2 Nyakati 33 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

2 Nyakati 33:1-25

Manase Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 21:1-18)

133:1 2Fal 21:1; 1Nya 3:13Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na mitano. 233:2 Yer 15:4; Kum 18:9; Law 18:24-30; 2Nya 28:3; 2Fal 17:11-15Akafanya maovu machoni pa Bwana, akafuata desturi za machukizo za mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli. 333:3 Kum 16:21-22; 2Nya 24:18; 2Fal 23:5-11; Kum 17:3; 2Nya 30:14; 2Fal 18:4; Yer 8:2; Sef 1:2Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake, alikuwa amepabomoa, pia akasimamisha madhabahu za Mabaali na nguzo za Maashera. Akalisujudia jeshi lote la angani na kuliabudu. 433:4 2Nya 7:16; 1Fal 8:29; Kum 12:11Akajenga madhabahu katika Hekalu la Bwana ambamo Bwana alikuwa amesema, “Jina langu litadumu Yerusalemu milele.” 533:5 2Nya 4:9Katika nyua zote mbili za Hekalu la Bwana akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la angani. 633:6 Law 18:21; Kum 18:10; Kut 22:18; Law 19:31; 1Sam 28:1333:6 2Nya 28:3; Eze 23:37; 2Fal 21:6Akawatoa wanawe kuwa kafara kwa kuwapitisha katika moto katika Bonde la Ben-Hinomu, akafanya ulozi, uaguzi na uchawi, akataka ushauri kwa wenye pepo wa utambuzi na wenye kuwasiliana na mizimu. Akafanya maovu mengi machoni pa Bwana, akaichochea hasira yake.

733:7 2Nya 7:16; Za 132:14Akachukua ile sanamu aliyoichonga na kuiweka katika Hekalu la Mungu ambalo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele. 833:8 2Sam 7:10Sitaifanya tena miguu ya Waisraeli iondoke tena katika nchi niliyowapa baba zenu, ikiwa watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru kuhusu sheria zote, maagizo na amri zilizotolewa kwa mkono wa Mose.” 933:9 Yer 15:4; Eze 5:7Lakini Manase akawaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu katika upotovu, kiasi kwamba walifanya maovu mengi kuliko mataifa ambayo Bwana aliwaangamiza mbele ya Waisraeli.

1033:10 Neh 9:29; Yer 25:4Bwana akasema na Manase pamoja na watu wake, lakini hawakumjali. 1133:11 Kum 28:36; Ay 36:8; Za 107:10-11Hivyo Bwana akaleta juu yao majemadari wa jeshi la mfalme wa Ashuru, ambao walimchukua Manase kwenda kifungoni, wakaweka ndoana katika pua yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli. 1233:12 2Nya 32:26; 1Pet 5:6; Yer 31:18-20; Lk 15:16-18; Kum 4:30-31; Za 118:5; Hos 5:15; Yn 2:2; Mik 6:9; Kut 10:3; Lk 18:4; 2Nya 32:16Katika dhiki yake akamsihi Bwana Mungu wake na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake. 1333:13 1Nya 5:20; Ezr 8:23; Mao 3:55-56; Za 142:1-7; 9:16; Dan 4:25Naye alipomwomba, Bwana akaguswa na kule kusihi kwake na akasikiliza kilio chake, kwa hiyo akamrudisha Yerusalemu na kwenye ufalme wake. Ndipo Manase akatambua kwamba Bwana ndiye Mungu.

1433:14 1Fal 1:33; Neh 3:3; 2Nya 27:3; Neh 3:26Baadaye akajenga ukuta wa nje wa Mji wa Daudi, magharibi mwa chemchemi ya Gihoni katika bonde, hadi kufikia ingilio la Lango la Samaki na akakizunguka kilima cha Ofeli, pia akaufanya kuwa mrefu zaidi. Akawaweka majemadari katika miji yote ya Yuda iliyokuwa imejengewa ngome.

1533:15 2Fal 23:12Akaondolea mbali miungu ya kigeni na kuondoa sanamu kutoka Hekalu la Bwana pamoja na madhabahu zote alizozijenga katika kile kilima kilichojengwa Hekalu na katika Yerusalemu, akazitupa nje ya mji. 1633:16 Law 7:11-18Kisha akarudisha madhabahu ya Bwana na kutolea juu yake dhabihu za sadaka za amani pamoja na sadaka za shukrani, naye akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli. 1733:17 1Fal 22:43; 2Nya 32:12; 2Fal 15:4; 2Nya 15:17Lakini hata hivyo watu wakaendelea kutoa dhabihu mahali pa juu pa kuabudia miungu, lakini wakimtolea Bwana Mungu wao peke yake.

