2 Nyakati 29 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

2 Nyakati 29:1-36

Hezekia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 18:1-12)

129:1 1Nya 3:13; 2Nya 26:5; 2Fal 18:1Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria. 229:2 2Nya 28:1; 34:2Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.

329:3 2Fal 18:16; 2Nya 28:24; Mit 8:17Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati. 4Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki 529:5 Law 11:44; Neh 13:9; Efe 5:26-27; 1Nya 15:12; 2Nya 35:6; Eze 36:25; Mt 21:12-13; 1Kor 3:16-17; 2Kor 6:16na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu. 629:6 Eze 23:35; Dan 9:5-6; 1Nya 5:25; Eze 8:16; Yer 2:27Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao. 729:7 2Fal 16:17-18; 2Nya 28:24Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli. 829:8 Kum 28:25; 2Nya 24:18; Law 26:32; Eze 8:16; Yer 18:16; 1Fal 9:8; Yer 19:8; 29:18Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe. 929:9 2Nya 28:5-8, 17; Law 26:17Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka. 1029:10 2Fal 11:17; 2Nya 15:12; Neh 9:38; Ezr 10:3; 2Nya 23:16Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi. 1129:11 Hes 3:6; 8:6-14; 1Nya 15:2; 1Kor 6:9Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”

1229:12 Hes 3:17-20; 2Nya 31:15Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi:

Kutoka kwa Wakohathi,

Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria;

kutoka kwa Wamerari,

Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli;

kutoka kwa Wagershoni,

Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;

1329:13 1Nya 6:36kutoka kwa wana wa Elisafani,

Shimri na Yeieli;

kutoka kwa wana wa Asafu,

Zekaria na Matania;

14kutoka kwa wana wa Hemani,

Yehieli na Shimei;

kutoka kwa wana wa Yeduthuni,

Shemaya na Uzieli.

1529:15 1Nya 23:28; Isa 1:25; 2Nya 30:12Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana. 1629:16 2Sam 15:23Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni. 1729:17 1Fal 6:3Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.

18Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote. 1929:19 2Nya 28:24Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”

Ibada Hekaluni Yarejeshwa

20Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana. 2129:21 Law 4:13-14Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana. 2229:22 Law 4:18; Hes 18:17; Ebr 9:21; Law 8:14-24Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu. 2329:23 Law 4:15, 24Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu. 2429:24 Kut 29:36; Law 4:20-26; Kol 1:20Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.

2529:25 1Nya 28:19; 2Nya 8:14; 1Sam 22:5; 2Sam 24:11; 1Nya 16:4; 23:6; 25:6; 2Nya 30:12Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake. 2629:26 1Nya 15:16-24; 23:5; Hes 10:10; 2Nya 12:13; Amo 6:5; 1Nya 16:6Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.

2729:27 1Sam 16:16; 2Nya 23:18; 20:21Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli. 28Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.

2929:29 2Nya 20:18; Rum 14:11Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu. 3029:30 Za 32:11; Flp 4:4Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.

3129:31 Ebr 13:15-16; Kut 35:22; 25:2; Law 7:12; 2Nya 13:9Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.

32Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana. 33Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000. 3429:34 2Nya 35:11; Hes 8:15; 2Nya 30:3; Eze 44:11; 1Nya 29:17; Za 7:10Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani. 3529:35 Mwa 4:4; 35:14; Hes 15:5-10; Law 3:16; 7:11-21; Kut 29:13Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa.

Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya. 3629:36 Za 118:23; Mdo 2:41Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.

New Russian Translation

2-я книга Паралипоменон 29:1-36

Езекия — царь Иудеи

(4 Цар. 18:1–3)

1Езекии было двадцать пять лет, когда он стал царем, и правил он в Иерусалиме двадцать девять лет. Его мать звали Авия, она была дочерью Захарии. 2Он делал то, что было правильным в глазах Господа, как и его предок Давид.

Езекия очищает храм

3В первый месяц, на первом году своего правления, он открыл двери Господнего дома и починил их. 4Он привел священников и левитов, собрал их на площади с восточной стороны 5и сказал им:

— Слушайте меня, левиты! Освятитесь сегодня сами и освятите дом Господа, Бога ваших отцов. Выбросите из святилища всякую скверну. 6Наши отцы поступали беззаконно, делая зло в глазах Господа, нашего Бога, и оставили Его. Они отвернули свои лица от жилища Господа и повернулись к нему спиной. 7Они заперли двери притвора и погасили светильники. Они не возжигали благовоний и не приносили всесожжений в святилище Бога Израиля. 8За это Господень гнев обрушился на Иудею и Иерусалим. Он отдал их на позор, на опустошение и на посмеяние, как вы видите своими глазами. 9Поэтому наши отцы пали от меча, а наши сыновья, дочери и жёны в плену. 10Теперь я хочу заключить завет с Господом, Богом Израиля, чтобы Его пылающий гнев на нас прекратился. 11Мои сыновья, не будьте же беспечными, потому что Господь избрал вас служить Ему и возжигать благовония.

