2 Nyakati 24 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

2 Nyakati 24:1-27

Yoashi Akarabati Hekalu

(2 Wafalme 12:1-16)

124:1 2Fal 11:21; 12:1Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba. 224:2 2Nya 25:2; 26:5Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani. 3Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.

4Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana. 524:5 Kut 30:16; Mt 17:24; 1Nya 26:20; 11:1; 2Fal 12:4; 2Nya 29:3; 34:8Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.

624:6 Kut 35:21; Hes 1:50; Mdo 7:44; Hes 17:7-8; Kut 30:12-16; 2Fal 12:7Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”

724:7 2Nya 21:17; 22:3-4; Za 12:8Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.

824:8 2Fal 12:9Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana. 924:9 Kut 36:6Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani. 1024:10 Kut 25:2; 1Nya 29:3-9Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa. 1124:11 2Fal 12:10Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana. 1224:12 2Nya 34:11Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.

1324:13 Neh 4:7Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha. 1424:14 1Fal 7:50; 2Fal 12:13; Kut 29:38; Ebr 7:27; 1Pet 1:18-19; Ufu 5:9Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.

1524:15 Ay 5:26Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130. 1624:16 1Fal 2:10Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.

Uovu Wa Yoashi

1724:17 Mdo 20:29Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza. 1824:18 Yos 24:20; 1Fal 14:23; Yer 17:2; Yos 22:20; 2Nya 19:2; Amu 5:8; 2Sam 24:1; 2Nya 28:13; Hos 5:10Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu. 1924:19 Hes 11:29; Zek 1:4; 2Nya 36:15; Neh 9:26; Yer 7:25-26; 25:4; Lk 11:47-51Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.

2024:20 Amu 3:10; Mt 23:35; 1Nya 12:18; Hes 14:41; 2Nya 15:2; Kum 31:17; 2Nya 15:1-2; Amu 6:34; 1Sam 13:13-14; Kum 29:25-26; Yer 2:19Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’ ”

2124:21 Yos 7:25; Mdo 7:58-59; Neh 9:26; Yer 26:21; 20:2; Mt 23:35Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana. 2224:22 Mwa 9:5Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”

2324:23 2Fal 12:17-18Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski. 2424:24 2Nya 14:9; Law 26:23-25; Kum 28:25; 32:30; Isa 10:5; 30:17Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi. 2524:25 2Nya 21:20; 2Fal 12:18-20; Za 10:14Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.

2624:26 2Fal 12:21; Rut 1:4Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu. 27Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

New International Version

2 Chronicles 24:1-27

Joash Repairs the Temple

1Joash was seven years old when he became king, and he reigned in Jerusalem forty years. His mother’s name was Zibiah; she was from Beersheba. 2Joash did what was right in the eyes of the Lord all the years of Jehoiada the priest. 3Jehoiada chose two wives for him, and he had sons and daughters.

4Some time later Joash decided to restore the temple of the Lord. 5He called together the priests and Levites and said to them, “Go to the towns of Judah and collect the money due annually from all Israel, to repair the temple of your God. Do it now.” But the Levites did not act at once.

6Therefore the king summoned Jehoiada the chief priest and said to him, “Why haven’t you required the Levites to bring in from Judah and Jerusalem the tax imposed by Moses the servant of the Lord and by the assembly of Israel for the tent of the covenant law?”

7Now the sons of that wicked woman Athaliah had broken into the temple of God and had used even its sacred objects for the Baals.

8At the king’s command, a chest was made and placed outside, at the gate of the temple of the Lord. 9A proclamation was then issued in Judah and Jerusalem that they should bring to the Lord the tax that Moses the servant of God had required of Israel in the wilderness. 10All the officials and all the people brought their contributions gladly, dropping them into the chest until it was full. 11Whenever the chest was brought in by the Levites to the king’s officials and they saw that there was a large amount of money, the royal secretary and the officer of the chief priest would come and empty the chest and carry it back to its place. They did this regularly and collected a great amount of money. 12The king and Jehoiada gave it to those who carried out the work required for the temple of the Lord. They hired masons and carpenters to restore the Lord’s temple, and also workers in iron and bronze to repair the temple.

13The men in charge of the work were diligent, and the repairs progressed under them. They rebuilt the temple of God according to its original design and reinforced it. 14When they had finished, they brought the rest of the money to the king and Jehoiada, and with it were made articles for the Lord’s temple: articles for the service and for the burnt offerings, and also dishes and other objects of gold and silver. As long as Jehoiada lived, burnt offerings were presented continually in the temple of the Lord.

15Now Jehoiada was old and full of years, and he died at the age of a hundred and thirty. 16He was buried with the kings in the City of David, because of the good he had done in Israel for God and his temple.

The Wickedness of Joash

17After the death of Jehoiada, the officials of Judah came and paid homage to the king, and he listened to them. 18They abandoned the temple of the Lord, the God of their ancestors, and worshiped Asherah poles and idols. Because of their guilt, God’s anger came on Judah and Jerusalem. 19Although the Lord sent prophets to the people to bring them back to him, and though they testified against them, they would not listen.

20Then the Spirit of God came on Zechariah son of Jehoiada the priest. He stood before the people and said, “This is what God says: ‘Why do you disobey the Lord’s commands? You will not prosper. Because you have forsaken the Lord, he has forsaken you.’ ”

21But they plotted against him, and by order of the king they stoned him to death in the courtyard of the Lord’s temple. 22King Joash did not remember the kindness Zechariah’s father Jehoiada had shown him but killed his son, who said as he lay dying, “May the Lord see this and call you to account.”

23At the turn of the year,24:23 Probably in the spring the army of Aram marched against Joash; it invaded Judah and Jerusalem and killed all the leaders of the people. They sent all the plunder to their king in Damascus. 24Although the Aramean army had come with only a few men, the Lord delivered into their hands a much larger army. Because Judah had forsaken the Lord, the God of their ancestors, judgment was executed on Joash. 25When the Arameans withdrew, they left Joash severely wounded. His officials conspired against him for murdering the son of Jehoiada the priest, and they killed him in his bed. So he died and was buried in the City of David, but not in the tombs of the kings.

26Those who conspired against him were Zabad,24:26 A variant of Jozabad son of Shimeath an Ammonite woman, and Jehozabad, son of Shimrith24:26 A variant of Shomer a Moabite woman. 27The account of his sons, the many prophecies about him, and the record of the restoration of the temple of God are written in the annotations on the book of the kings. And Amaziah his son succeeded him as king.