18Matukio mengine ya utawala wa Manase, maombi yake kwa Mungu wake na maneno aliyoambiwa na waonaji walionena naye kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli. 1933:19 2Nya 6:37; 2Fal 21; 17Maombi yake, pamoja na jinsi Mungu alivyoguswa na kusihi kwake, pia dhambi zake zote na kukosa kwake uaminifu pamoja na sehemu alizojenga mahali pa juu pa kuabudia miungu, kule kusimamisha nguzo za Ashera na sanamu kabla ya kujinyenyekeza kwake, yote yameandikwa katika kumbukumbu za waonaji. 2033:20 2Fal 21:18-20Manase akalala pamoja na baba zake akazikwa katika jumba lake la kifalme. Naye Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.

Amoni Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 21:19-26)

21Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili, alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili. 22Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya. Amoni akaabudu na kutoa dhabihu kwa sanamu zote alizokuwa ametengeneza Manase. 2333:23 Kut 10:3; 2Nya 7:14; Za 18:27; 147:6; Mit 3:34Lakini tofauti na Manase baba yake, hakujinyenyekeza mbele za Bwana, badala yake Amoni aliongeza hatia zaidi na zaidi.

2433:24 2Nya 24:25Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani. 2533:25 2Nya 22:1; 2Fal 21:23-24; 2Nya 25:27-28Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme mahali pake.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

歷代志下 33:1-25

猶大王瑪拿西

1瑪拿西十二歲登基,在耶路撒冷執政五十五年。 2他做耶和華視為惡的事,效法耶和華在以色列人面前趕走的外族人的可憎行徑。 3他重建他父親希西迦拆毀的邱壇,為巴力築造祭壇,製造亞舍拉神像,並祭拜和供奉天上的萬象。 4耶和華曾指著祂的殿說:「我的名必永遠在耶路撒冷,」他卻在耶和華的殿內建造異教的祭壇。 5他在耶和華殿的兩個院子裡為天上萬象建造祭壇。 6他還在欣嫩子谷把自己的兒子燒死,獻作祭物。他行邪術、占卜、觀兆,求問靈媒和巫師,做了許多耶和華視為惡的事,惹耶和華發怒。 7他雕刻神像,放在上帝的殿中。關於這殿,上帝曾對大衛和他兒子所羅門說:「我從以色列各支派中選擇了這殿和耶路撒冷,我的名要永遠立在這裡。 8只要以色列人謹遵我藉著摩西頒給他們的一切法度、律例和典章,我就不再把他們從我賜給他們祖先的土地上趕走。」 9瑪拿西誘使猶大人和耶路撒冷的居民作惡,比耶和華在以色列人面前所毀滅的各族更嚴重。

瑪拿西悔改

10耶和華警告瑪拿西和他的百姓,他們卻不肯聽從。 11所以,耶和華就差遣亞述王的將領來攻擊他們,他們捉住瑪拿西,把他用鉤子鉤著、用銅鏈鎖著押往巴比倫12在困苦中,瑪拿西祈求他的上帝耶和華的幫助,並且在他祖先的上帝面前極其謙卑。 13耶和華應允他的禱告,垂聽他的懇求,使他返回耶路撒冷繼續做王。瑪拿西這才明白耶和華是上帝。

14這事以後,瑪拿西重建大衛城的外牆,從谷中基訓泉的西邊直到魚門口,環繞俄斐勒,築高城牆。他又派將領駐紮猶大各堅城。 15瑪拿西將偶像和外族人的神像從耶和華的殿中除去,又把他在聖殿山和耶路撒冷築造的一切祭壇全部拆掉,扔在城外。 16他重建耶和華的祭壇,在上面獻平安祭和感恩祭,又吩咐猶大人事奉以色列的上帝耶和華。 17然而,眾人仍然在邱壇獻祭,只是獻給他們的上帝耶和華。

瑪拿西逝世

18瑪拿西其他的事、他向上帝的禱告和先見奉以色列的上帝耶和華的名對他說的話,都記在《以色列列王史》上。 19他的禱告,上帝的答覆,他在謙卑下來之前的罪惡和不忠,他在哪裡修築邱壇以及設立亞舍拉神像和其他偶像的事,都記在《先知書》33·19 《先知書》或譯《何賽的書》。上。 20瑪拿西與祖先同眠後,葬在宮內,他兒子亞們繼位。

亞們做猶大王

21亞們二十二歲登基,在耶路撒冷執政兩年。 22亞們像他父親瑪拿西一樣做耶和華視為惡的事。他祭拜和供奉他父親瑪拿西製造的一切偶像。 23可是,亞們沒有像他父親瑪拿西一樣在耶和華面前謙卑下來。相反,他犯的罪越來越多。 24他的臣僕謀反,在王宮裡殺了他。 25民眾殺死那些背叛亞們王的人,讓他兒子約西亞接續他作王。