12И начали свое служение левиты:

из потомков Каафа —

Махат, сын Амасая, и Иоиль, сын Азарии;

из потомков Мерари —

Киш, сын Авдия, и Азария, сын Иегаллелела;

из потомков Гершона —

Иоах, сын Зиммы, и Еден, сын Иоаха;

13из потомков Элицафана —

Шимрий и Иеил;

из потомков Асафа —

Захария и Маттания;

14из потомков Емана —

Иехиил и Шимей;

из потомков Идутуна —

Шемая и Уззиил.

15Собрав своих братьев и освятившись, они пришли очищать Господень дом, как, следуя словам Господа, повелел царь. 16Священники прошли в святилище Господа, чтобы очистить его. Они вынесли во двор Господнего дома все нечистое, что нашли в доме Господа. Левиты взяли это и отнесли в долину Кедрон. 17Приступив к освящению в первый день первого месяца, они подошли к притвору дома Господа в восьмой день того же месяца. Еще восемь дней они освящали сам Господень дом и закончили на шестнадцатый день первого месяца.

18Они пришли к царю Езекии и доложили:

— Мы очистили весь Господень дом, жертвенник для всесожжений со всеми его принадлежностями и стол, на который кладут священный хлеб, со всеми его принадлежностями. 19Все предметы, которые во время своего правления убрал неверный царь Ахаз, мы приготовили и освятили. Они сейчас перед Господним жертвенником.

Освящение храма

20На следующий день, ранним утром, царь Езекия собрал начальников города и отправился в дом Господа. 21Они привели семь быков, семь баранов, семь ягнят и семь козлов, чтобы принести их в жертву за грех29:21 Или: как очистительную жертву, так же в ст. 23, 24. за царскую семью, за святилище и за всю Иудею. Царь велел священникам, потомкам Аарона, принести их в жертву на жертвеннике Господа. 22Быков закололи, и священники, взяв крови, окропили ею жертвенник. Затем закололи баранов и окропили жертвенник их кровью. Затем закололи ягнят и окропили жертвенник их кровью. 23А козлов, которые были предназначены в жертву за грех, поставили перед царем и собранием, и они возложили на них руки. 24Затем священники закололи козлов и принесли их кровь на жертвеннике как жертву за грех, чтобы искупить весь Израиль, потому что царь велел совершить всесожжение и принести жертву за грех за весь Израиль.

25Езекия поставил левитов с тарелками, лирами и арфами в доме Господа, по установлению Давида, царского провидца Гада и пророка Нафана. Это установление было дано Господом через Его пророков. 26Левиты стояли наготове с музыкальными инструментами Давида, а священники — с трубами.

27Езекия велел принести на жертвеннике всесожжение. Когда началось жертвоприношение, началось и пение Господу под голос труб и музыкальных инструментов Давида, царя Израиля. 28Всё собрание совершало поклонение, певцы пели, а трубачи трубили. Так продолжалось, пока жертвоприношение не было завершено.

29Когда жертвы были принесены, царь и все, кто был с ним, преклонили колени и поклонились. 30Царь Езекия со своими приближенными велел левитам славить Господа словами Давида и провидца Асафа. И они радостно пели хвалу, низко кланялись и поклонялись.

31Езекия сказал:

— Итак, вы посвятили себя Господу. Приступайте, несите жертвы и благодарственные приношения в Господень дом.

Собрание принесло жертвы и благодарственные приношения, а все, кто был к этому расположен, принесли и всесожжения.

32Жертв всесожжения, которые принесло собрание, было общим счетом: семьдесят быков, сто баранов, двести ягнят — всё это для всесожжения Господу. 33Других священных жертв было: шестьсот голов крупного и три тысячи голов мелкого скота. 34Но священников было слишком мало, чтобы освежевать все туши жертв всесожжения, и пока другие священники не освятились, их сородичи левиты помогали им, пока работа не была сделана, потому что левиты отнеслись к освящению добросовестнее29:34 Букв.: левиты в освящении были сердцем праведнее., чем священники. 35Жертв всесожжения и жира жертв примирения с жертвенными возлияниями, которыми сопровождались всесожжения, было в изобилии.

Так было восстановлено служение в Господнем доме. 36Езекия и весь народ радовались тому, что сделал для Своего народа Бог, ведь сделано это было так быстро.