwake.

40Mfalme alipovuka kwenda Gilgali, Kimhamu akavuka pamoja naye. Vikosi vyote vya Yuda na nusu ya vikosi vya Israeli vilimvusha mfalme.

4119:41 Amu 8:1; 12:1; 2Sam 19:15Baada ya kitambo kidogo watu wote wa Israeli wakaja kwa mfalme na kumwambia, “Kwa nini ndugu zetu, watu wa Yuda, wamemrudisha mfalme kwa siri bila kutushirikisha, na kumvusha ngʼambo ya Yordani, yeye na nyumba yake, pamoja na watu wake wote?”

4219:42 2Sam 19:12; Rut 4:12; 1Nya 2:3-15; Za 78:68-70Watu wote wa Yuda wakawajibu watu wa Israeli, “Tulifanya hivi kwa sababu mfalme ni jamaa yetu wa karibu. Kwa nini mnakasirikia jambo hili? Je, tumekula kitu chochote cha mfalme? Je, tumejichukulia kitu chochote kwa ajili yetu wenyewe?”

4319:43 2Sam 5:1; 1Fal 11:30-31Ndipo watu wa Israeli wakawajibu watu wa Yuda, “Tunayo haki mara kumi kwa mfalme; sisi tunahusika zaidi na Daudi kuliko ninyi. Kwa nini basi mnatudharau? Je, hatukuwa wa kwanza kuzungumza kuhusu kumrudisha mfalme nyumbani?”

Lakini watu wa Yuda wakajibu kwa ukali hata zaidi kuliko watu wa Israeli.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

撒母耳記下 19:1-43

約押勸告大衛

1有人告訴約押,說:「王在為押沙龍哀傷痛哭。」 2士兵們聽說王為押沙龍哀痛,勝利的歡騰頓時變為一片哀愁。 3那一天,眾人都靜悄悄地回城去,好像敗兵一樣羞愧。 4王仍掩面痛哭:「我兒押沙龍啊!押沙龍!我兒!我兒啊!」 5約押就進到屋裡,對王說:「你的僕人們救了你和你妻妾兒女的性命,你今天卻使他們感到羞愧。 6仇視你的人,你倒去愛他;那些愛你的人,你反憎惡他們。這表明我王的心中根本沒有我們這些將領和部下。如今我明白了,要是死去的不是押沙龍而是我們,你就高興了。 7你現在應該出去安撫士兵們。我憑耶和華起誓,如果你不這樣做,今晚必無一人再追隨你。那將是你一生所遭遇的最大災難!」 8於是王出去坐在城門口,眾人聽說後,都來到他面前。這時,跟隨押沙龍以色列人都各自逃回家去了。

大衛返回耶路撒冷

9以色列各支派的人都在紛紛議論:「王曾把我們從眾仇敵和非利士人手中救出來。如今他為了躲避押沙龍而逃離本國。 10我們膏立為王的押沙龍已經死了,為什麼無人說請王回來呢?」

11大衛王派人去對祭司撒督亞比亞他說:「你們去問猶大的長老,『全以色列已經準備迎接王回宮,你們為什麼遲遲沒有反應? 12你們是王的弟兄,是王的骨肉,為什麼遲遲沒有迎接王回宮?』 13你們也要對亞瑪撒說,『你是我的骨肉,要是我不立你為元帥取代約押,願上帝重重地處罰我。』」 14王的這番話打動了所有猶大人的心,他們派人去請王和王的臣僕回來。

15王便啟程回宮。他來到約旦河時,猶大人都到吉甲來迎接他,要護送他過河。 16來自巴戶琳便雅憫基拉的兒子示每也急忙跟著猶大人趕來迎接大衛王, 17有一千便雅憫人跟示每一起去迎接大衛王。掃羅的僕人洗巴帶著十五個兒子和二十個僕人也趕到約旦河。 18他們渡到河對面幫助王的家眷過河,為王效勞。王正要過河的時候,基拉的兒子示每就俯伏在他面前, 19說:「求我主饒恕僕人的罪過!僕人在我主我王離開耶路撒冷時所犯的罪,求我王不要記在心上。 20僕人自知有罪,所以今天我是整個約瑟家族中第一個迎接我主我王的人。」 21洗魯雅的兒子亞比篩說:「示每曾經咒罵耶和華所膏立的君王,難道不應該處死他嗎?」 22大衛說:「洗魯雅的兒子,不要管我的事。你今天是在跟我作對。今天在以色列怎麼可以處死人呢?難道我不知道今天我是以色列的王嗎?」 23於是大衛起誓不殺示每

24掃羅的孫子米非波設也來迎接王。從王離開那天,直到大衛平安回來之日,他沒有修過腳,沒有剃過鬍子,也沒有洗過衣服。 25他到耶路撒冷來迎接王,王問他:「米非波設,當時你為什麼不跟我一起走呢?」 26米非波設答道:「我主我王,我是瘸腿的,我本想預備一頭驢騎著與我王同去,是我的僕人洗巴欺騙了我。 27他在我主我王面前譭謗我。我主我王就像上帝的天使,請王定奪。 28我父全家在我主我王面前都是該死的,但王卻讓我與王同席吃飯,我還能向王要求什麼呢?」 29王對他說:「不要再提這事了,我決定讓你和洗巴平分土地。」 30米非波設說:「把土地都給他吧,我主我王平安地回來就好了。」

31基列巴西萊也從羅基琳下來護送王過約旦河,然後送王上路。 32那時,巴西萊已經是八十高齡了。王留在瑪哈念的時候,他曾供應王食物,因為他非常富有。 33王對巴西萊說:「你跟我一同回耶路撒冷,我會照顧你。」 34巴西萊說:「我何必跟王一同去耶路撒冷呢?我還能活多久呢? 35我已經八十歲了,美醜難分,食不知味,樂不辨音,何必為我主我王添麻煩呢? 36僕人只不過是陪王過約旦河,王何必給我這麼大的賞賜呢? 37請准我回去,我好死在故鄉,葬在父母的墓旁。這裡有王的僕人金罕,讓他跟我主我王一起去。你看怎麼好,就怎麼對待他吧。」 38王說:「金罕可以跟我去,我會照你的心願待他。無論你有什麼要求,我都會答應你。」 39王和眾人過了約旦河以後,就親吻巴西萊,為他祝福。巴西萊返回了家鄉。

40王過河後,來到吉甲金罕跟隨著他。護送王的有猶大的士兵和半數的以色列士兵。 41後來,所有的以色列人來見王,說:「為什麼我們的弟兄猶大人偷偷地送王、王的家眷和王的部下渡河?」 42猶大人答道:「我們這樣做是因為王是我們的親族。你們為什麼生氣呢?難道我們吃了王的供應,得了什麼禮物嗎?」 43以色列人說:「但我們和王有十份的情分,我們在大衛身上比你們更有份。你們為什麼輕視我們?難道不是我們首先提出要請王回來的嗎?」

猶大人的態度比以色列人還要強硬。